Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 9,995
- 34,607
Miongoni mwa habari kubwa kwa sasa hapa nchini inayozungumziwa ni kuhusu mkwamo wa ununuaji na ubanguaji wa korosho. Hali ya mambo sio nzuri tena. Tumekwama.
Kila mtu anamtupia mpira mwenzake. Jeshi limeshanawa mikono kwa kusema linakwamishwa na utendaji wa taratibu na urasimu wa maafisa husika, timu ya wataalamu inasema zoezi la kubangua huenda litachukua miaka 2-14, Waziri husika ameamua kuwapigia magoti wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi waje tena mezani kununua na kubangua korosho, wakulima nao wanalalamika kudhulumiwa korosho zao kinguvu. Kiujumla mambo yameharibika.
Hakuna tena sababu ya kusubiri au kutafuta mchawi bali ni wakati muafaka wa kwenda kuokoa jahazi, na shughuli za uokozi zinapaswa kufanywa na wazalendo zaidi. Na sote tunajua, wazalendo halisi wako CCM.
WanaCCM msisubiri kuja kupongeza tu kila mara, ila sasa ndio wakati muafaka wa kuonyesha uzalendo wenu kwa vitendo. Chonde chonde popote pale mlipo, makada wa CCM jitoeni kimasomaso kwenda kusini kununua na kubangua korosho. Wakati ndio huu.
CCM Oyeee.
Hapa kazi tu.
Kila mtu anamtupia mpira mwenzake. Jeshi limeshanawa mikono kwa kusema linakwamishwa na utendaji wa taratibu na urasimu wa maafisa husika, timu ya wataalamu inasema zoezi la kubangua huenda litachukua miaka 2-14, Waziri husika ameamua kuwapigia magoti wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi waje tena mezani kununua na kubangua korosho, wakulima nao wanalalamika kudhulumiwa korosho zao kinguvu. Kiujumla mambo yameharibika.
Hakuna tena sababu ya kusubiri au kutafuta mchawi bali ni wakati muafaka wa kwenda kuokoa jahazi, na shughuli za uokozi zinapaswa kufanywa na wazalendo zaidi. Na sote tunajua, wazalendo halisi wako CCM.
WanaCCM msisubiri kuja kupongeza tu kila mara, ila sasa ndio wakati muafaka wa kuonyesha uzalendo wenu kwa vitendo. Chonde chonde popote pale mlipo, makada wa CCM jitoeni kimasomaso kwenda kusini kununua na kubangua korosho. Wakati ndio huu.
CCM Oyeee.
Hapa kazi tu.