Mliowahi kuacha au kuachwa Mke/Mume, mlikutana na changamoto gani kubwa baada ya ndoa kuvunjika?

Ligaba

JF-Expert Member
Oct 12, 2018
1,045
2,821
Habari za Nyerere day.

After six years of being in marriage naona kama ibilisi anakaribia kukata panga. I have two kids kwa huyu bidada but I see the end of road. Kila wakati nikiwaangalia hivi vitoto na wanapotaka kuelekea naona maji yanajaa katika macho yangu, wananipenda na nawapenda hasa lakini hatupendani na mama yao.

Nawaza sana niumie ili wabaki na furaha au niitafute furaha wao waumie? Mliopitia changamoto za divorcing hebu saidieni picha ya maisha after marriage.
 
Kuishi katika ndoa ambayo haina mapenzi na imejaa ugomvi kila leo si jambo jema hao watoto kulishuhudia. Kama hamuwezi kuweka pembeni tofauti zenu ili muishi kwa amani basi ni bora kufanya maamuzi muafaka ili kila mtu ashike 50 zake watoto watateseka hasa kama GF/Mke mpya atakuwa na roho mbaya.
 
Mkiwa hamjaolewa mnahuruma mkiolewa sasa kila rangi mtu utaona..
unajua nawahurumia watoto maana mi nilivyokua mdogo mama akisafir tu lazima kila siku jioni nitaenda kusimama njia aliyo ondokea nikisubil arudi likiingia giza narudi ndani weeee hakuna KAMA mama labda huyo baba ndio apewe talaka aondoke mama abaki na hela za matumizi ziko pale pale
 
Kuishi katika ndoa ambayo haina mapenzi na imejaa ugomvi kila leo si jambo jema hao watoto kulishuhudia. Kama hamuwezi kuweka pembeni tofauti zenu ili muishi kwa amani basi ni bora kufanya maamuzi muafaka ili kila mtu ashike 50 zake watoto watateseka hasa kama GF/Mke mpya atakuwa na roho mbaya.
Ni vizuri shida huruma ya watoto na bahati mwanamke akijua unawapenda sana atatumia kama turufu ya kukusumbua.
 
Mpaka mnafikia kuachana mlijaribu suluhu ikakosa, Sasa kwa nini ujitese? Unadhani mama wa kambo wote wabaya kuna watu wanaupendo hata kwa watoto wa kambo.

Ujatueleza watoto wana umei gani kama washaanza shule oa mwingine. Ishiiiiiy usijitese mwaya oa.
 
Hapo ndiyo Mkuu inabidi uamua kusuka au kunyoa. Mnaendelea kuishi pamoja for the sake of your kids lakini kila mtu ana yake anaingia na kutoka atakavyo hakuna kuulizana maana ndoa imeshajifia.
Ngoja tuone
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
unajua nawahurumia watoto maana mi nilivyokua mdogo mama akisafir tu lazima kila siku jioni nitaenda kusimama njia aliyo ondokea nikisubil arudi likiingia giza narudi ndani weeee hakuna KAMA mama labda huyo baba ndio apewe talaka aondoke mama abaki na hela za matumizi ziko pale pale
Vitoto vyamwisho bhana..😅
 
Habari za Nyerere day.

After six years of being in marriage naona kama ibilisi anakaribia kukata panga. I have two kids kwa huyu bidada but I see the end of road. Kila wakati nikiwaangalia hivi vitoto na wanapotaka kuelekea naona maji yanajaa katika macho yangu, wananipenda na nawapenda hasa lakini hatupendani na mama yao.

Nawaza sana niumie ili wabaki na furaha au niitafute furaha wao waumie? Mliopitia changamoto za divorcing hebu saidieni picha ya maisha after marriage.
Mkuu, mimi ni mtoto wa kulelewa na mama wa Kambo namshukuru mama yule ni mama mwema sana kwa upande wangu, yupo mdogo wangu wa kike ambaye naye tumelelewa pamoja lkn bahati mbaya sana hawakuiva na yule mama yetu aisee sitaki kurejea taswira za aliyopitia its bad na niliapa kuwa sitokuja kuwa sababu ya watoto wangu kulelewa na Mama wa Kambo.

Kwa kifupi nakushauri hivi;
1. Kuchokana kupo sana tu, lkn goes with certain period of time, vumilia ipo siku utaanza kumpenda tena mama yao, ndio sababu watu wanaweza achana leo wakarudiana baada ya miaka kadhaa kupita, that means wamerejea katika hali mpya ya kupendana hasa watoto wakiwa kiunganishi.

2. Kama huwezi ku balance mambo epuka michepuko maana u might fall totally kwa mchepuko nyumbani ukawa unaona ni kama jela/tanuri. (Kurogwa kupo)

3. Jitahidi kuwa sehemu tofauti na mama watoto wako mfano vacations na mitoko mingine can assist kwenye ku-reunite and revamping ur marriage.

4. Make sure maamuzi juu ya mahusiano yenu ni yenu yasiingiliwe na yyt iwe wa upande wako au wake, wengi hufurahia mabaya ya wengine yanapowakuta.

5. It might happen watoto wakawa wanalewewa na mama, certainly mama akaja kuolewa tena, wapo wababa wa kambo wenye kufanya unyama mkubwa kwa watoto waliowakuta kwa mwanamke including kuwalawiti etc....

Siafiki watoto kulelewa na mama wa kambo hutojua kinachoendelea kwa watoto ukiwa haupo, utajua ikiwa too late.

Testimonial
Ninaye shemeji yangu (dada wa mke wangu) ameachana na mumewe, katika vitu huwa anatusihi ni kufikia hatua aliyofikia yeye maana inamtesa kuona wale watoto wanavyohangaika na kuteseka kwa sababu ya wao kuachana. Mm nimechukua jukumu la kumlelea mwanae mmoja kwasababu ya mateso aliyokuwa akipitia huyo mtoto.

Nikutakie kila la kheri na busara kwenye uamuzi wa hili. Kumbuka kosa pekee gumu kusameheka ni uasharati mengine yanarekebishika na kusameheka.
 
Kuishi katika ndoa ambayo haina mapenzi na imejaa ugomvi kila leo si jambo jema hao watoto kulishuhudia. Kama hamuwezi kuweka pembeni tofauti zenu ili muishi kwa amani basi ni bora kufanya maamuzi muafaka ili kila mtu ashike 50 zake watoto watateseka hasa kama GF/Mke mpya atakuwa na roho mbaya.
Linapokuja suala la wivu, wanawake hapa wanakosaga ustahimilivu. Hapa ndio utesi wa watoto huanziaga!
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom