Mnalionaje Suala la Wanawake Kutaka Haki Sawa 50/50 Kijamii, Kiuchumi and Kisiasa

zagarinojo

JF-Expert Member
Jul 26, 2020
2,622
2,835
Habari wana Jamvi. Wataalamu wa vitabu vya dini wanasema mwanamke alitokea kwenye ubavu wa kushoto wa mwanaume katika uumbaji.

Ila tuachane na hayo kwanza walezi wakuu wa familia tunatambua kuwa ni wanawake na viongozi wakuu wa familia huwa ni wanaume hasa katika jamii zetu za Kiafrika.Lakini hili linatambulika na Dunia kwa ujumla.

Ila kwa siku za hivi karibuni wanawake wamekuwa wakipaza sauti na kudai uwepo wa haki sawa kati ya wanaume na wanawake(Gender Equality).Hii inamanisha haki sawa katika ugawaji wa kazi,fursa na ajira.

Kwa mfano siku chache zilizopita wanawake nchini Kenya wameibuka na kudai Kuwepo na idadi sawa ya wabunge bungeni yani nusu ya wabunge wawe wa kiume na nusu iliyobakia wawe wanawake(Gender Balance).

Takwimu zinaonesha kuna idadi(population) kubwa ya wanawake duniani kote ukilinganisha na idadi ya wanaume.
Ila kilio cha haki sawa hakijawahi kuisha kabisa licha ya idadi hiyo kubwa ya wanawake.

Wengine wamekuwa wakitoa mitazamo yao kuwa haiwezekani kabisa kuwepo kwa usawa(Gender Equality) kwa sababu ya mfumo dume wa nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania unaowafanya wanaume kuwa Superior zaidi ya Wanawake.

Wengine wamediriki kusema haiwezekani kwasababu ni asili ndio iko hivyo kuwa mwanamke siku zote atakuwa kiumbe dhaifu na atakuwa inferior kwa mwanaume.

Wengine wameamini kuwa hata maandiko yanalitambua hilo kuwa mwanamke atakuwa mtu wa kutii na atakuwa chini ya mume wake kwasababu ametoka katika ubavu wake wa kushoto.

Wanawake wanatumia nguvu kubwa kudai haki na usawa katika nyanja zote.Wakati jamii imeshindwa kuelewa tatizo liko wapi?

Mada hii ni pana sana Ila kwa kifupi tuanzie hapa
Kwanini wadai haki na usawa?
Je Hakuna haki na usawa Tanzania na Afrika Kwa ujumla?

Ni upi ushauri na mtazamo wako juu ya hili suala?
 
Unapokuwa na zaidi ya nusu ya wananchi hawana kipato na hawachangii chochote ktk ujenzi wa nchi ,maendeleo yanakuwa magumu kupatikana


TZ Kuna watu millioni 55,harafu unakuta milioni 35 ni wanawake,na hawana uwezo wa kiuchumi,yaani wanaume millioni 15,wazichange,walishe watu millioni 35!


Sasa ebu fikiria hao millioni 35!wakipewa uwezo wa kiuchumi,na wao wakachangia,nchi itaendelea haraka sana.
 
Katka Maisha Yangu Hakuna Kitu Nitakipinga Zaidi Ya Hiki!
Hata Kama Wataomba Haki Sawa, Ila Mwanamke Atabaki Kuwa Mwanamke Na Mwanaume Atabaki Kuwa Mwanaume!
 
Katka Maisha Yangu Hakuna Kitu Nitakipinga Zaidi Ya Hiki!
Hata Kama Wataomba Haki Sawa, Ila Mwanamke Atabaki Kuwa Mwanamke Na Mwanaume Atabaki Kuwa Mwanaume!
 
Wanawake wanatumia nguvu kubwa kudai haki na usawa katika nyanja zote.Wakati jamii imeshindwa kuelewa tatizo liko wapi?

Mada hii ni pana sana Ila kwa kifupi tuanzie hapa
Kwanini wadai haki na usawa?
Je Hakuna haki na usawa Tanzania na Afrika Kwa ujumla?

Ni upi ushauri na mtazamo wako juu ya hili suala?
Wanawake wa Kiafrika wanadai usawa kwenye nyanja zote kama ilivyo kwa nchi za Ulaya. Ila ukiwachunguza sana utagundua Wandai haki sawa ila majukumu kwa mwanaume tu, wao wanayakimbia. Wanataka wachape kazi wapate mshahara ila kula yao na watoto kwa ujumla pamoja na ulipaji wa bili zote za kila mwezi liwe jukumu la mme.

Hii ni tofauti kabisa na Ulaya wanapowaiga. Kwa Ulaya, suala la kununua chukula kwa familia sio jukumu la mme pekee au mke pekee. Yeyote anaweza kwenda supermarket na kukusanya mahitaji ya kutumia kwa wiki au siku kadhaa na akalipia pesa yake, na wala Hakuna kutegeana.

Nilikuwa siku moja kwa mgahawa fulani huko Europe, akaja mtu na mkewe kununua chakula (take away). Kila mmoja akaweka order yake. Ilipokuja ktk kulipia, mme akaanza kulipia (kwa kadi yake ya bank) na akaja mke naye akalipia bili yake. Kwa Wanawake wa kiswahili (waAfrika) angetaka alipiwe (akwepe jukumu) wakati huo huo anadai haki sawa.

Pia ukitoka out na binti wa kizungu, kanuni mama ni kuwa kila mmoja atajilipia gharama ya chakula na vinywaji atavyoagiza. Labda pafanyike makubaliano mengineyo...mfano mmoja alipie vyakula, mwingine vinywaji au mwanaume ampa ofa mwanamke au kinyume chake (mwanamke ampa ofa mwanaume)

Kwa kifupi wanawake wengi wa kiswahili (waAfrika) wanaopigania usawa wanasumbuliwa zaidi na umasikini tu. Ndio maana hutawasikia kuzungumzia majukumu kwa wote kama walivyo wenzao wa Ulaya.

Cc: cariha njoo huku my dear kuna uzi unakuhusu, uje utoe vidonge kwa wanaume na insecurities (huwa wapenda litumia sana neno hilo) zao.
 
nchini Kenya wameibuka na kudai Kuwepo na idadi sawa ya wabunge bungeni yani nusu ya wabunge wawe wa kiume na nusu iliyobakia wawe wanawake(Gender Balance).
Kwani izo nafazi zinagiwa kama pipi mpaka wasema wanataka wawe 50/50?
 
👉 Mada hii ni pana sana Ila kwa kifupi tuanzie hapa
Kwelu mada ni mtambuka sana hii kijaba wangu zagarinojo ila nimeipenda sana hii maana tutajifunza na kuelezana kila mtu anavyofahamu in/out dini na real life.

Kwa sasa dunia inatakiwa kugeuka chini juu ili kufikia malengo ambayo mwanadamu anayataka na huyu anaeyataka siyo mtu wa kawaida kwamba yatakuwa na amani, furaha au jambo lolote jema HAPANA.

Mpango wa 50/50 ulianzia pale bustani ya Eden ambapo bi mkubwa Hawa alitaka kuwa juu ya babu yetu Adam (huko mbele nitaeleza kwa undani zaidi) na siyo Beijing kama wengi wanavyodhani ila from there ndipo gonjwa la usawa limeendelea kuwa chronic kwa kila binadamu wa jinsia ya kike anayepuliziwa dawa iitwayo gender balance anakurupuka.

Hii 50/50 ina secret agenda ambayo haionekani machoni na inafanya kazi kwa watu wengi wanaotumikishwa pasipo wao kujua ili kufikia malengo.

Labda niseme, hii itafanikiwa japo kiuchumi nk hakuna mabadiliko yoyote japo italazimishwa kuonyesha mafanikio na ..
 
Sisi kina 'marioo' tunasema hivi hii mambo isitishwe mara moja


vvl
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom