Mliofuatilia tukio la JNHPP wamesema mradi unakamilika lini?

saidoo25

JF-Expert Member
Jul 4, 2022
602
1,407
Kwa mliofanikiwa kufuatilia tukio la jana Disemba 22, 2022 la kuanza kujaza maji Bwawa la JNHPP wamesema mradi utakamilika lini. bahati mbaya mimi umeme ulikuwa umekatika sikuweza kufuatilia kwenye TV.

Hadi kufikia jana Naibu Waziri wa Nishati alisema Bunge lililopita la Novemba kuwa mradi utakwisha Juni 2023 japo kwa mujibu wa Mkataba ilikuwa mradi ukamilike Juni 2022.

Kwa mliosikiliza tukio la jana wamesema mradi utakamilika lini na kuanza uzalishaji.

Rejea mkanganyiko uliotokea bungeni baina ya Spika, Dk. Tulia Ackoson, Naibu Waziri wa Nishati Byabato na Waziri Simbachawene ambao wote walishindwa kulieleza Bunge tarehe rasmi ya kukamilika kwa mradi.

Spika alimuagiza Waziri Mkuu atoe taarifa rasmi ya mradi huo bungeni au sehemu yoyote nje ya bunge kuwaeleza watanzania ukweli kuhusu kumalizika kwa mradi huo.

Swali la mwisho madai ya Serikali kwa Mkandarasi Kampuni ya Arab Contractors ya Trilioni 1.5 za kuchelewesha mradi nayo wamesemaje kwenye tukio la jana.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
changa la macho hilo tukio la jana ni la kisiasa zaidi kuliko uhalisia we subiri na ndio mana tarehe maalum na mwaka haujatajwa
 
Kwa mliofanikiwa kufuatilia tukio la jana Disemba 22, 2022 la kuanza kujaza maji Bwawa la JNHPP wamesema mradi utakamilika lini. bahati mbaya mimi umeme ulikuwa umekatika sikuweza kufuatilia kwenye TV.

Hadi kufikia jana Naibu Waziri wa Nishati alisema Bunge lililopita la Novemba kuwa mradi utakwisha Juni 2023 japo kwa mujibu wa Mkataba ilikuwa mradi ukamilike Juni 2022.

Kwa mliosikiliza tukio la jana wamesema mradi utakamilika lini na kuanza uzalishaji.

Rejea mkanganyiko uliotokea bungeni baina ya Spika, Dk. Tulia Ackoson, Naibu Waziri wa Nishati Byabato na Waziri Simbachawene ambao wote walishindwa kulieleza Bunge tarehe rasmi ya kukamilika kwa mradi.

Spika alimuagiza Waziri Mkuu atoe taarifa rasmi ya mradi huo bungeni au sehemu yoyote nje ya bunge kuwaeleza watanzania ukweli kuhusu kumalizika kwa mradi huo.

Swali la mwisho madai ya Serikali kwa Mkandarasi Kampuni ya Arab Contractors ya Trilioni 1.5 za kuchelewesha mradi nayo wamesemaje kwenye tukio la jana.

Mungu Ibariki Tanzania.
Walisema Mungu akipenda litakamilika
 
Mradi umesogezwa mbele, utakamilika juni 2024 kwa sasa ukiwa umekamilika kwa karibu 73%. Na pesa zilizotumika ni kodi za watanzania na hatujakopa nje.
 
Ma ccm sio ya kuamini utashangaa bwawa linaanza operation 2025 humu katikati ni kupeana migao tuu. Hadi invoice za wauza majenereta zimalizike
 
Back
Top Bottom