Mnaosema Hayati Dkt. Magufuli ndiye aliwaambia Wamachinga wajenge mabanda kila mahali, sikilizeni maagizo yake

mama D

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
19,760
35,205
Wamachinga ni wananchi kama wengine na wana haki ya kuishi mijini kama watanzania wengine. Mkitaka kuwahamisha hakikisheni mmeandaa mazingira ambayo hayataathiri biashara zao, maana hii ndio kazi inayowafanya wazilee familia zao na kusomesha watoto.

Hawa watu hawakupenda kuwa wamachinga kwahiyo wasionewe. Ma RC, DC, DED msitumie police vibaya kuwafukuza hawa, wala msiwapeleke ambako hawawezi kufanya biashara. Mkiona hamuwezi acheni kazi; nyie mmeteuliwa ila Mimi, Samia, Wabunge na Madiwani ndio tulizunguka kuomba kura na ndio tunajua shida za wananchi.

Serikali ndio ilitengeneza hawa wamachinga kwa kuwa na mifumo mibaya. Na hawa wamachinga wameonewa zaidi ya miaka 50 huku wanaoona wao ni wa class ya juu wakipendelewa. Sisi tunawasaidia hawa maskini.

Wamachinga na nyie mfuate taratibu. Msijenge mabanda kila mahali fanyeni biashara zenu bila kuathiri miji yetu - JPM.

Mnaosema JPM ndio aliwaambia wamachinga wajenge mabanda kila mahali sikilizeni maagizo yake halafu waulizeni hao viongozi wanaoshindwa kusimamia wananchi kwanini hawafuati maelekezo ya serikali.



Endelea kupumzika salama shujaa JPM

Rais wetu mama SSH kazi iendelee

Mungu ibariki Tanzania
 
Sasa mkuu unapendekeza waendelee kuchafua miji kwa kisingizio cha unyonge, mbona maeneo mengine wapo na wana maeneo yao, kwanini wapange vitu barabarani na mbele ya frame za watu, is that fair?

Angalia Nyerere road Mwanza na Kariakoo DSM palivyo pachafu, masoko yapo ila mradi tu wakae barabarani.. sio sawa
 
Sasa mkuu unapendekeza waendelee kuchafua miji kwa kisingizio cha unyonge, mbona maeneo mengine wapo na wana maeneo yao, kwanini wapange vitu barabarani na mbele ya frame za watu, is that fair?..
Hapo ndipo wakuu wa wilaya na wakurugenzi wanapotakiwa kuwajibika kwa kushindwa kutumia mamlaka na resources walizo nazo kuweka mambo sawa. Na sio kuwaangushia mzigo watu wanaotafuta riziki za watoto wao
 
Miji yetu imekuwa mihafu. Sio busara kuruhusu watu kufanya biashara zao kwenye kila maeneo. Kuna sehemu nyingine wanaziba njia kabisa. Hapo sasa wanafanya biashara gani?

Kwa mfano kidogo kidogo njia ya Sinza watu wameanza kuweka vibanda kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajiri ya kutembelea. Kabla hatijaziduka, watu wataanza kutembea barabarani kama magari
 
Miji yetu imekuwa mihafu. Sio busara kuruhusu watu kufanya biashara zao kwenye kila maeneo. Kuna sehemu nyingine wanaziba njia kabisa.
Hapo sasa wanafanya biashara gani? Kwa mfano kidogo kidogo njia ya Sinza watu wameanza kuweka vibanda kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajiri ya kutembelea. Kabla hatijaziduka, watu wataanza kutembea barabarani kama magari

Sikiliza hiyo clip ya kikao kabla ya kuweka comment ili uje na wazo linalojenga badala ya lawama
 
Wamachinga ni wananchi kama wengine na wana haki ya kuishi mijini kama watanzania wengine. Mkitaka kuwahamisha hakikisheni mmeandaa mazingira ambayo hayataathiri biashara zao, maana hii ndio kazi inayowafanya wazilee familia zao na kusomesha watoto.

Hawa watu hawakupenda kuwa wamachinga kwahiyo wasionewe. Ma RC, DC, DED msitumie police vibaya kuwafukuza hawa, wala msiwapeleke ambako hawawezi kufanya biashara. Mkiona hamuwezi acheni kazi; nyie mmeteuliwa ila Mimi, Samia, Wabunge na Madiwani ndio tulizunguka kuomba kura na ndio tunajua shida za wananchi.

