Mlioko Tanzania tutupieni jamvini picha za sayari ya Jupiter na Saturn

Post #150 umeandika hivi.

"Nimekupa uthibitisho wa uumbaji wake nikakutajia mpaka vitu alivyoumba , ninajua kwamba Mungu ndiye alieumba vitu hivyo kwa maana hakuna kiumbe yoyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana (malaika n.k) na ulimwengu huu unaoonekana(sayari zote na vyote vilivyomo), najua kwamba Mungu yupo kwa ushahidi wa uumbaji wake, hakuna kitu kinaweza kutokea bila muumbaji"

Nakuuliza hivi.

Unajuaje kwamba huo unaouita uumbaji wake ni uumbaji wake kweli, na kwamba, hiyo habari ya "uumbaji wake" si hadithi za watu tu wanaosema huu ni uumbaji wake kwa sababu hawajui uumbaji huu umetokea vipi?

Kujua kwamba hakuna kiumbe anayeweza kuumba uumbaji huo hakuthibitishi Mungu yupo wala kaumba.

Hujajibu swali hili.
Asante. Hapo kwenye hiyo post nimekujibu ninajua kwamba Mungu ndiye alieumba vitu hivyo kwa maana hakuna kiumbe yoyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana (malaika n.k) na ulimwengu huu unaoonekana(sayari zote na vyote vilivyomo). Pia nilikujibu kwenye post #153 kutokuweza kwa kiumbe yeyote kuumba ulimwengu usioonekana na unaoonekana kunathibitisha kwamba yupo Mungu pekee ambaye alieumba uumbaji wote(usioonekana na unaoonekana). Majibu haya nimeyarudia tena kwa faida ya akili zako. Asante.

Nakupa mfano mdogo mmoja, hakuna kiumbe yeyote anaweza kuumba bahari na vyote vilivyomo ndani ya bahari(samaki n.k). bali ni Mungu pekee ndiye alieumba uumbaji huo.
 
Asante. Hapo kwenye hiyo post nimekujibu ninajua kwamba Mungu ndiye alieumba vitu hivyo kwa maana hakuna kiumbe yoyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana (malaika n.k) na ulimwengu huu unaoonekana(sayari zote na vyote vilivyomo). Pia nilikujibu kwenye post #153 kutokuweza kwa kiumbe yeyote kuumba ulimwengu usioonekana na unaoonekana kunathibitisha kwamba yupo Mungu pekee ambaye alieumba uumbaji wote(usioonekana na unaoonekana). Majibu haya nimeyarudia tena kwa faida ya akili zako. Asante.
Wewe unajua kwamba Mama yako si Mjerumani?
 
Wewe unajua kwamba Mama yako si Mjerumani?
Ndio najua mama yangu si mjerumani, je wewe unajua kwamba Mungu ndie aliekuumba wewe na kukuwekea mifumo mbalimbali mwilini mwako(Ubongo,moyo,mapafu,mdomo,pua, mifumo ya uzazi n.k) inayokusaidia kuishi?
 
Ndio najua mama yangu si mjerumani, je wewe unajua kwamba Mungu ndie aliekuumba wewe na kukuwekea mifumo mbalimbali mwilini mwako(Ubongo,moyo,mapafu,mdomo,pua, mifumo ya uzazi n.k) inayokusaidia kuishi?
Sasa wewe kujua kwamba Mama yako si Mjerumani kunathibitisha Mama yako ni Malaika?

Kimsingi, ukisema unajua Mungu ndiye kaumba dunia kwa sababu hakuna kiumbe anayeweza kuumba dunia, ni sawa na kusema unajua wewe mama yako ni malaika, kwa sababu hakuna Mjerumani aliye Mama yako.

Hujaangalia uwezekano kwamba mama yako anaweza akawa si Mjerumani wala malaika.

Hujaangalia uwezekano kwamba uumbaji huu haujatokana na kiumbe wala Mungu.
 
Sasa wewe kujua kwamba Mama yako si Mjerumani kunathibitisha Mama yako ni Malaika?

Kimsingi, ukisema unajua Mungu ndiye kaumba dunia kwa sababu hakuna kiumbe anayeweza kuumba dunia, ni sawa na kusema unajua wewe mama yako ni malaika, kwa sababu hakuna Mjerumani aliye Mama yako.

Hujaangalia uwezekano kwamba mama yako anaweza akawa si Mjerumani wala malaika.

Hujaangalia uwezekano kwamba uumbaji huu haujatokana na kiumbe wala Mungu
Mifano yako unayoitoa haina uhalisia na ni mifano mfu. nakuambia kwamba mama yangu si mjerumani ni mtanzania(hii ni kwa mujibu wa mifumo ya kidunia na sheria zake/utaifa), lakini fahamu kwamba kabla ya mifumo ya utaifa Mungu aliumba kiumbe binadamu ME na KE hawa viumbe wakaijaza dunia hapakua na utaifa enzi hizo, utaifa ulikuja baadae. Hii ni elimu nimekuongezea.

mama yangu hawezi kuwa malaika kwa sababu aliumbwa katika ulimwengu wa kuonekana ili aishi katika ulimwengu huu wa kuonekana. Malaika ni viumbe walioumbwa kuishi katika ulimwengu usioonekana kwa macho.

nimekuthibitishia na ni uthibitisho ulio wazi, wa kweli na halisi kwamba uwezekano wa uumbaji unaoonekana kwa macho(Sayari zote na vyote vilivyomo) na usioonekana kwa macho(Malaika n.k) hautokani na kiumbe yeyote BALI ULIUMBWA NA MUNGU MWENYEWE.
 
Mifano yako unayoitoa haina uhalisia na ni mifano mfu. nakuambia kwamba mama yangu si mjerumani ni mtanzania(hii ni kwa mujibu wa mifumo ya kidunia na sheria zake/utaifa), lakini fahamu kwamba kabla ya mifumo ya utaifa Mungu aliumba kiumbe binadamu ME na KE hawa viumbe wakaijaza dunia hapakua na utaifa enzi hizo, utaifa ulikuja baadae. Hii ni elimu nimekuongezea.

mama yangu hawezi kuwa malaika kwa sababu aliumbwa katika ulimwengu wa kuonekana ili aishi katika ulimwengu huu wa kuonekana. Malaika ni viumbe walioumbwa kuishi katika ulimwengu usioonekana kwa macho.

nimekuthibitishia na ni uthibitisho ulio wazi, wa kweli na halisi kwamba uwezekano wa uumbaji unaoonekana kwa macho(Sayari zote na vyote vilivyomo) na usioonekana kwa macho(Malaika n.k) hautokani na kiumbe yeyote BALI ULIUMBWA NA MUNGU MWENYEWE.
Umekubali kwamba kujua Mama yako si Mjerumani hakuthibitishi Mama yako ni Malaika?

Umekubali kujua Mama yako si Mjerumani hakuna uhusiano na habari ya kwamba Mama yako ni Malaika, mambo haya mawili hayana uhusiano?
 
Umekubali kwamba kujua Mama yako si Mjerumani hakuthibitishi Mama yako ni Malaika?

Umekubali kujua Mama yako si Mjerumani hakuna uhusiano na habari ya kwamba Mama yako ni Malaika, mambo haya mawili hayana uhusiano?
narudia kusema mifano yako si hai. unawezaje kuhusisha kiumbe binadamu na kiumbe malaika? malaika hawezi kuzaa binadamu lakini binadamu atazaliwa na binadamu mwenzie, vivyo hivyo mimi nimezaliwa na binadamu(mama yangu). Anyway nilikuuliza hili swali hujanijibu je wewe unajua kwamba Mungu ndie aliekuumba wewe na kukuwekea mifumo mbalimbali mwilini mwako(Ubongo,moyo,mapafu,mdomo,pua, mifumo ya uzazi n.k) inayokusaidia kuishi?
 
narudia kusema mifano yako si hai. unawezaje kuhusisha kiumbe binadamu na kiumbe malaika? malaika hawezi kuzaa binadamu lakini binadamu atazaliwa na binadamu mwenzie, vivyo hivyo mimi nimezaliwa na binadamu(mama yangu). Anyway nilikuuliza hili swali hujanijibu je wewe unajua kwamba Mungu ndie aliekuumba wewe na kukuwekea mifumo mbalimbali mwilini mwako(Ubongo,moyo,mapafu,mdomo,pua, mifumo ya uzazi n.k) inayokusaidia kuishi?
Yani wewe uliyehusisha viumbe na Mungu, na kusema kwa kuwa hakuna kiumbe aliyeumba bahari, basi ni lazima imeumbwa na Mungu, unanishangaa mimi kuhusisha kiumbe binadamu na kiumbe Malaika?

Unaelewa hata unachoandika wewe mwenyewe?

Unaelewa kwamba unanikataza kufanya kitu kile kile ulichofanya?

Unaelewa double standard ni nini? Unaelewa logical non sequitur ni nini?

Unaniuliza kama mimi najua kuwa Mungu ndiye aliyeniumba wakati umeshindwa kum define na kuthibitisha huyo Mungu yupo?

Define Mungu ni nini.
Thibitisha Mungu yupo kwanza.
 
Yani wewe uliyehusisha viumbe na Mungu, na kusema kwa kuwa hakuna kiumbe aliyeumba bahari, basi ni lazima imeumbwa na Mungu, unanishangaa mimi kuhusisha kiumbe binadamu na kiumbe Malaika?

Unaelewa hata unachoandika wewe mwenyewe?

Unaelewa kwamba unanikataza kufanya kitu kile kile ulichofanya?

Unaelewa double standard ni nini? Unaelewa logical non sequitur ni nini?

Unaniuliza kama mimi najua kuwa Mungu ndiye aliyeniumba wakati umeshindwa kum define na kuthibitisha huyo Mungu yupo?

Define Mungu ni nini.
Thibitisha Mungu yupo kwanza.
Mkuu, naona unajaribu kugeuza contents. wewe ndie ulietoa mifano ambayo si hai, ukahusisha kiumbe binadamu na kiumbe malaika. rejea mifano yako vizuri. mimi nimekupa facts kwamba Mungu ndiye alietuumba viumbe vyote(ulimwengu usioonekana(Malaika n.k) na unaoonekana (Sayari zote na vyote vilivyomo/viumbe na mimea)

Bado maswali yako unayouliza yanajirudia na nimeshayajibu, nimeshakuthibitishia na kukupa mifano mingi ya uumbaji wake. bado unauliza Mungu ni nini? Mungu ni muasisi na muumbaji wa ulimwengu usioonekana(Malaika n.k) na ulimwengu unaoonekana (Sayari zote na vyote vilivyomo/viumbe na mimea). Mungu yupo katika ulimwengu usioonekana kwa macho na malaika. Kwa sisi viumbe aliotuumba katika ulimwengu unaoonekana kwa macho(especially Sayari Dunia) hatuwezi kumuona kwa macho.
 
Mkuu, naona unajaribu kugeuza contents. wewe ndie ulietoa mifano ambayo si hai, ukahusisha kiumbe binadamu na kiumbe malaika. rejea mifano yako vizuri. mimi nimekupa facts kwamba Mungu ndiye alietuumba viumbe vyote(ulimwengu usioonekana(Malaika n.k) na unaoonekana (Sayari zote na vyote vilivyomo/viumbe na mimea)

Bado maswali yako unayouliza yanajirudia na nimeshayajibu, nimeshakuthibitishia na kukupa mifano mingi ya uumbaji wake. bado unauliza Mungu ni nini? Mungu ni muasisi na muumbaji wa ulimwengu usioonekana(Malaika n.k) na ulimwengu unaoonekana (Sayari zote na vyote vilivyomo/viumbe na mimea). Mungu yupo katika ulimwengu usioonekana kwa macho na malaika. Kwa sisi viumbe aliotuumba katika ulimwengu unaoonekana kwa macho(especially Sayari Dunia) hatuwezi kumuona kwa macho.
Wewe hujahusisha viumbe na Mungu kwa kusema kwa sababu hakuna kiumbe anayeweza kuumba bahari, basi lazima imeumbwa na Mungu?

Unaelewa kusema hivyo ni logical non sequitur?

Unaelewa logical non sequitur ni nini?
 
Wewe hujahusisha viumbe na Mungu kwa kusema kwa sababu hakuna kiumbe anayeweza kuumba bahari, basi lazima imeumbwa na Mungu?

Unaelewa kusema hivyo ni logical non sequitur?

Unaelewa logical non sequitur ni nini?
Yes, viumbe wote wasioonekana kwa macho(malaika) na sisi tunaoonekana kwa macho (Binadamu,wanyama,samaki,ndege n.k) tuna uhusiano na Mungu maana yeye ndiye alietuumba.

Kwa hiyo mkuu, maisha yetu viumbe wote hasa(tunaoonekana kwa macho) tunaishi kwa kuwezeshwa na Mungu. Ametuumba kwa kutuwekea mifumo ya mapafu ili itusaidie kupumua na ametuumbia hewa itusaidie, katuumbia pia vyakula (matunda ya kila aina na mimea mbogamboga) ili tule tuishi. Mungu anahusiana na sisi kwa namna kubwa.
 
Yes, viumbe wote wasioonekana kwa macho(malaika) na sisi tunaoonekana kwa macho (Binadamu,wanyama,samaki,ndege n.k) tuna uhusiano na Mungu maana yeye ndiye alietuumba.

Kwa hiyo mkuu, maisha yetu viumbe wote hasa(tunaoonekana kwa macho) tunaishi kwa kuwezeshwa na Mungu. Ametuumba kwa kutuwekea mifumo ya mapafu ili itusaidie kupumua na ametuumbia hewa itusaidie, katuumbia pia vyakula (matunda ya kila aina na mimea mbogamboga) ili tule tuishi. Mungu anahusiana na sisi kwa namna kubwa.
Hujathibitisha Mungu yupo, hujathibitisha Malaika wapo.

Unapiga hadithi tu.
 
Hujathibitisha Mungu yupo, hujathibitisha Malaika wapo.

Unapiga hadithi tu.
Huko kusema Mungu hayupo,ni uthibitisho tosha,wa uwepo Mungu.Kinachosemwa na wengi kuwa kipo,na wakatokea wachache wakasema hakipo,huko kusema hakipo,ndio kuwako kwenyewe.Kisichokuwepo,hakisemwi hakipo,ila ni kwa kuwako,ndiko kunakofanya kisemwe hakipo
 
Hujathibitisha Mungu yupo, hujathibitisha Malaika wapo.

Unapiga hadithi tu.
Nimeshakuthibitishia kwa kukupa mifano iliyo hai na wazi, mifano ambayo ni halisi unaishuhudia kwa upeo wa akili na macho yako uumbaji wa Mungu.

Uwepo wako wewe tu, ni uthibitisho tosha, Mungu amekuumba wewe ili uwe binadamu na si viumbe wengine na akakuweka uishi nchi kavu. Je nikuulize wewe unaweza kuishi majini kama viumbe Samaki wa kila aina mule baharini? Nijibu

Je wewe au kiumbe yoyote unaweza kutengeneza tunda Nanasi? (Usije kusema napanda zinaota, No maana hiyo mbegu, arthi, mbolea na maji yanayotumika kuotesha ni MUNGU aliyeumba) Nijibu
 
Nimeshakuthibitishia kwa kukupa mifano iliyo hai na wazi, mifano ambayo ni halisi unaishuhudia kwa upeo wa akili na macho yako uumbaji wa Mungu.

Uwepo wako wewe tu, ni uthibitisho tosha, Mungu amekuumba wewe ili uwe binadamu na si viumbe wengine na akakuweka uishi nchi kavu. Je nikuulize wewe unaweza kuishi majini kama viumbe Samaki wa kila aina mule baharini? Nijibu
Sio tu hujathibitisha Mungu yupo, hujui kuthibitisha ni nini na unaji contradict.

Uwepo wangu hauthibitishi Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo.

Uwepo wangu unathibitisha Mungu huyo hayupo.

Kwa sababu.

1. Mimi nakunya. Waste products ni characteristic ya imperfect system. Mungu huyo muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote kwa nini katengeneza watu imperfect wanakunya badala ya watu perfect wasiokunya wala ku waste energy?

2.Mimi naumwa, same thing, Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna magonjwa? Kama lishindwa, ni kweli ana uwezo wote? Kama hakushindwa, ni kweli ana upendo wote?

3. Kwa nini Mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mambo kama umasikini, vita majanga ya asili,ujambazi etc yanawezekana? Alishindwa kuumba ulimwengu ambao mambo haya hayawezekani? Kama alishindwa, ana uwezo wote kweli? Kama hakushindwa ila kaamua tu kutuumbia ulimwengu wenye mabaya yote haya, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, je, ni kweli ana upendo wote?

4. Mungu ana uwezo wa kutengeneza jiwe kubwa na zito sana kiasi hata yeye mwenyewe hawezi kulibeba?
Kama anaweza kuumba hilo jiwe, basi hana uwezo wote kwa kuwa hawezi kulibeba hilo jiwe.
Kama hawezi kuumba hilo jiwe, basi hana uwezo wote kwa kuwa hawezi kuumba hilo jiwe.

Mungu wako yupo kweli au ni hadithi tu?

Thibitisha yupo kweli.
 
Sio tu hujathibitisha Mungu yupo, hujui kuthibitisha ni nini na unaji contradict.

Uwepo wangu hauthibitishi Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo.

Uwepo wangu unathibitisha Mungu huyo hayupo.

Kwa sababu.

1. Mimi nakunya. Waste products ni characteristic ya imperfect system. Mungu huyo muweza yote, mwenye ujuzi wote na upendo wote kwa nini katengeneza watu imperfect wanakunya badala ya watu perfect wasiokunya wala ku waste energy?

2.Mimi naumwa, same thing, Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna magonjwa? Kama lishindwa, ni kweli ana uwezo wote? Kama hakushindwa, ni kweli ana upendo wote?

3. Kwa nini Mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mambo kama umasikini, vita majanga ya asili,ujambazi etc yanawezekana? Alishindwa kuumba ulimwengu ambao mambo haya hayawezekani? Kama alishindwa, ana uwezo wote kweli? Kama hakushindwa ila kaamua tu kutuumbia ulimwengu wenye mabaya yote haya, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, je, ni kweli ana upendo wote?

4. Mungu ana uwezo wa kutengeneza jiwe kubwa na zito sana kiasi hata yeye mwenyewe hawezi kulibeba?
Kama anaweza kuumba hilo jiwe, basi hana uwezo wote kwa kuwa hawezi kulibeba hilo jiwe.
Kama hawezi kuumba hilo jiwe, basi hana uwezo wote kwa kuwa hawezi kuumba hilo jiwe.

Mungu wako yupo kweli au ni hadithi tu?

Thibitisha yupo kweli.
1. Sio wewe tu kunya, kila kiumbe amemuumbia hivyo, hasa sisi tunaoishi ulimwengu unaoonekana(Duniani). Kuanzia binadamu, wanyama, ndege na samaki woote tunakunya haja kubwa na ndogo. Huu ni mfumo alituumbia ili kutoa taka mwili. Chakula unachokula kikishameng'enywa kinachujwa kisichotakiwa mwilini kinatoka kama taka mwili. Kwa wanyama inasaidia kupatikana mbolea.

2. Baada ya Mungu kuiumba dunia na kutuumba binadamu, sisi viumbe binadamu kwa lifestyles n.k tukaiharibu dunia kwa namna tofauti na maradhi kutokea. Lakini Mungu akatufunulia binadamu akili ya kuunda madawa(Hospitalised Medicines) ambayo madawa haya hutokana na mimea ambayo aliyoiumba, pia kupitia mimea na matunda ni tiba kubwa ambayo ametuumbia. So kutufunulia uwezo wa kutengeneza madawa ni njia ya kutuwezesha sisi kutibu maradhi mbalimbali.

3. Hili limekaa kiimani zaidi na mimi sitaki kuingia kwenye mada hiyo. Hilo ni somo jingine. Lakini kwa faida yako hapo mwanzo Mungu alivyoumba dunia na viumbe wote, alituumba kwa kusudi zuri na hakukuwa na contents kama unazosema. Lakini uharibifu uliofanywa na kiumbe kisichoonekana(malaika aliehasi) kwa kuharibu utaratibu alioukusudia Mungu kwa kiumbe binadamu(Binadamu ambae aliumbwa ili kutawala vitu vyote alivyoviumba Mungu duniani) ndio chanzo cha uharibifu wote hapa duniani. So ni huruma ya Mungu bado anatuvumilia.

4. Mungu yupo na anavumilia uovu wote unaofanywa duniani na kiumbe binadamu aliyeharibiwa na kiumbe kisichoonekana(malaika aliehasi), LINI NA SAA NGAPI ATAKOMESHA UOVU WOTE ANAJUA YEYE PEKEE MUNGU ALIETUUMBA. Kuvumilia kwake kusikupotoshe hata kidogo kwamba hayupo na haoni.
 
Back
Top Bottom