Kaka Pekee
JF-Expert Member
- Apr 3, 2018
- 336
- 559
Watanzania tusikubali propaganda za kijinga hizi.!!! Tamko la bunge La ulaya lina hoja nyingine zaidi ya 14 tofauti na ushoga, watu kupigwa risasi na kukosekana uchunguzi,watu kupotea na kukutwa kwenye viroba,sheria ngumu ya mitandao,chaguzi na wapinzani kunyanyaswa,kufunguliwa kesi za kisiasa na dola,kudorora kwa haki za binadamu, wanafunzi waliopata ujauzito kupata haki ya kuendelea kusoma na mambo mengine mengi.
Zimbabwe ya Mugabe alitumia propaganda ya mashamba kuwadanganya wananchi lakini nchi ilipozama sasa wanateseka wazimbambwe wote.
Acheni propaganda jibuni hoja zote zinazosababisha nchi inakosa sifa za kupata misaada kama zamani ilivyokua, mkiulizwa mnasema kuna vibaraka wa mabeberu na nyie mnajiita wazalendo baada ya mda mchache nyie wazalendo mnaenda airport kuwapokea hao mnaoita mabeberu mnawachezea na ngoma na kuwasafishia barabara .
Mlifanya propaganda kwenye sukari kwamba imefichwa na wafanyabiashara leo bei ya sukari imepanda mmenyamaza hamsemi chochote mwananchi wa kawaida anaumia semeni ukweli. Mpango jibuni hoja za Eu bila propaganda tusaidie nchi.
Zimbabwe ya Mugabe alitumia propaganda ya mashamba kuwadanganya wananchi lakini nchi ilipozama sasa wanateseka wazimbambwe wote.
Acheni propaganda jibuni hoja zote zinazosababisha nchi inakosa sifa za kupata misaada kama zamani ilivyokua, mkiulizwa mnasema kuna vibaraka wa mabeberu na nyie mnajiita wazalendo baada ya mda mchache nyie wazalendo mnaenda airport kuwapokea hao mnaoita mabeberu mnawachezea na ngoma na kuwasafishia barabara .
Mlifanya propaganda kwenye sukari kwamba imefichwa na wafanyabiashara leo bei ya sukari imepanda mmenyamaza hamsemi chochote mwananchi wa kawaida anaumia semeni ukweli. Mpango jibuni hoja za Eu bila propaganda tusaidie nchi.