Mlolongo wa ajali za misafara ya Rais Kikwete - Nini kifanyike?

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
000000ajalikikwete.jpg

Rais Jakaya Kikwete akiteremka kwenye gari lake eneo la Kimara Rombo,
Dar es Salaam kumjulia hali Askari wa kikosi cha Usalama Barabarani
Sajent Steven Laizer, baada ya kupata ajali akiongoza
msafara wa Rais kuelekea kwenye msiba wa dereva wa Ikulu


  1. MSAFARA wa Rais Jakaya Kikwete jana ulipata ajali baada ya askari aliyekuwa akiuongoza kwa pikipiki kudondoka na kujeruhiwa katika eneo la Kimara, Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea eneo la Kimara Rombo saa 4.30 asubuhi wakati Rais Kikwete alipokuwa akielekea Kimara Kilungule kwenye msiba wa Dereva wa Ikulu, Deokalyus Makwasinga aliyefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari katika eneo la Kimara-Korogwe, Msikitini usiku wa kuamkia Ijumaa.
  2. Tukio la kwanza lilitokea maeneo ya Kimara Mwisho wakati Rais alipokuwa akitokea Kimara-Bonyokwa katika alikokwenda kutembelea maeneo yaliyokuwa na matatizo ya maji kwa muda mrefu. Msafara huo ulilazimika kusimama ghafla kutokana na gari alilokuwa amepanda kuchomoka tairi la mbele.
  3. Katika tukio la pili, msafara wa Rais ulisimama ghafla eneo la bandarini karibu na eneo la Matangini baada ya gari alilokuwemo kuchomoka tari la nyuma wakati akitokea Keko Toroli.
  4. Januari 2010, msafara wa Rais Kikwete ulipata ajali mkoani Shinyanga wakati gari la polisi lililokuwa likiuongoza kuacha njia na kupinduka na kujeruhi askari. Walioshuhudia ajali hiyo walisema waliliona gari hilo likiyumba na baadaye kuacha njia na kupinduka kando ya barabara iendayo Meatu. Katika ajali hiyo iliyotokea katika Kijiji cha Nyikoboko wakati msafara wa Rais ukitokea Kisese alikokuwa amekwenda kuzindua Mto Simiyu unaounganisha Wilaya za Bariadi na Meatu, askari sita walijeruhiwa.
  5. Mei, 2010, magari aliyokuwa amepanda Rais Kikwete akiwa katika ziara yake ya siku mbili Dar es Salaam yalipata hitilafu baada ya magari hayo kuchomoka matairi katika maeneo tofuati yakiwa safarini.
  6. Kuna ajali iliyotokea msafara wa Salma Kikwete barabara ya Segerea kama sijakosea iligharibu uhai wa mtu.
 
Mara nyingi riders( waendesha pikipiki za msafara) hujisababishia ajali kwanini huwa wanailaza zigzag pikipiki huku wakiwa kasi kubwa? Wakati sumaye alikwa waziri mkuu rider alinusurika kufa pale brake point bado wanaendelea kuzilaza pikipiki...sisi tufanyeje sasa?
 
Sheikh Yahya anawaita taratibu! Akisikia njaa anaita damu za the gambaz fasta unashangaa ajali hiyoooooooo!!!!
 
Mara nyingi riders( waendesha pikipiki za msafara) hujisababishia ajali kwanini huwa wanailaza zigzag pikipiki huku wakiwa kasi kubwa? Wakati sumaye alikwa waziri mkuu rider alinusurika kufa pale brake point bado wanaendelea kuzilaza pikipiki...sisi tufanyeje sasa?

Kasi ya msafari ni kitu hatari zaidi. Sioni sababu ya kwenda kasi kiasi hicho. Mbona jana Kikwete alisubiri dakika kadhaa ilipotokea ajali hakikutokea kitu kibaya? Kasi ile wanaogopa nini kama si mtindo tu wa maisha na woga?
 
Mara nyingi riders( waendesha pikipiki za msafara) hujisababishia ajali kwanini huwa wanailaza zigzag pikipiki huku wakiwa kasi kubwa? Wakati sumaye alikwa waziri mkuu rider alinusurika kufa pale brake point bado wanaendelea kuzilaza pikipiki...sisi tufanyeje sasa?

Kuchamba Kwingi!! - Wanatakiwa Wajue Safety Kwanza!!
 
Apande mabasi tunayopanda sisi aone kama mpaka 2015 hajawa mkono mmoja,mguu mmoja,jicho moja na kalio moja.
 
Kasi ya msafari ni kitu hatari zaidi. Sioni sababu ya kwenda kasi kiasi hicho. Mbona jana Kikwete alisubiri dakika kadhaa ilipotokea ajali hakikutokea kitu kibaya? Kasi ile wanaogopa nini kama si mtindo tu wa maisha na woga?

Mkuu tatizo siyo kasi peke yake, kwa kuwa tangia enzi ya nyerere walikuwa wanaendesha hivyo!
Mi nadhani hii kauli ya CHADEMA kutokulipiza kisasi kwa wauaji wa CCM ndiyo sababu. CHADEMA walisema wao wamewachinja watu wetu, lakini sisi hatutalipiza kisasi, tunawaachia Mungu atafanya!

Sisi tuna Mungu
Wao wana Pesa
 
Mkuu tatizo siyo kasi peke yake, kwa kuwa tangia enzi ya nyerere walikuwa wanaendesha hivyo!
Mi nadhani hii kauli ya CHADEMA kutokulipiza kisasi kwa wauaji wa CCM ndiyo sababu. CHADEMA walisema wao wamewachinja watu wetu, lakini sisi hatutalipiza kisasi, tunawaachia Mungu atafanya!

Sisi tuna Mungu
Wao wana Pesa

Damu za wahanga wetu zinawamaliza
 
Kwani si hukohuko kimara mwaka jana tairi lilichomoka?

RAIS2.JPG


Inawezekana misafara ya Mkulu haipangwi katika takwimu zake sahihi hivyo vyombo huwa havijaandaliwa ipasavyo. Kuna dalili kama za kushtukiza vile.

Inaelekea akiwa pale Ikulu panawasha akikaa hivyo anaamua kuinuka ghafla na kupanga safari zisizotarajiwa na matokeo ndo hayo. Ni fikra zangu binafsi.
 
yeye mwenyewe hana umakini na watu wanaoangalia ulinzi wake hawako makini kinachobaki ni kudra za Mungu tu
 
Ukiona hivyo ujue yale majini aliyowekewa na Shekh Yahya hajapata msosi siku nyiingi sasa yanabeep, yasipopigiwa yatafanya balaa siku si nyingi.
 
Ukiona hivyo ujue yale majini aliyowekewa na Shekh Yahya hajapata msosi siku nyiingi sasa yanabeep, yasipopigiwa yatafanya balaa siku si nyingi.

Una maana Rais wetu analindwa na majini ya Shekh Yahya, na sasa yanataka mlo wa damu ya binadamu? Watu wengine bana wanatuvunja mbavu kwani ni hadithi za kufikirika.
 
000000ajalikikwete.jpg

Rais Jakaya Kikwete akiteremka kwenye gari lake eneo la Kimara Rombo,
Dar es Salaam kumjulia hali Askari wa kikosi cha Usalama Barabarani
Sajent Steven Laizer, baada ya kupata ajali akiongoza
msafara wa Rais kuelekea kwenye msiba wa dereva wa Ikulu


  1. MSAFARA wa Rais Jakaya Kikwete jana ulipata ajali baada ya askari aliyekuwa akiuongoza kwa pikipiki kudondoka na kujeruhiwa katika eneo la Kimara, Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea eneo la Kimara Rombo saa 4.30 asubuhi wakati Rais Kikwete alipokuwa akielekea Kimara Kilungule kwenye msiba wa Dereva wa Ikulu, Deokalyus Makwasinga aliyefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari katika eneo la Kimara-Korogwe, Msikitini usiku wa kuamkia Ijumaa.
  2. Tukio la kwanza lilitokea maeneo ya Kimara Mwisho wakati Rais alipokuwa akitokea Kimara-Bonyokwa katika alikokwenda kutembelea maeneo yaliyokuwa na matatizo ya maji kwa muda mrefu. Msafara huo ulilazimika kusimama ghafla kutokana na gari alilokuwa amepanda kuchomoka tairi la mbele.
  3. Katika tukio la pili, msafara wa Rais ulisimama ghafla eneo la bandarini karibu na eneo la Matangini baada ya gari alilokuwemo kuchomoka tari la nyuma wakati akitokea Keko Toroli.
  4. Januari 2010, msafara wa Rais Kikwete ulipata ajali mkoani Shinyanga wakati gari la polisi lililokuwa likiuongoza kuacha njia na kupinduka na kujeruhi askari. Walioshuhudia ajali hiyo walisema waliliona gari hilo likiyumba na baadaye kuacha njia na kupinduka kando ya barabara iendayo Meatu. Katika ajali hiyo iliyotokea katika Kijiji cha Nyikoboko wakati msafara wa Rais ukitokea Kisese alikokuwa amekwenda kuzindua Mto Simiyu unaounganisha Wilaya za Bariadi na Meatu, askari sita walijeruhiwa.
  5. Mei, 2010, magari aliyokuwa amepanda Rais Kikwete akiwa katika ziara yake ya siku mbili Dar es Salaam yalipata hitilafu baada ya magari hayo kuchomoka matairi katika maeneo tofuati yakiwa safarini.
  6. Kuna ajali iliyotokea msafara wa Salma Kikwete barabara ya Segerea kama sijakosea iligharibu uhai wa mtu.

