marejesho
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 6,636
- 3,655
Nawasalimu wanaJF kwa upendo ..
Leo mida ya saa nne hivi asubuhi, tumepata mgeni wa kushtukiza ofisini (BUBU).. Mgeni huyu kwa njia anazojua yeye,alibahatika kumdanganya mlinzi(mzembe) na kuruhusiwa kuingia moja kwa moja mjengoni.
Huyu jamaa ni pande la mtu, kavaa smart sana na ni mtu anayejiamnini ..
Aliingia na kuanza kumsalimia mmoja wetu kwa kumpa mkono, na kukabidhi makaratasi aliyokuwa nayo... Zilikuwa ni barua za kuomba msaada.. Kwa vile hatuna utaratibu wa kampuni kama kampuni kutoa msaada, watu waliokuwa na huruma walianza kujisearch angalau kumsaidia kwa chochote.. Mmoja alitoa Tshs 5,000/=, mwingine akaingiza mkono mfukoni ikatoka Tshs 1000/= huku wengine wakiendelea kutafuta walichonacho...
Jamaa alikuwa pembeni akiangalia zoezi zima kwa dharau fulani, akasimama na kukusanya makaratasi yake na kuondoka akionyesha ishara kwamba haitaji hizo fedha.... Hatukuamini macho yetu pale alipoziacha kweli na kuchapa mwendo... Kufika eneo la gate, akatuachia hii barua fupi (ATTACHED)ambayo imetuachia sisi maswali mengi sana..
1.Hivi msaada ni lazima au hiari?
2.Mtu anapangiliaje matumizi ya fedha za mwenzake?
Au alikuwa mwanga?
Chukueni tahadhari. Madame B, PakaJimmy , Filipo , Erickb52 , Preta , Mungi Kaizer Babu DC , Arushaone , Mzee wa Rula , St. Paka Mweusi , majany Nicas Mtei Boflo LiverpoolFC , Mr Rocky , Blaki Womani and MANY OTHERS
Leo mida ya saa nne hivi asubuhi, tumepata mgeni wa kushtukiza ofisini (BUBU).. Mgeni huyu kwa njia anazojua yeye,alibahatika kumdanganya mlinzi(mzembe) na kuruhusiwa kuingia moja kwa moja mjengoni.
Huyu jamaa ni pande la mtu, kavaa smart sana na ni mtu anayejiamnini ..
Aliingia na kuanza kumsalimia mmoja wetu kwa kumpa mkono, na kukabidhi makaratasi aliyokuwa nayo... Zilikuwa ni barua za kuomba msaada.. Kwa vile hatuna utaratibu wa kampuni kama kampuni kutoa msaada, watu waliokuwa na huruma walianza kujisearch angalau kumsaidia kwa chochote.. Mmoja alitoa Tshs 5,000/=, mwingine akaingiza mkono mfukoni ikatoka Tshs 1000/= huku wengine wakiendelea kutafuta walichonacho...
Jamaa alikuwa pembeni akiangalia zoezi zima kwa dharau fulani, akasimama na kukusanya makaratasi yake na kuondoka akionyesha ishara kwamba haitaji hizo fedha.... Hatukuamini macho yetu pale alipoziacha kweli na kuchapa mwendo... Kufika eneo la gate, akatuachia hii barua fupi (ATTACHED)ambayo imetuachia sisi maswali mengi sana..
1.Hivi msaada ni lazima au hiari?
2.Mtu anapangiliaje matumizi ya fedha za mwenzake?
Au alikuwa mwanga?
Chukueni tahadhari. Madame B, PakaJimmy , Filipo , Erickb52 , Preta , Mungi Kaizer Babu DC , Arushaone , Mzee wa Rula , St. Paka Mweusi , majany Nicas Mtei Boflo LiverpoolFC , Mr Rocky , Blaki Womani and MANY OTHERS
Attachments
Last edited by a moderator: