Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Rais Jakaya Kikwete akiteremka kwenye gari lake eneo la Kimara Rombo,
Dar es Salaam kumjulia hali Askari wa kikosi cha Usalama Barabarani
Sajent Steven Laizer, baada ya kupata ajali akiongoza
msafara wa Rais kuelekea kwenye msiba wa dereva wa Ikulu
- MSAFARA wa Rais Jakaya Kikwete jana ulipata ajali baada ya askari aliyekuwa akiuongoza kwa pikipiki kudondoka na kujeruhiwa katika eneo la Kimara, Dar es Salaam. Ajali hiyo ilitokea eneo la Kimara Rombo saa 4.30 asubuhi wakati Rais Kikwete alipokuwa akielekea Kimara Kilungule kwenye msiba wa Dereva wa Ikulu, Deokalyus Makwasinga aliyefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari katika eneo la Kimara-Korogwe, Msikitini usiku wa kuamkia Ijumaa.
- Tukio la kwanza lilitokea maeneo ya Kimara Mwisho wakati Rais alipokuwa akitokea Kimara-Bonyokwa katika alikokwenda kutembelea maeneo yaliyokuwa na matatizo ya maji kwa muda mrefu. Msafara huo ulilazimika kusimama ghafla kutokana na gari alilokuwa amepanda kuchomoka tairi la mbele.
- Katika tukio la pili, msafara wa Rais ulisimama ghafla eneo la bandarini karibu na eneo la Matangini baada ya gari alilokuwemo kuchomoka tari la nyuma wakati akitokea Keko Toroli.
- Januari 2010, msafara wa Rais Kikwete ulipata ajali mkoani Shinyanga wakati gari la polisi lililokuwa likiuongoza kuacha njia na kupinduka na kujeruhi askari. Walioshuhudia ajali hiyo walisema waliliona gari hilo likiyumba na baadaye kuacha njia na kupinduka kando ya barabara iendayo Meatu. Katika ajali hiyo iliyotokea katika Kijiji cha Nyikoboko wakati msafara wa Rais ukitokea Kisese alikokuwa amekwenda kuzindua Mto Simiyu unaounganisha Wilaya za Bariadi na Meatu, askari sita walijeruhiwa.
- Mei, 2010, magari aliyokuwa amepanda Rais Kikwete akiwa katika ziara yake ya siku mbili Dar es Salaam yalipata hitilafu baada ya magari hayo kuchomoka matairi katika maeneo tofuati yakiwa safarini.
- Kuna ajali iliyotokea msafara wa Salma Kikwete barabara ya Segerea kama sijakosea iligharibu uhai wa mtu.