Mlemavu msomi

marejesho

JF-Expert Member
Jan 6, 2011
6,636
3,655
Nawasalimu wanaJF kwa upendo ..

Leo mida ya saa nne hivi asubuhi, tumepata mgeni wa kushtukiza ofisini (BUBU).. Mgeni huyu kwa njia anazojua yeye,alibahatika kumdanganya mlinzi(mzembe) na kuruhusiwa kuingia moja kwa moja mjengoni.
Huyu jamaa ni pande la mtu, kavaa smart sana na ni mtu anayejiamnini ..

Aliingia na kuanza kumsalimia mmoja wetu kwa kumpa mkono, na kukabidhi makaratasi aliyokuwa nayo... Zilikuwa ni barua za kuomba msaada.. Kwa vile hatuna utaratibu wa kampuni kama kampuni kutoa msaada, watu waliokuwa na huruma walianza kujisearch angalau kumsaidia kwa chochote.. Mmoja alitoa Tshs 5,000/=, mwingine akaingiza mkono mfukoni ikatoka Tshs 1000/= huku wengine wakiendelea kutafuta walichonacho...

Jamaa alikuwa pembeni akiangalia zoezi zima kwa dharau fulani, akasimama na kukusanya makaratasi yake na kuondoka akionyesha ishara kwamba haitaji hizo fedha.... Hatukuamini macho yetu pale alipoziacha kweli na kuchapa mwendo... Kufika eneo la gate, akatuachia hii barua fupi (ATTACHED)ambayo imetuachia sisi maswali mengi sana..

1.Hivi msaada ni lazima au hiari?
2.Mtu anapangiliaje matumizi ya fedha za mwenzake?

Au alikuwa mwanga?

Chukueni tahadhari. Madame B, PakaJimmy , Filipo , Erickb52 , Preta , Mungi Kaizer Babu DC , Arushaone , Mzee wa Rula , St. Paka Mweusi , majany Nicas Mtei Boflo LiverpoolFC , Mr Rocky , Blaki Womani and MANY OTHERS
 

Attachments

  • MLEMAVU MSOMI.jpg
    MLEMAVU MSOMI.jpg
    44.1 KB · Views: 74
Last edited by a moderator:
duh anakuja akiwa na mawazo kuwa atapata laki moja moja na sio hizo za kwenu
Kuna watu wana dharau sana aise yaani unampa msaada halafu anauangalia mara mbili mbili yaani kusema kuwa haumtoshi na hakupangilia kukpata kiasi hicho kutoka kwako as if anajua mfukoni kwako kuna nini au umejipangaje aise
Pole sana marejesho hao ndio waomba msaada
 
Last edited by a moderator:
duh anakuja akiwa na mawazo kuwa atapata laki moja moja na sio hizo za kwenu
Kuna watu wana dharau sana aise yaani unampa msaada halafu anauangalia mara mbili mbili yaani kusema kuwa haumtoshi na hakupangilia kukpata kiasi hicho kutoka kwako as if anajua mfukoni kwako kuna nini au umejipangaje aise
Pole sana marejesho hao ndio waomba msaada

Asante Mr Rocky . Kwa kweli huyu jamaa (MLEMAVU MSOMI) amenihuzunisha sana.. Ameniweka katika wakati mgumu,kiasi kwamba hata wengine wakija wale wanaohitaji msaada wa kweli itakuwa ni vigumu kuwasaidia .......
 
Last edited by a moderator:
watu wenye ulemavu wanakuwaga na hasira sana,na wengi hawajiamini,nahisi na malezi pia yamechangia.....majibu haya hapa
**kusaidia mtu ni jambo la hiari,na kupangia hela za mwenzako labda mlishirikiana kuzitafuta au mna special connection kama ndoa** mawazo yangu tu hayo
 
Asante Mr Rocky . Kwa kweli huyu jamaa (MLEMAVU MSOMI) amenihuzunisha sana.. Ameniweka katika wakati mgumu,kiasi kwamba hata wengine wakija wale wanaohitaji msaada wa kweli itakuwa ni vigumu kuwasaidia .......

Sana na tatizo hawajui kuwa wanafunga milango ya wengine wenye shida kweli kusaidiwa maana hata akija mtu mwingine mwenye shida kweli mawazo ya watu yatakuwa yanamuwaza yule alikataa msaada tena kwa kejeli aise
Pole sana marejesho
 
Last edited by a moderator:
Mie siwapagi,kuna jamaa mmoja alikuwaga anakuja pale UDSM,kila mwaka anaomba fedha za kumchangia nauli,first year nilimchangia...nikashangaa wakati niko 2nd year akarudi na sound zilezile......NILINAWA MIKONO........!!
Labda nimkute church na kiongozi atuhamasishe la sivyo..kalaghabaho
 
Sana na tatizo hawajui kuwa wanafunga milango ya wengine wenye shida kweli kusaidiwa maana hata akija mtu mwingine mwenye shida kweli mawazo ya watu yatakuwa yanamuwaza yule alikataa msaada tena kwa kejeli aise
Pole sana marejesho

Usemayo ni kweli kabisa Mr Rocky
 
Last edited by a moderator:
Mie siwapagi,kuna jamaa mmoja alikuwaga anakuja pale UDSM,kila mwaka anaomba fedha za kumchangia nauli,first year nilimchangia...nikashangaa wakati niko 2nd year akarudi na sound zilezile......NILINAWA MIKONO........!!
Labda nimkute church na kiongozi atuhamasishe la sivyo..kalaghabaho

Hili ni Janga la Kijamii..
 
Duh! Pole sana marejesho! Ikute alitaka dola huyo... si unajua msomi+$=mwake..
BTW nimeshangaa sana!!!!
 
Last edited by a moderator:
Urudi kufanya nini? Ishia hukohuko mwalimu msomi.
Nitarudi.

Afu Asprin kama unanitaka si uniambie tu.
Sio kujipitisha pitisha mbele yangu.
Una Ashuo la Panya,Kujipitisha kwa Wageni.
 
Last edited by a moderator:
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom