Mnadhibiti vipi wizi katika ujenzi?

Kama unataka mafundi waaminifu nenda kachukue wapemba ambao hawajaingia dar.

Sio kwamba hakuna wapigaji Ila kwa kiasi kikubwa wazenj Ni watu waaminifu sana ukilinganisha na huku bara kwani kule wamekuzwa katika misingi ya dini wamefundwa kuwa na hofu ya mungu.

Bara watu wamepinda hawaogopi mungu Wala shetani kila wanachokifanya kwao Ni sawa tu.

Sema wazenj wavivu tu wamezembea kwa kwazi Ila katika suala la uaminifu nawapa 90%

Binafsi mm nilisimamia ujenz wa brother Wang chanika mafund walikua Ni kutoka Pemba hawakuhaw huiba hata kipande Cha mbao.
Ilifikia wakati vilivyokua vinabakia havina kazi Tena Ila wananirejeshea ukweli nikiwaona watu wa ajabu sana.

Niliwaamini kiasi kwamba nikawa nafanya Mambo yangu siku tatu sijapita malalamiko na huwez amini niliokoa hela nyingi sana kwenye bajet iliyokua imepangwa.

fundi alienipa ramani alinipa mahsab almost mil.35 mpaka kumalizia jengo Ila kupitia mafundi hao nimemtumia mil.29 tu mpaka finishing.hapo nimesev mil.6 ambazo zingepote kwa wapigaji.
 
Hata wewe wakati unatafuta hela ya kujengea kuna sehemu lazima ulipiga. Iwe ni ofisini bas ulifanya upigaji kwa madokezo ya uwongo na mambo kama za milungula lazma zilihusika. Kama mfanyabiashara bas ulipiga kwa namna yako hukutoa risiti, ulizidisha beii...uliuza na kununua magendo. Maisha yako hivyo, usimbane sana fundi lazima atakuibia tuuu. Japo hutakiwi ku relax ukaibiwa vingi.

Kama unaanza kujenga nyumba anza kujenga fensi kwanza kudhibiti utoroshaji wa vitu kokoto, mawe, tofali mbao, na vingine
Halafu mambo za "Matirio" inatakiwa kwenda fronti wewe "kabageini" dukani kanunue mwenyewe, fundi akisema cement kumi leta 8, bati mita 460 weka 410, marumaru box 100 weka 70.. mbao 320 weka 250... gypsum board 150 weka mia; vitu vikipelea unaongezea.
Yaaan hii ndio kitu naitumia mimi hadi sasa kwenye ujenzi wangu...kila kitu nanunua mwenyewe na bagaini mwenyewe fundi analetewa vifaaa...navyo nampelekea kidogo vikipelea naongeza..sema changamoto yake ni kwamba utagharamikia usafiri mara kwa mara ila sio mbaya maana unacho okoa ni kikubwa kuliko usafiri


Pili ni vema kuweka fensi mapema itakusaidia kuzuia utoroshaji wa vitu


Issue nyingine na sisi tuwe wadadisi ukiambia nahitaji kitu fulan kwa idadi kadhaa na bei ni shilingi kadhaaa usikubali moja kwa moja fanya udadisi

Mfano fundi wangu alinimbia mbao moja ya 2*4 ni 7000 sehemu fulan ...tuchukue hapo nikaenda kudadisi nikakuta mbao hiyo hiyo naipata kwa 5500


Kwenye issue mbao pia tunapigwa sana simpe fundi pesa....anaweza akakupa idadi sawa kabisa ila atapiga cha juuu
 
Tengeneza BOQ lipa kampuni ya ujenzi watakukabidhi funguo nyumba ikiwa imekamilika.

Labda jiulize bank wanaibaje na pesa zote zipo kwenye hesabu na kuna wasomi nguli wa mahesabu?
Tunapenda sana kutumia kampuni ila hela ngumu...unakuta ujenzi unafanya hata miaka 5 ..ukipata unafanya hili ...kampuni si watataka hela yao yote
 
Mungu saidia mwezi w 12 na anza ujenzi!! Ila mpk ss vitu vingi nimecheki mm mwenyewe. Yani macho macho nitasimamia mm mwenyewe. Ninacho pigania ni kupunguza kupigwa sanaaaa (mnoooo).
 
Back
Top Bottom