Mlioko Tanzania tutupieni jamvini picha za sayari ya Jupiter na Saturn

Nimeshakuthibitishia tayari kwamba Mungu ameumba ulimwengu huu unaonekana kwa macho na usioonekana kwa macho. Na nimekupa mifano ya vitu alivyoumba.
Hujathibitisha kwamba Mungubyupo na kaumba.

Umeandika tu kwamba Mungu yupo na kaumba.

Kuandika tu si kuthibitisha.

Unajuaje Mungu ndiye kaumba hivyo unavyosema Mungu kaumba?

Unajuaje huyo Mungu yupo kweli na si hadithi tu?
 
Inakuwaje wanajamvi?

Usiku wa kuamkia leo Sayari ya Jupiter na Saturn zitaonekana kwa macho ya kawaida.

Mlioko nyumbani bongo ama Africa kwa jumla mna bahati kwasababu anga liko wazi sky is clear. Tokeni nje sasa hivi mpige picha hata na simu mshare.

Huku Skendinevia tulipo hatuna iyo bahati anga limefunika na pupwe linapuliza.

Kumbukeni hili ni tukio la Kihistoria. Ilirekodiwa na waba anga wa zamani march 14 1200, na baada ya miaka 400 1600. Baada ya miaka 400 tena imetokea leo.

Wanajamvi please mlioko nyumbani Tokeni nje basi mtutumie mapicha ya Jupiter na sayari nayoipenda kuliko zote the gas giant Saturn. Naipenda Saturn kwasababu ya mwezi wake titan inawezekana kuna uhai kwenye iyo Saturn moon titan na labda ndio huko tuaenda tukifa.

Tukio kama hili la leo litatokea tena baada ya miaka 80 2080. Na baada ya hapo litatokea tena baada yya miaka 400 2400.

Ntafurahi sana mwanajamvi yeyote atakayeweka picga aliyopiga ya hizi sayari na nipo tayari kutoa zawadi.

God bless humanity
Umefikaje huko tupe njia ya kishule
 
Kwhayo majibu yako sina cha kukuuliza,nilicho kigundua nikama vile natwanga maji kwenye kinu

Endelea na sinema zako.
maswali ya mtu yanaonesha uelewa wake...nyie wote hamna swali la maana mlilouliza.

Na kama ambavyo mnasema yupo Mungu aliumba Basi hamna tofauti na mimi ninayesema mimi ndo niliumba....Au kuna tofauti gani?
 
Hiyo niliokupa ni Logically proof ambayo unaithibitisha wewe mwenyewe kwa macho na akili. wewe unafikiri uumbaji wa ulimwengu huu unaoonekana kwa macho ulijitokezea tu wenyewe?
"Logically proof" ndiyo dudu gani hilo?

Unajua hata unachoandika ni nini?
 
Hujathibitisha kwamba Mungubyupo na kaumba.

Umeandika tu kwamba Mungu yupo na kaumba.

Kuandika tu si kuthibitisha.

Unajuaje Mungu ndiye kaumba hivyo unavyosema Mungu kaumba?

Unajuaje huyo Mungu yupo kweli na si hadithi tu?
Nimekupa uthibitisho wa uumbaji wake nikakutajia mpaka vitu alivyoumba , ninajua kwamba Mungu ndiye alieumba vitu hivyo kwa maana hakuna kiumbe yoyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana (malaika n.k) na ulimwengu huu unaoonekana(sayari zote na vyote vilivyomo), najua kwamba Mungu yupo kwa ushahidi wa uumbaji wake, hakuna kitu kinaweza kutokea bila muumbaji
 
Nimekupa uthibitisho wa uumbaji wake nikakutajia mpaka vitu alivyoumba , ninajua kwamba Mungu ndiye alieumba vitu hivyo kwa maana hakuna kiumbe yoyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana (malaika n.k) na ulimwengu huu unaoonekana(sayari zote na vyote vilivyomo), najua kwamba Mungu yupo kwa ushahidi wa uumbaji wake, hakuna kitu kinaweza kutokea bila muumbaji
Unaelewa kwamba kujua kwamba hakuna kiumbe yeyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana hakuthibitishi kwamba Mungu ndiye aliyeuumba?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo na habari kwamba yupo si hadithi za watu tu?
 
Unaelewa kwamba kujua kwamba hakuna kiumbe yeyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana hakuthibitishi kwamba Mungu ndiye aliyeuumba?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo na habari kwamba yupo si hadithi za watu tu?
kutokuweza kwa kiumbe yeyote kuumba ulimwengu usioonekana na unaoonekana kunathibitisha kwamba yupo Mungu pekee ambaye alieumba uumbaji wote(usioonekana na unaoonekana). Nimeshathibitisha mala nyingi kwamba Mungu yupo kwa uthibitisho wa uumbaji wake wa ulimwengu usioonekana na unaoonekana.
 
kutokuweza kwa kiumbe yeyote kuumba ulimwengu usioonekana na unaoonekana kunathibitisha kwamba yupo Mungu pekee ambaye alieumba uumbaji wote(usioonekana na unaoonekana). Nimeshathibitisha mala nyingi kwamba Mungu yupo kwa uthibitisho wa uumbaji wake wa ulimwengu usioonekana na unaoonekana.
Wewe hujui herufi za Kiswahili tu.

Hujui tofauti ya "mara" na "mala".

Labda kabla ya kuparamia habari za uwepo wa Mungu, jifunze Kiswahili.

Hapo ulichoandika ni sawa na kusema kwamba kutokuwepo na pembetatu yoyote yenye nyuzi 360 kunathibitisha kuna pembetatu ambayo pia ni duara yenye nyuzi 360.

Mimi nakwambia thibitisha hiyo pembetatu ambayo pia ni duara ipo na si hadithi tu.

Unawayawaya.

Thibitisha huyo Mungu unayemsema yupo, yupo kweli, na si hadithi tu.

Hujathibitisha.
 
Wewe hujui herufi za Kiswahili tu.

Hujui tofauti ya "mara" na "mala".

Labda kabla ya kuparamia habari za uwepo wa Mungu, jifunze Kiswahili.

Hapo ulichoandika ni sawa na kusema kwamba kutokuwepo na pembetatu yoyote yenye nyuzi 360 kunathibitisha kuna pembetatu ambayo pia ni duara yenye nyuzi 360.

Mimi nakwambia thibitisha hiyo pembetatu ambayo pia ni duara ipo na si hadithi tu.

Unawayawaya.

Thibitisha huyo Mungu unayemsema yupo, yupo kweli, na si hadithi tu.

Hujathibitisha.
Mkuu mimi siwayiwayi, nimekupa uthibitisho ulio wazi kabisa kwa ushahidi unaoonekana kwa macho. nimeshakuthibitishia kwamba Mungu yupo na ndiye alieumba ulimwengu huu unaoonekana kwa macho(sayari zote na vyote vilivyomo) na usioonekana kwa macho (malaika n.k) sizungumzi vitu porojo bali nazungumza ukweli na uhakika.
 
Samahani sana mkuu, huku wengi tumelikosa hilo tukio, kisa kutafuta, hali ngumu kaka yetu huku, ya Saturn na Jupiter kwenu, sisi twawaza kupata unga, maharage, nguo za shule za watoto, ada, bima, kodi, nauli kwenda kutafuta, wapi tutakopa January hii,.....yaani...Acha tu..
 
Mkuu mimi siwayiwayi, nimekupa uthibitisho ulio wazi kabisa kwa ushahidi unaoonekana kwa macho. nimeshakuthibitishia kwamba Mungu yupo na ndiye alieumba ulimwengu huu unaoonekana kwa macho(sayari zote na vyote vilivyomo) na usioonekana kwa macho (malaika n.k) sizungumzi vitu porojo bali nazungumza ukweli na uhakika.
Unajuaje aliyeumba ulimwengu ni Mungu, na kwamba habari hiyo si hadithi iliyotungwa na watu tu kwa sababu hawajui ulimwengu umetokea vipi na hawataki kukubali kwamba hawajui ulimwengu umetokea vipi?
 
Unajuaje aliyeumba ulimwengu ni Mungu, na kwamba habari hiyo si hadithi iliyotungwa na watu tu kwa sababu hawajui ulimwengu umetokea vipi na hawataki kukubali kwamba hawajui ulimwengu umetokea vipi?
Nilishakujibu hili swali kwenye post #150, kutokana na swali kama hili uliloniuliza sasa hivi. Rejea vizuri hiyo post Mkuu
 
Nilishakujibu hili swali kwenye post #150, kutokana na swali kama hili uliloniuliza sasa hivi. Rejea vizuri hiyo post Mkuu
Post #150 umeandika hivi.

"Nimekupa uthibitisho wa uumbaji wake nikakutajia mpaka vitu alivyoumba , ninajua kwamba Mungu ndiye alieumba vitu hivyo kwa maana hakuna kiumbe yoyote anayeweza kuumba ulimwengu usioonekana (malaika n.k) na ulimwengu huu unaoonekana(sayari zote na vyote vilivyomo), najua kwamba Mungu yupo kwa ushahidi wa uumbaji wake, hakuna kitu kinaweza kutokea bila muumbaji"

Nakuuliza hivi.

Unajuaje kwamba huo unaouita uumbaji wake ni uumbaji wake kweli, na kwamba, hiyo habari ya "uumbaji wake" si hadithi za watu tu wanaosema huu ni uumbaji wake kwa sababu hawajui uumbaji huu umetokea vipi?

Kujua kwamba hakuna kiumbe anayeweza kuumba uumbaji huo hakuthibitishi Mungu yupo wala kaumba.

Kunathibitisha hakuna kiumbe anayeweza kuumba uumbaji huo tu.

Kuthibitisha kwamba hakuna Mjerumani aliyekuzaa wewe, hakuthibitishi wewe Mama yako ni malaika.

Kunathibitisha hakuna Mjerumani aliyekuzaa wewe.

Ulichoandika hapo ni sawa na kusema wewe lazima mama yako ni malaika, kwa sababu hakuna Mjerumani aliyekuzaa.

Unaunganisha vitu viwili ambavyo havina uhusiano.

Logical non sequitur.

Unajuaje Mungu yupo na ndiye muumbaji na habari hiyo si hadithi ya watu wasioweza kuelezea uumbaji umetokeaje tu?

Hujajibu swali hili.
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom