Hahari yenyewe eti-Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mh Kisare Makori,anasema ameamua kumkamata Meya wa Halmashauri ya Ubungo na kuagiza Polisi wamuweke ndani sababu amekiuka taratibu za kazi kwa kuwaleta wanachama wa CHADEMA wa kanda ya Pwani na kuwatembeza katika miradi ya maendeleo ya halmashauri ya Ubungo ambayo inaongozwa na CHADEMA.
Hivi Meya wa Ubungo hilo eneo si ndilo eneo lake la kazi iweje akiwa katika eneo lake la kazi akamatwe ? Haya ni matumizi ya hovyo kabisa ya madaraka kwa Mkuu wa wilaya huyo, inafanana kabisa na Mkuu wa wilaya huyo kukamatwa kisa amekutwa na bahasha za tanzania government ofisini kwake sasa kumbe bahasha hizo zikutwe wapi? Au kumkamata polisi kisa amevaa kofia ya polisi sasa kumbe avae nini na yuko kazini? Au kumkata daktari mazani kwake na stetoscope shingoni sasa daktari stetoscope awe nayo wapi?
Mstahiki meya amekamatwa akiwa eneo lake la kazi hakuwa Temeke ambapo ni wilaya ingine sasa mkuu wa wilaya huyo anataka Meya wa Ubungo akafanyie wapi kazi?
Huu ni ulevi wa madaraka uliokithiri kwa mkuu wa wilaya huyo, na kama kujikomba kwa bosi basi ujikombaji huu umevuka mpaka.