Mkuu wa Wilaya ya Kyela asimamishwa kazi baada ya kufumaniwa na mkewe


Wakuu naomba kuuliza hivi kuwa DC wa Wilaya ni lazima uwe member wa CCM au? Eti hata ishu za uzinzi nazo ni za vyama pia?

Na hii habari hivi ni kweli ina ukweli? Kweli kuna kiongozi wa Tanzania amekuwa releived power kwa sababu ya hawara? Mbona wengine wamesafiri nao huko NY?

Naomba mwenye ukweli anihakikishie kwua hii habari ni ya kweli.

Ndio maana huwa nasema hatuwezi tukajikita katika mijadala iliyo based on mtu kusikia sikia!

Umewahi kuona wapi Sheria ina enforce maadili ya kuto chiti kwenye ndoa ?

Na hata kama ingekuwepo, kuna kitu katika Katiba ya Tanzania kinaitwa "equal protection" au "legal process," au sehemu nyingine duniani wanakiita "due process" of law. Kabla ya kuchukuliwa hatua kama hizo ilibidi huyu mfumaniwa Uzinzi nae asikilizwe (kitu ambacho Lowassa alilia Mwakyembe hakumfanyia, ) na awe na haki ya rufaa, na ifuatwe misingi anuwai ya ushahidi. Sio mke kakuta "mwizi" kimada halafu Mkuu wa wilaya akafukuzwa kazi baada ya hapo.

Haki ya Usawa mbele ya Sheria:
Sehemu ya 3, Ibara ya 13, Kipengele 6 (a)

Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria, Mamlaka ya Nchi itaweka taratibu zinazofaa au zinazozingatia misingi kwamba:
wakati haki na wajibu wa mtu yeyote vinahitaji kufanyiwa uamuzi wa mahakama au chombo kinginecho kinachohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na pia haki ya kukata rufaa au kupata nafuu nyingine ya kisheria kutokana na maamuzi ya mahakama au chombo hicho kingenecho kinachohusika;
 
Dah !!, Je raisi naye akishikwa kwa mtindo huo ina maana nchi itakaimiwa na rais wa Kenya??
 
1.
Inaelekea sababu sio kuwa na hawara bali zogo lililotokea na kumfanya DC adharauliwe na wananchi anaotakiwa kuwaongoza.

2.
Ndio maana huwa nasema hatuwezi tukajitika katika mijadala iliyo based on mtu kusikia sikia! Umewahi kuona wapi Sheria ina enforce maadili ya kuto chiti kwenye ndoa ?

Hapana mkuu, tunaweza kujikita kwenye mijadala, au kujenga hoja based on habari za kusikia, uamuzi ni wananchi wa hapa JF iwapo wanataka kukuamini mleta habari au hapana, reading between the lines ya hii habari ni kwamba ninaamini kuwa kwenye kukamatwa huyo mkuu, kulitokea zogo kubwa na ninafahamu kuwa kila Wilaya ina mkuu wa uwt, ambaye atakuwa alimuarifu RC mara moja na the whole situation na ninaamini kuwa RC ambaye ana uwezo kisheria wa kumuapisha DC, aliamia kum-relieve yule DC madaraka kwa muda ili kuepusha shari kutokana na lile zogo, kama sheria inavyomruhusu,

Kwa sababu DC huchaguliwa na rais kwa hiyo ni rais peke yake ndiye anayeweza kumfukuza kazi, meaning kwamba huyu DC amesimamishwa kwa sababu ya kuepusha zogo na hivyo kushusha heshima ya serikali, lakini siamini kuwa amefukuzwa kazi au amefikishwa kwenye mikono ya sheria, nafikiri mleta habari hakuileta kama inavyotakiwa either kwa makusudi au kwa kutokuwa na all the facts to the ishu,

JF tutaendelea kuwa na mijadala ya habari based on kusikia, kwa sababu hapa hakuna watu wajinga, sijawahi kuona habari yoyote ya hapa ikipita bila kuchujwa, ambayo imekaa ki-design design hata iwe imeandikwa na nani, wananchi hapa wasichotaka ni hoja based on chuki za binafsi, au kuvuruga mijadala tu bila sababu maalum, halafu wakati mwingine ni vyema unapoona habari haina muelekeo, unaidharau na inajifia kifo cha mende, kuulizia ukweli ni wajibu lakini sio lazima iwe kwa ugomvi.

Leo umeona Mkulu Invisible, ameanzisha topic ya kumsifu member mmoja hapa kwa kufikisha namba flani, lakini so far hakuna aliyeigusa sasa unafikiri kweli members hapa ni wajinga, serikali ilipotupa taabu haikuwahi kusema kuwa sisi ni waongo, ila ilitaka kujua tunapata wapi habari nyeti, na hilo siku zote ndio swali kubwa toka kwa viongozi wa juu, nimelisikia hili swali time and time again,

Yes kuna habari zinahitaji clarifications na kuna ambazo ni kutumia common sense, na kuna kumuuliza mleta habari ukweli wa ile habari kwa lugha ya kistaarabu, I mean huwezi kukurupuka na kuanza kuwaita watu wazima kuwa ni waongo, au wanatoa habari ambazo ni bizzare, I mean hapo kuna kukosa heshima kwa sababu wewe unayerusha hayo maneno huna uhakika au ukweli, halafu hata wewe sometime pia unatumia habari hizo hizo za kusikia, ukiisoma vizuri hii habari unaona kabisa ukweli ulipo na uongo ulipo,

Tutaendelea kukata ishus kwa habari za kusikia, lakini kama kawaida tunakuwa waangalifu kitu ambacho hapa JF hakijawahi kuwa tatizo. Mkuu Mtanzania, ni mtu ninayemuaminia kwa hiyo ndio maana ninaamini kuwa hii habari ni kweli lakini tumepunjwa facts tu za exctly kilichomtokea DC.
 
(kitu ambacho Lowassa alilia Mwakyembe hakumfanyia, ) na awe na haki ya rufaa, na ifuatwe misingi anuwai ya ushahidi. Sio mke kakuta "mwizi" kimada halafu Mkuu wa wilaya akafukuzwa kazi baada ya hapo.

Mkuu siku zote mimi nina tatizo sana na hii hoja, Lowassa aliajribu kutumia kila mbinu kuuharibu uchunguzi wa kamati, aliposhidwa akajaribu kutumia hela, aliposhindwa akaenda kwa rais kuomba msaada rais akakataa na kuambiwa akajitete kwenye bunge la wananchi, aliposhindwa akajaribu kui-counterfeit ile ripoti kwa kuipachika ya uongo kama alivyofanya kwenye ripoti ya Hosea, aliposhindwa sasa mbele ya umma yaani bungeni akakimbia,

Great kwa msomi kama Lowassa nilitegemea kuwa baada ya kukimbia bungeni sasa ataenda kwenye sheria, he did not, badala yake akaenda jimboni kutoa kilio chake, eti after all this Lowassa hakupewa haki? Haki ipi hiyo?

Hivi mkuu ni wananchi wangapi wa Tanzania wanapatiwa nafasi kama hizo zote alizopewa Lowassa mpaka leo?
 
Mkuu wa wilaya ya Kyela kasimamishwa kazi baada ya kufumaniwa na mkewe akiwa na mwanamke mwingine. Inasemekana huyu mkewe anasoma Dar. Alipata habari na kuamua kutinga Kyela kimya kimya. Alipofika na kukuta huyo mwanamke ndani, akapiga kelele za mwizi na kusababaisha vurugu kubwa.

Kwasasa mkuu wa wilaya ya Ileje ndiye kapelekwa Kyela, sijui kama ni kwa muda au la.

