Wana Jamvi naomba kuuliza.
Nimeona matangazo mengi kuhusu kuupigia kura Mlima Kilimanjaro uwepo kati ya maajabu saba ya Dunia. Mimi kama mwenyeji wa mkoa huu na mkazi wa maporomoko ya mlima huo nimeshindwa kuelewa ni nini faida kwetu sisi wakazi kama mlima huo ukiingizwa kwenye orodha ya maajabu saba ya dunia.
Tumeshuhudia maeneo kama ngorongoro ambapo kitendo cha kuwepo kwenye orodha ya urithi wa dunia kimefanya eneo hilo liwe msumari wa moto kwa wamasai na wasonjo ambao ni wakazi wa asili. Wenyeji wakitumia eneo hilo wanaambiwa wanaharibu urithi wa dunia, ila mwarabu anapokuja kuua na kukamata na kusafirisha wanyama, mahoteli makubwa yanapojengwa kwenye mapito ya wanyama, hakuna taabu. Ukiangalia mbuga ya Selous, mzungu anaruhusiwa kuchimba Uranium lakini kwa mwafrika hata kuchota maji mbugani ni taabu.
Wasiwasi wangu ni kuwa mlima huu ukiingia katika maajabu saba ya dunia inaweza ikawa sababu ya wenyeji kunyang'anywa ardhi yao kwa kisingizio cha kutunza maajabu ya dunia halafu ikapewa wazungu/wawekezaji.
Nimeona matangazo mengi kuhusu kuupigia kura Mlima Kilimanjaro uwepo kati ya maajabu saba ya Dunia. Mimi kama mwenyeji wa mkoa huu na mkazi wa maporomoko ya mlima huo nimeshindwa kuelewa ni nini faida kwetu sisi wakazi kama mlima huo ukiingizwa kwenye orodha ya maajabu saba ya dunia.
Tumeshuhudia maeneo kama ngorongoro ambapo kitendo cha kuwepo kwenye orodha ya urithi wa dunia kimefanya eneo hilo liwe msumari wa moto kwa wamasai na wasonjo ambao ni wakazi wa asili. Wenyeji wakitumia eneo hilo wanaambiwa wanaharibu urithi wa dunia, ila mwarabu anapokuja kuua na kukamata na kusafirisha wanyama, mahoteli makubwa yanapojengwa kwenye mapito ya wanyama, hakuna taabu. Ukiangalia mbuga ya Selous, mzungu anaruhusiwa kuchimba Uranium lakini kwa mwafrika hata kuchota maji mbugani ni taabu.
Wasiwasi wangu ni kuwa mlima huu ukiingia katika maajabu saba ya dunia inaweza ikawa sababu ya wenyeji kunyang'anywa ardhi yao kwa kisingizio cha kutunza maajabu ya dunia halafu ikapewa wazungu/wawekezaji.