Elections 2010 Mnakumbuka Pinda alivyomchulia Mpiganaji Zitto Kabwe?

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Hivi ile hadithi ya "2010 hautarudi bungeni" aliyoianzisha Waziri Mkuu asiye na sauti dhidi ya Kamanda Zito Kabwe, iliishia wapi?

Manake naskia Mzee Pinda alipita bila kupingwa, nikapatwa na hofu kwamba sasa kiama cha Kabwe kimefika.

Zito karudi Mjengoni au aliyosema mzee wa Mpanda yametimia?

Naomba kueleweshwa.
 
Lilikuwa dua la kuku, laana ya walaaniwa (kama chama), na kauli zisizoitakia mema nchi yetu kwa mtu kupinga waleta maendeleo bila kuwa na sera za maana. Alikuwa na lipi la maana kumuombea mwanajeshi huyu njaa? Wapo ndugu zake kadhaa waliowahi kushinikiza kwa mbwembwe kwamba kijana afukuzwe bungeni, eti kwa maneno yao ya uzushi, alisema uongo. Laana iliwarudia na sasa tunawatafuta bungeni kwa tochi, hatuwaoni. (Mfano Mudhihir Mudhihir). Enzi za wadanganyika zimeisha, wajifunze kujenga hoja sio longolongo
 
Lilikuwa dua la kuku, laana ya walaaniwa (kama chama), na kauli zisizoitakia mema nchi yetu kwa mtu kupinga waleta maendeleo bila kuwa na sera za maana. Alikuwa na lipi la maana kumuombea mwanajeshi huyu njaa? Wapo ndugu zake kadhaa waliowahi kushinikiza kwa mbwembwe kwamba kijana afukuzwe bungeni, eti kwa maneno yao ya uzushi, alisema uongo. Laana iliwarudia na sasa tunawatafuta bungeni kwa tochi, hatuwaoni. (Mfano Mudhihir Mudhihir). Enzi za wadanganyika zimeisha, wajifunze kujenga hoja sio longolongo


Mudhihir???

Kwishne
 
Nadhani ilikuwa wakati akizindua rasmi barabara fulani. Wananchi wa huko wamemthibitishia vinginevyo.
 
Back
Top Bottom