Mleta hoja hakusema kafukuzwa bali kasimamishwa. Nadhani ni kawaida mtu kusimamishwa wakati uchunguzi unafanyika kuhusu tuhuma dhidi yake. Tatizo ni kuwa huyu si wa kwanza kufumaniwa, kufanyiwa fujo (wengine mpaka mali ya serikali iliharibiwa) n.k. Inaonekana hii sheria (kama ipo) inatumika kwa upendeleo. Au kosa ni kufumaniwa na si adultery? Huyu mheshimiwa inaelekea alikuwa anatembea na huyo binti waziwazi ( mpaka habari zifike Dar lazima Kyela nzima watakuwa wanajua) na hatua imechukuliwa baada ya kufumaniwa tu! Je kuwa na kimada wazi wazi hakuonekana kudhalilisha ofisi? Mimi naona huu ni mfano wa hypocrisy iliyotawala jamii yetu.
 
A word of caution. Chonde chonde, tusiupeleke huu mjadala kule tulikoenda kwenye mjadala wa stahili za wastaafu. Tujibu hoja badala ya kurudia rudia yale yasiyomo kwenye mjadala HUU! Tutauharibu.
 
Kwa namna moja au nyingine wote mliotoa maoni mnamatatizo. Hawa wawili walisaini ndoa ya mke/mme mmoja ndiyo maana yeyote atakayekutwa akifungua tabernakulo upande wowote hana jina jingine zaidi ya mwizi.tusihalalishe wizi eti kwa sababu tumezoea kuiba/kuibiwa
 
Huyo mkuu wa wilaya kama sijakosea ni Muislam kwahiyo dini yake na sheria za nchi zinamruhusu kuoa zaidi ya mke mmoja. Kule Kyela mtu kuoa sio lazima uende kanisani au
kwa mkuu wa wilaya. Unapeleka ng'ombe tu kwa wenye mtoto, kula wali hapo na kunywa, tayari ndoa imefungwa kimila.

Kuna kipindi JK aliwaonya wakuu wa wilaya kutojidharirisha huko wilayani kwa kukopa, kuchukua wake za watu au kulewa. nafikiri ile hotuba ilikuwa hapa pia. Huenda ndio hatua hizo.

Mimi naifuatilia hii habari, kitu ambacho nime confirm ni kwamba ni kweli jamaa kasimamishwa kazi na mkuu wa wilaya ya Ileje tayari yupo Kyela aki act kama DC wa Kyela.

Pia nime confirm huko kufumaniwa wiki moja kabla ya kusimamishwa kazi.

Viongozi mbalimbali wa wilaya wanasema hiyo ndio sababu iliyomfanya asimamishwe. Ila sina confirmation 100% kwamba ni kweli kasimamishwa kwasababu ya hilo zogo.

Tuendelee kufuatilia habari na labda waandishi wa habari watusaidie.
 
Ajari kazini tuu ayo mambo kwa viongozi wa sasa ni suala la kawaida tuu.
Nampa pole mkuu wa wilaya hakuwa na jinsi si unajua alishaonja asali mpaka akapitiliza na kumbuka nyumba ndogo kwa manjonjo yaaani wee acha.Pole ingawa ndo wamekutoa kafara!!!!!!
 
Huyo mke nae mjinga angeyamaliza na mme wake au kifamilia tu!sasa kumchafua mme wake ndo nini?kina magufuli hadi wana vimada na mke anajua na anaishi na mtoto wa kimada wa magufuli!
Sijafurahia kitendo cha mke wa huyu mkuu wa wilaya!mimi siwezi muabisha namna hii mme wangu!wangeyamaliza kibusara tu!
FIRST LADY huwezi jua katendwa mara ngapi, yawezekana uvumilivu ulifikia kikomo,
 
mie nafikiri huyo mama DC hajakosea hata kidogo, mwizi ni mwizi tu haijalishi kaiba nini..hata ningekuwa mimi ningefanya hivyo hivyo..halafu nikiondoka hapo sirudi teena kama kuna talaka itanifuata huko huko niliko...yaani mtu ana chiti kwa raha zake na uhuru hadi anamleta bedroom kabisa? hata kama angekuwa ameoa ghafla si angesema tu kuliko kumuingiza mtu nyumbani mkewe akiwa hayupo?
 
