Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Wadau. Nimedunduliza kahela ka kununua gari Kampuni ya Autorec ya Japan. Nimekuwa nalipia kwa awamu, nimelipa awamu mbili bado moja ya mwisho. Changamoto ni kuwa kila ninapotuma pesa huwa nawajulisha Autorec na kuwatumia risiti ya TT. Ajabu ni kuwa kwa awamu zote mbili, Autorec wanakiri kupokea pesa lakini zinakuwa zimepungua $ 25/-. Nimefuatilia benki nilizotumia kulipia na wamehakisha kuwa wametuma kama nilivyolipia.
Autorec wanadai wamepokea pesa pungufu ya $ 25/-. Nijuzeni, hawa ni matapeli?
Autorec wanadai wamepokea pesa pungufu ya $ 25/-. Nijuzeni, hawa ni matapeli?