Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,055
DISCLAIMER: Tamthiliya hii sio ya kimama kama wengi wanavyoichukulia. Ni historical fact so nikisikia watu wanawabeza wanaume kuitazama nabaki kusikitika tu. Nakumbuka niliisoma hii historia kwenye mafundisho ya dini miaka ya nyuma. Nikaja kuisoma tena kwa undani kutoka kwenye mtazamo wa kihistoria kuhusu tawala zilizotikisa ulimwengu - Ottoman ikiwemo. Ni historia ya kibabe sana na miamba iliyowahi kutikisa dunia hii. Tusiichukulie poa!
Back to the topic
Ni historia ya kusisimua sana. Naamini na tamthiliya nayo itakuwa vivyo hivyo. Huu ni utawala ambao umeacha alama kubwa kutokana na kutawaliwa na vituko kuliko tawala zote za Ottoman zilizopita. Ni visa vya mapenzi, urafiki na utawala.
Historia hii pia inahuzunisha sana. Vifo, usaliti, fitna vimetawala ndani ya hekalu la Mfalme.
Kwa mfano:
Matukio ya hivi karibuni
Sijajua Azam Two watatufikisha wapi lakini angalau nimeona wanaingia mule mule. So, natoa fursa kwa wanaopenda kujua yajayo, waniulize maswali nami nitajibu kwa kadri ya kumbukumbu zangu.
Poleni team Hurrem na team Pasha in advance.
Back to the topic
Ni historia ya kusisimua sana. Naamini na tamthiliya nayo itakuwa vivyo hivyo. Huu ni utawala ambao umeacha alama kubwa kutokana na kutawaliwa na vituko kuliko tawala zote za Ottoman zilizopita. Ni visa vya mapenzi, urafiki na utawala.
Historia hii pia inahuzunisha sana. Vifo, usaliti, fitna vimetawala ndani ya hekalu la Mfalme.
Kwa mfano:
Matukio ya hivi karibuni
- Mustafa atamuoa binti Hellena
- Nigar kalfa atafanikiwa kutoroshwa. Mtoto wake atakulia sehemu nyingine kwa kufichwa. Jina lake ataiwa Kadar/Kadir.
- Hurrem atamuagiza Rustem Pasha amuue suria Feruze. Rustem Pasha atagundua siri ya tattoo ya Feruze shingoni, atamwambia Hurrem naye atamwambia Sultan kisha suria huyo atafukuzwa.
- Ibarahim Pasha ataalikwa dinner/futari na kuuwawa na Mfalme Suleyman na kurithiwa nafasi yake na Ayas Pasha
- Mustafa atauwawa na Mfalme Suleiman kutokana na fitna za Hurrem, watu kumpenda na hofu ya kupinduliwa itakayomkumba Sultan.
- Hadija Sultan atajiua kwa hofu ya adhabu ya Sultan baada ya kufanya mchezo hatari wa kumuweka mateka Hurrem.
- Hurrem atafariki dunia kwa maradhi
- Watoto wa Hurrem watauwawa. Bayezid na Selim 2 watakuwa na bifu wakigombea madaraka. Jihangir atakufa kwa sonono kufuatia kifo cha kaka yake, Mustapha.
- Sultan Suleiman ataugua na kufariki dunia. Selim 2 (cha pombe) atamrithi.
Sijajua Azam Two watatufikisha wapi lakini angalau nimeona wanaingia mule mule. So, natoa fursa kwa wanaopenda kujua yajayo, waniulize maswali nami nitajibu kwa kadri ya kumbukumbu zangu.
Poleni team Hurrem na team Pasha in advance.