Mkuu wa Wilaya Serengeti aliyeteuliwa kimakosa aaibishwa kwa kutolewa nje ya Ukumbi Ikulu

sohwa

JF-Expert Member
Dec 28, 2015
1,039
772
UTEUZI: Leo, Nurdin Babu ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Serengeti kuchukua nafasi ya Emile Ntakamulega ambaye alitajwa kimakosa.

==============

Nlikuwa natizama hapa Azam two (Kama sijakosea) ghafla mkuu mmoja wa wilaya Mteule akaambiwa atoke nje/atupishe kwani aliteuliwa kimakosa bila hata ya kuambiwa neno kama samahani au ishara yoyote ya kuonesha kuwa wamemletea usumbufu,lakini kuambiwa'tupishe'kwani uliteuliwa kimakosa!!!

Mimi naona ingefaa Sana kama angefuatwa alipoketi aambiwe bila hata ya watu wengi kunotice kuwa hakustahili kuwapo pale(kwamba kuteuliwa kimakosa na aombwe radhi kwa usumbufu), Lakini Haikuwa Hivyo, badala yake Katolewa nje wazi wazi.

Mnalionaje hili Wakuu?

Umepata muda ukajiuliza kwa yule Mkuu wa Wilaya aliyedhalilishwa ukumbini nini kinaweza kuwa chanzo? Nadhan hujapata nafasi hiyo pengine kwa kuwa hakuwa akifahamika sana hapo nyuma au kwa vile halijaonekana kama ni jambo kubwa. Lakini umewahi kufikiria ingekuwa wewe ungejisikiaje? Sijui kama umefikiria hivyo. Kiuhalisia ukiwa kama mtu mzima mwenye kujielewa jaribu kukaa nafasi yake.

Nimepata muda nikawaza hivi ni kweli jina lake lilikosewa kwa siku zote hizo? ni nani anayeteua hao wakuu wa wilaya? Inawezekana kuwa aliteua mtu asiyewafaham wahusika? Au jina lake lilichomekwa?

Hujajiuliza hayo maswali,sisi machizi huwa tunajiuliza maswali ambayo ninyi wenye akili timamu hamtaki kujiuliza maana mnayaona hayana maana ila kwa sisi machizi tunajiuliza.

Yale majina yametangazwa redio,TV na magazetini. ina maana wala hakuna mtu aliyekuwa makini kufatilia na kuona kuwa kuna jina limekosewa yaani halikupaswa kuwepo? Hamna? Kuna shida.

Lakini kwanini hakuambiwa mapema au ni nani aliyekuja kugundua kuwa huyu bwana jina lake halikupaswa kuwepo? Aligunduaje? Lakini huyu mhusika ambaye jina lake liliwekwa pale kimakosa ni nani na ilikuaje akawa pale? Je mmemwangalia alikuwa nani hapo kabla?Au kambi ya nani katika zile kambi kuu? Au kuna jambo gani baya alinena au tenda kabla ya kuapishwa na ikasababishwa atenguliwe kwa kudhalilishwa vile?

Lakini kama hakukuwa na suala la kumkomoa unadhani ni nini kilisababisha aoendolewe kwa style ile? Kwanini mhusika hakumtafuta au kuita kwenye kipaza sauti kuwa Mr X tafadhari onana na Y ana ujumbe wako kisha huko akampa taarifa hiyo ili aondoke kwa staha? Nimewaza sana nikawazua nikasema haya mambo ni madogo yanapomtokea mwingine usiombe yakukute wewe,usiombe kabisa. Ila inawezekana kuna mambo mengi tusiyoyajua juu ya sakata hili. Mimi na mwombea awe na roho ya uvumilivu maana ni wazi atakuwa ameathirika kisaikolojia. Lakini kwa nchi zetu za africa. WHO CARES?AAAARHG acha tu nikaokote makopo huko majalalani huenda nikapata tena mambo muhimu yakiwa yametupwa pamoja na taka nyingine.
 
Nlikuwa natizama hapa azam two,ghafla mkuu mmoja WA wilaya Mteule akaambiwa atoke nje/atupishe Kwani aliteuliwa kimakosa,,bila hata ya kuambiwa neno Kama samahani au ishara yoyote ya kuonesha kuwa wamemletea usumbufu,lakini kuambiwa'tupishe'kwani uliteuliwA kimakosa!!!
Mimi naona ingefaa Sana kama angefuatwa alipoketi aambiwe bila hata ya watu wengi kunotice kuwa hakustahili kuwapo pale(kwamba kuteuliwa kimakosa na aombwe radhi kwa usumbufu),, Lakini Haikuwa Hivyo, badala yake Katolewa nje wazi wazi,, mnalionaje hili Wakuu???
Serikali ya mizukaaaa


#sugu.rais.wa. mbeya
 
Ndiyo maana mnaitwa malofa!! Ni nani huyo ameteuliwa kimakosa!! Serikali ya kukurupuka hii!!!

"Nlikuwa natizama hapa azam two,(Kama cjakosea) ghafla mkuu mmoja WA wilaya Mteule akaambiwa atoke nje/atupishe Kwani aliteuliwa kimakosa,,bila hata ya kuambiwa neno Kama samahani au ishara yoyote ya kuonesha kuwa wamemletea usumbufu,lakini kuambiwa'tupishe'kwani uliteuliwA kimakosa!!!
Mimi naona ingefaa Sana kama angefuatwa alipoketi aambiwe bila hata ya watu wengi kunotice kuwa hakustahili kuwapo pale(kwamba kuteuliwa kimakosa na aombwe radhi kwa usumbufu),, Lakini Haikuwa Hivyo, badala yake Katolewa nje wazi wazi,, mnalionaje hili Wakuu???"

Jee hiyo hapo juu ni uungwana?
 
Sanaa katika ubora wake, kama alimteua kimakosa kwanini hasingetangaza siku hile hile kubatilisha taarifa au msigwa anakazi gani.....?? Sema labda alikua na kisasi nae akaona aje amuaibishe mbele ya kadamnasi tu maana jamaa nae mtu wa visasi hatari.
 
32 Reactions
Reply
Back
Top Bottom