Serikali ndio ilitengeneza hawa wamachinga kwa kuwa na mifumo mibaya. Na hawa wamachinga wameonewa zaidi ya miaka 50 huku wanaoona wao ni wa class ya juu wakipendelewa. Sisi tunawasaidia hawa maskini

Wamachinga na nyie mfuate taratibu. Msijenge mabanda kila mahali fanyeni biashara zenu bila kuathiri miji yetu - JPM

Mnaosema JPM ndio aliwaambia wamachinga wajenge mabanda kila mahali sikilizeni maagizo yake halafu waulizeni hao viongozi wanaoshindwa kusimamia wananchi kwanini hawafuati maelekezo ya serikali



Endelea kupumzika salama shujaa JPM

Rais wetu mama SSH kazi iendelee

Mungu ibariki Tanzania

Jf Moderator Naomba msiunganishe huu uzi kwingine

Rubbish
 
Sikiliza hiyo clip ya kikao kabla ya kuweka comment ili uje na wazo linalojenga badala ya lawama
Si lawama. Yes waliomba kura na machinga ni wapiga kura kama wapiga kura wengine. Issue hapa ni sheria na taratibu. Wote lazima tufuate sheria na taratibu
 
Si lawama. Yes waliomba kura na machinga ni wapiga kura kama wapiga kura wengine. Issue hapa ni sheria na taratibu. Wote lazima tufuate sheria na taratibu
Sheria gani inamzuia mmachinga kufanya biashara mijini??
 
Wamachinga ni wananchi kama wengine na wana haki ya kuishi mijini kama watanzania wengine. Mkitaka kuwahamisha hakikisheni mmeandaa mazingira ambayo hayataathiri biashara zao, maana hii ndio kazi inayowafanya wazilee familia zao na kusomesha watoto.

Hawa watu hawakupenda kuwa wamachinga kwahiyo wasionewe. Ma RC, DC, DED msitumie police vibaya kuwafukuza hawa, wala msiwapeleke ambako hawawezi kufanya biashara. Mkiona hamuwezi acheni kazi; nyie mmeteuliwa ila Mimi, Samia, Wabunge na Madiwani ndio tulizunguka kuomba kura na ndio tunajua shida za wananchi.

Serikali ndio ilitengeneza hawa wamachinga kwa kuwa na mifumo mibaya. Na hawa wamachinga wameonewa zaidi ya miaka 50 huku wanaoona wao ni wa class ya juu wakipendelewa. Sisi tunawasaidia hawa maskini

Wamachinga na nyie mfuate taratibu. Msijenge mabanda kila mahali fanyeni biashara zenu bila kuathiri miji yetu - JPM

Mnaosema JPM ndio aliwaambia wamachinga wajenge mabanda kila mahali sikilizeni maagizo yake halafu waulizeni hao viongozi wanaoshindwa kusimamia wananchi kwanini hawafuati maelekezo ya serikali



Endelea kupumzika salama shujaa JPM

Rais wetu mama SSH kazi iendelee

Mungu ibariki Tanzania

Jf Moderator Naomba msiunganishe huu uzi kwingine

Mama D! Nilikua nimekumiss sana!
 
Zipo sheria na taratibu za kuendesha miji ambazo zimewekwa pembeni. Njia ya wapita njia kwa miguu sio duka wala sio sehemu ya biashara. Unataka kusema huko sio kuvunja sheria?
Kuna mahali Rais Samia au Magufuli aliwahi kuwaambia wakatumie hizo njia?
Viongozi husika katika level ya kata, wilaya, mkoa, walifanyie kazi kama hawawezi waondoke waingie wanaoweza
 
Kuna mahali Rais Samia au Magufuli aliwahi kuwaambia wakatumie hizo njia?
Viongozi husika katika level ya kata, wilaya, mkoa, walifanyie kazi kama hawawezi waondoke waingie wanaoweza
Walioanza kuambiwa waende maeneo ya kufanya biashara wakaambiwa ole wake mtu awaguse. I think if we want our cities to be clean, machinga should have allocated area for their businesses. Haiwezekani wakawa wanafanya biashara popote na wasiguswe. Ni siasa ambazo zinania ya kuwatumia tu. Ipo siku wataondolewa akija mtu ambaye atataka miji ikae sawasawa. Tuanze mapema na sio kukaa kimya kama vile hakuna tatizo
 
Wamachinga wana haki ya kufanya biashara bila kubugudhiwa. Ila wawe na maeneo rasmi na yenye kuwa na wateja. Wasiruhusiwe kuweka biashara kila sehemu. Tukumbuke sisi sote tunawajibika kufanya mazingira na maisha yetu yawe salama na endelevu
 
Back
Top Bottom