Ajali ni kawaida, Mungu akishapanga huwezi kukwepa.
 
Wapunguze speed zao ambazo sizo za lazima wanakimbiaa sanaa......wanaogopa nini?au wanakambia nini??
 
000000ajalikikwete.jpg

Rais Jakaya Kikwete akiteremka kwenye gari lake eneo la Kimara Rombo,
Dar es Salaam kumjulia hali Askari wa kikosi cha Usalama Barabarani
Sajent Steven Laizer, baada ya kupata ajali akiongoza
msafara wa Rais kuelekea kwenye msiba wa dereva wa Ikulu


  1. MSAFARA wa Rais Jakaya Kikwete jana ulipata ajali baada ya askari aliyekuwa akiuongoza kwa pikipiki kudondoka na kujeruhiwa katika eneo la Kimara, Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea eneo la Kimara Rombo saa 4.30 asubuhi wakati Rais Kikwete alipokuwa akielekea Kimara Kilungule kwenye msiba wa Dereva wa Ikulu, Deokalyus Makwasinga aliyefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari katika eneo la Kimara-Korogwe, Msikitini usiku wa kuamkia Ijumaa.
  2. Tukio la kwanza lilitokea maeneo ya Kimara Mwisho wakati Rais alipokuwa akitokea Kimara-Bonyokwa katika alikokwenda kutembelea maeneo yaliyokuwa na matatizo ya maji kwa muda mrefu. Msafara huo ulilazimika kusimama ghafla kutokana na gari alilokuwa amepanda kuchomoka tairi la mbele.
  3. [FONT=ver
    [/COLOR][/SIZE][/FONT]
  4. Januari 2010, Shinyanga wakati gari la polisi lililokuwa likiuongoza kuacha njia na kupinduka na kujeruhi askari. Walioshuhudia ajali hiyo walisema waliliona gari hilo likiyumba na baadaye kuacha njia na kupinduka kando ya barabara iendayo Meatu. Katika ajali hiyo iliyotokea katika Kijiji cha Nyikoboko wakati msafara wa Rais ukitokea Kisese alikokuwa amekwenda kuzindua Mto Simiyu unaounganisha Wilaya za Bariadi na Meatu, askari sita walijeruhiwa.
  5. Mei, 2010, magari aliyokuwa amepanda Rais Kikwete akiwa katika ziara yake ya siku mbili Dar es Salaam yalipata hitilafu baada ya magari hayo kuchomoka matairi katika maeneo tofuati yakiwa safarini.
  6. Kuna ajali iliyotokea msafara wa Salma Kikwete barabara ya Segerea kama sijakosea iligharibu uhai wa mtu.

Umesahau kituko cha moshi ..magari Yake yote yalizimika baada ya kuwekwa mafuta mabovu...kwenye vituo vya uchochoroni vya mafuta......ililetaa tafrani Kali walinzi wake wakiohofia kuna tukio lilipangwa kumbe uzembe tu
 
Una maana Rais wetu analindwa na majini ya Shekh Yahya, na sasa yanataka mlo wa damu ya binadamu? Watu wengine bana wanatuvunja mbavu kwani ni hadithi za kufikirika.

Shehe yahaya alisema atampatia ulinzi uliojificha usiooneka na yeye na ikulu yake hawakukanusha kwa hiyo unganisha dots
 
Mungu atuondolee huu udhia mapema iwezekanavyo... Mungu tunakuomba usikie maombi yetu..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom