Mlipa kodi wa Tanzania ni sawa na mbeba ndoo ya maji alielemewa barabarani ila hana jinsi ni la

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Tatizo letu ni poor reasoning inayotaokana na IQ yetu kuwa ndogo.

Wanachokifanya hawa jamaa ni sawa na anachokifanya mbeba mzigo alielemewa na mzigo barabarani lakini hana budi inabidi ajikongoje tu mradi afike.

"Mbeba mzigo huyu(mlipa kodi) kabebeshwa ndoo nzito ya maji(kodi) kuliko uweza wake na umbali anaokwenda ni mrefu kwahiyo anachofanya ili afike ni kuweka mzigo wake kichwani kwanza alafu anapiga hatua chache akichoka then anahamishia ndoo yake mkono wa kulia kisha anatembea hatua kadhaa anahamishia tena mzigo huo mkono wa kushoto kabla ya kuurudisha tena kichwani mpaka pale atakopifika."

Mtu huyu mpaka afike sijui atakuwa hoi kiasi gani.

Mlipa kodi wa Tanzania hana tofauti na mbeba ndoo ya maji alielemewa lakini hana budi kufika anakokwenda.

Bila kubuni vyanzo vipya vya mapato na vyenye kueleweka tutaendelea kuwekewa mzigo huu wa kodi kichwani then watauhamishia mkono wa kulia na baadae mkono wa kushoto kabla ya kuuridisha mzigo huo kichwani huku wakikuambia wanakusaidi usifike ukiwa umechoka huku mwili wako ni ule ule.
 
Tutakuteua kuwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri moja wapo hapo Dodoma,ili upunguze nyongo humu jf!
 
Tatizo letu ni poor reasoning inayotaokana na IQ yetu kuwa ndogo.

Wanachokifanya hawa jamaa ni sawa na anachokifanya mbeba mzigo alielemewa na mzigo barabarani lakini hana budi inabidi ajikongoje tu mradi afike.

"Mbeba mzigo huyu(mlipa kodi) kabebeshwa ndoo nzito ya maji(kodi) kuliko uweza wake na umbali anaokwenda ni mrefu kwahiyo anachofanya ili afike ni kuweka mzigo wake kichwani kwanza alafu anapiga hatua chache akichoka then anahamishia ndoo yake mkono wa kulia kisha anatembea hatua kadhaa anahamishia tena mzigo huo mkono wa kushoto kabla ya kuurudisha tena kichwani mpaka pale atakopifika."

Mtu huyu mpaka afike sijui atakuwa hoi kiasi gani.

Mlipa kodi wa Tanzania hana tofauti na mbeba ndoo ya maji alielemewa lakini hana budi kufika anakokwenda.

Bila kubuni vyanzo vipya vya mapato na vyenye kueleweka tutaendelea kuwekewa mzigo huu wa kodi kichwani then watauhamishia mkono wa kulia na baadae mkono wa kushoto kabla ya kuuridisha mzigo huo kichwani huku wakikuambia wanakusaidi usifike ukiwa umechoka huku mwili wako ni ule ule.
Tunasubiri bajeti ya kambi ya upinzani, usitutoe kwenye reli.
 
Kamanda, nakuona unahangaika tangu asubuhi na Bajeti ya Mpango. Wenzako wameshanyoosha mikono. Utabaki peke yako
 
Nakuona unaumia sana kwa kukosa pa kushikia, ndege zimebuma, tetemeko la ardhi limebuma, vifo vomebuma, nakushauri jaribu kupata kiki kwa kutumia tukio la Kibiti.
Mikataba ya ndege mmeweka wazi?

Unaposema ya tetemeko yamebuma uko kwenye nafsi za watu?

Acha kuwa na akili ujazo wa kijijko cha chai.
 
Back
Top Bottom