cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 85,148
- 136,657
kipindi nipo darasa la sita... kwenye kukaa tulikua tunapangwa ile wavulana wawili msichana katikati au wasichana na mvulana ili kuepusha kelele. Bhas bwana siku ya ijumaa kama kawaida vipind vichache na unakuta kila mtu karudi kukaa na shosti yake. .
nilipokua nakaa mimi wasichana walikua wawili na mvulana mmoja, sasa tulishajikusanya kupiga umbea mashosti ka ilivyo ada.. Eeee ghafla bin vuu jamaa katoka alipotoka kaja kukaa sasa dawati linabeba watatu yeye wanne kaja jiongeza Aaa tukaona mazinguz tukawa tunamsukuma,sasa si akaanguka na mimi ndio nilikua pembeni yake so alipoibuka na hasira akanivaa mimi tukanza ugomvi jamaa alinibutua mateke ya tumbo..
dah nikainama kusikilizia maumivu uku darasa zima linamwambia umeuaa!! umeuaaa!! aseh kuskia vile nilishikwa na hasira nilimuibukia jamaa na mangumi aliyoshindwa zuia adi tulipokuja amuliwa alishageuka nyanya maana alikua mweupe kukaa kidogo kengele nayo iyoo mda wa usafi...
haha iyo siku ndiyo ilikua mara yangu ya kwanza kupigana skuli