ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Kwa kweli Mkuu wetu wa nchi anajitahidi sana kutafuta wawekezaji toka nchi mbalimbali kuja kuwezeza Nchini Tanzania. haieleweki kikwazo nini. AKiwa nchini Brazil, mwezi Aprili, 2012 Mhe. Rais alitembelea na kuongea na Chama Cha wafanyabiashara na Wawekezaji wa nchi hiyo,na kama kawaida walieleza maeneo ya vivutio lukuki vya uwekezaji, lakini ya furahisha ni hii ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza ndege na kuwaomba walisaidie shirika la ndege la Tanzania (ATC) kupata ndege mpya....(khaaa, mkuuu!!!, kivipi?)
Hivi kwa nini tanzania panafaa kwa uwekizaji?
(i) Kuna amani na utulivu
(ii) kuna watu zaidi ya 40milioni
(iii) Tanzania mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na bado majadiliano bado yanaendelea kuyafikia masoko ya kimataifa ikiwamo Marekani na nchi za Ulaya ambako tunapeleka kila kitu tunachozalisha isipokuwa Silaha.
Hivi kwa nini tanzania panafaa kwa uwekizaji?
(i) Kuna amani na utulivu
(ii) kuna watu zaidi ya 40milioni
(iii) Tanzania mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na bado majadiliano bado yanaendelea kuyafikia masoko ya kimataifa ikiwamo Marekani na nchi za Ulaya ambako tunapeleka kila kitu tunachozalisha isipokuwa Silaha.