robinson crusoe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2020
- 740
- 1,214
Wakuu wa Wilaya hujinasibu kumwakilisha rais lakini baadhi ya watu hawa ni balaa. Nimesimuliwa anayoyafanya mkuu wa wilaya ya Ukerewe, yanasikitisha. Tangu Mkuu huyu wa Wilaya amepelekwa wilayani, Migogoro haiishi. Mgogogro na kanisa katoliki juu ya ardhi, migogoro na wavuvi na matumizi ya nguvu kukusanya pesa na polisi wakati maafisa watendaji wa wilaya wapo. Kukusanya pesa za ujenzi wa madarasa na kuwaahidi Wananchi kuwaletea mabati baadaye kutokomea bila majibu, n.k.
Jipya sasa ni matumizi ya jeshi la polisi ktk kukusanya michango ya ujenzi wa madarasa unaoendelea. Mkuu huyu wa Wilaya Bw. Cornel Magembe amekuwa tena ni mtu wa vitisho na kukusanya pesa za wananchi bila risiti bila kuulizwa. Kinachoendelea ni ushirikiano kati ya mkuu huyu na polisi kuhakikisha watu wanapata taabu na kutoa pesa bila maswali. Wanaouliza maswali juu ya matumizi ya pesa zao, wanakusanywa na kupelekwa polisi kwa kisingizio cha kupinga ujenzi. Huko hawatoki lazima walipe, tena zaidi ya kilichopangwa.
Mkuu huyu hafai. Urafi wa pesa umemzidi. Ujenzi wa mashule ni kujitolea. Kujitolea siyo kazi ya kusimamiwa na polisi na mkuu wa wilaya. Huu ni wizi! Malipo yasiyo na hesabu.
Jipya sasa ni matumizi ya jeshi la polisi ktk kukusanya michango ya ujenzi wa madarasa unaoendelea. Mkuu huyu wa Wilaya Bw. Cornel Magembe amekuwa tena ni mtu wa vitisho na kukusanya pesa za wananchi bila risiti bila kuulizwa. Kinachoendelea ni ushirikiano kati ya mkuu huyu na polisi kuhakikisha watu wanapata taabu na kutoa pesa bila maswali. Wanaouliza maswali juu ya matumizi ya pesa zao, wanakusanywa na kupelekwa polisi kwa kisingizio cha kupinga ujenzi. Huko hawatoki lazima walipe, tena zaidi ya kilichopangwa.
Mkuu huyu hafai. Urafi wa pesa umemzidi. Ujenzi wa mashule ni kujitolea. Kujitolea siyo kazi ya kusimamiwa na polisi na mkuu wa wilaya. Huu ni wizi! Malipo yasiyo na hesabu.