Nona jinsi kila mtu anavyoijadili hii maada, mwanaume amefanya kosa la kufanya part time. Watu tunaona mkewe kakosea kwa sababu wanaume wanaona wana haki ya kuanya kazi za nje. Jamaa kaharibu, na amejiabisha wala si mkewe aliyemwaibisha. Na Kyela inavyotisha kwa ngoma lakini watu bado hawaachi kazi za nje. Tutakufa kama kuku . sasa huyo mkuu wa wilaya alikuwa anawaeleza nini kyela kuhusu ngono uzembe. tutamalizika sote namna hii.
...Mwakaleli una uhakika alifanya ngono Zembe??? nadhani small house ndio tatizo hapa ukizingatia jamaa ana mke na huyo DC sidhani kama anaweza kula small house chukuchuku....Salama Sh.200 tu ajitoe mhanga!??
 
Huyu mheshimiwa amerudi kituoni kwake kuendelea na kuandaa ujio wa rais JK hapo Kyela tarehe 10 Oct. kama hataahirisha tena.

Huenda jamaa kashinda hiyo case, sina uhakika.
 
Hivi cheo cha mume kina thamani kuliko feelings za mke...hata kama mi masikini wewe mume waziri...ukichiti na deal na wewe kama ambavyo ninge deal na mume muendesha mkokoteni...cheo mwisho wake getini...

Ndio maana wake wa waheshimiwa wamebaki wake jina...wamewaendekeza sana waume zao mpaka wamekuwa cheaters sugu...
 
Huyo Mama ni janja yake tu...Sasa ina maana kuwa alirudi kutoka Dar kuja kufumfumania mwizi aliyeletwa na mume wake kuja kuiba mali zao?

Kiutaratibu alitakiwa kumwuliza mumewe ni kwanini kaleta mwizi ndani ya nyumba na si kupiga kelele...Na kama asipodai talaka basi huko Dar kasukwa kwa minajili ya kisiasa..Sasa ni ethier aombe talaka ama afunguwe mashitaka ya uwizi wa mwanamke huyo kwa kushirikiana na mumewe..Otherwise ni mambo ya siasa tu yanaingizwa ndani ya familia...Kweli siasa ni ulaji...
.
Tumshaona mambo ya wake kushiriki kwenye mambo ya siasa na kujikuta wakiingia kwenye mitego ambayo sometimes ni mauti kwa waume zao ama wao wenyewe.

Sasa kama mwanasiasa mpinzani anaweza kuingilia familia...Tusije kushangaa ugomvi wa kisiasa ukahamishiwa na kuendelezwa ndani ya familia na uadui kuongezeka...Kwa mfano kitendo cha Deus Mallya kufagiliwa na mke/mpenzi huyu ama ndugu huyu na kupingwa na mke/mpenzi ama ndugu yule...Tatizo lilitokea hapo mtu anazikwa tu na mambo yanaendelea kuona kuwa ni nani atakayeibuka baada ya ndugu huyo either kufa kimwili ama kisiasa ama vyote vyote yani kimwili na kisiasa.

Ni bora kisiasa kwani inawezekana kuwa ulikuwepo upande mbaya wa siasa lakini nia yako ni nzuri..Kifo cha kimwili legacy yako sasa ndiyo hiyo...Huyo mkuu wa wilaya ndiyo hivyo tena.....Tunakoelekea huko hatahamishiwa wilaya nyingine tena..Bali kisiasa ndio hivyo tena.

Wewe umeandika pumba. Ndo ninyi mnakumbatia makosa kwa kuutukuza mfumo dume. Huyo mkuu wa wilaya angemkuta,mkewe na mwanamme mwingine angelimsamehe?

Namuunga huyo mama mkono.
 
Back
Top Bottom