Mkuu wa Wilaya Salum Ali Hapi na ardhi ya Sumaye

CHUAKACHARA

JF-Expert Member
Jun 3, 2011
12,358
6,422
Inasikitisha kuwa DC wa Kinondoni anawapa matumaini wavamizi wa ardhi ya Sumaye kuwa Lukuvi ataumaliza mgogoro huo na wanashangilia kwa matumaini.

DC mnahubiri kutovunja sheria wakati huo huo mnawapa wavamizi waliovunja sheria za nchi kuwa "Hapa kazi tu" itawapa makazi hapo.

Si sahihi! Simtetei Sumaye, concern yangu ni uvunjaji wa sheria kuwafurahisha wavunja sheria kwa manufaa ya kisiasa.

Hata kama Sumaye amehamia upinzani, nadhani haki zake hazibadiliki kwa vile kaende upinzani.

Tunayasema haya kwa vile trend hii itakwenda kwa wote walio upinzania na broadly kugusa haki za msingi za binadamu.
 
Hii hali ikiachwa iendelee itapelekea uvunjifu wa amani siku za usoni.Ni viongozi wengi ambao wanakosa fursa chama tawala wanapenda kuhamia upinzani,hiyo ni hali ya kawaida katika kusaka fursa,sasa kama wakihamia upinzani wana fanyiwa figisu figisu na utawala,hapo haki za msingi zinakiukwa na wasimamia haki.
Hali hii itaibadili sura na sifa nzuri ya Tanzania tuliyoaminishwa kwa miongo kadha
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kama ardhi haiendelezwi na kuna watu wanauhitaji wa hiyo. Hakuna kumwangalia nyani usoni ni kuua tu.
 
Mmmmh!! Ardhi ya Sumaye. Si ndo huyu aliwahi kuwatamkia w/biashara kule Moshi kuwa ukitaka mambo yakunyokee, hamia ccm. Maana yake ukiwa nje ya ccm ni kuisoma namba mazima. Sijui anakumbuka hili? Kama anakumbuka bora arudi ccm kwani ccm ni ile ile na makali ni yale yale.
 
Mmmmh!! Ardhi ya Sumaye. Si ndo huyu aliwahi kuwatamkia w/biashara kule Moshi kuwa ukitaka mambo yakunyokee, hamia ccm. Maana yake
Yes, ninachokizungumzia hapa ni haki , kuwahimiza watu wavunje sheria. Hawa walivamia ardhi yake (Sumaye has a granted right of occupancy), trend hii kesho itakukumba wewe au anyone you are related to!
 
Sumaye alishapora mashamba ya Kibaigwa na Mvomero akiwa waziri mkuu.Tulipiga kelele sana lakini serikali ya Mkapa iliziba masikio.
 
Inasikitisha kuwa DC wa Kinondoni anawapa matumaini wavamizi wa ardhi ya Sumaye kuwa Lukuvi ataumaliza mgogoro huo na wanashangilia kwa matumaini. DC mnahubiri kutovunja sheria wakati huo huo mnawapa wavamizi waliovunja sheria za nchi kuwa "Hapa kazi tu" itawapa makazi hapo. Si sahihi! Simtetei Sumaye, concern yangu ni uvunjaji wa sheria kuwafurahisha wavunja sheria kwa manufaa ya kisiasa. Hata kama Sumaye amehamia upinzani, nadhani haki zake hazibadiliki kwa vile kaende upinzani.Tunayasema haya kwa vile trend hii itakwenda kwa wote walio upinzania na broadly kugusa haki za msingi za binadamu.


Sasa wewe ardhi ya Sumaye inakuhusu nini? Umeshasema ardhi ya Sumaye ni kwa nini usimwachie mwenyewe aipiganie, kwa sababu ni mali yake binafsi yeye ndiyo anajua alivyoipata na siyo wewe! Au ndiyo kila kitu Siasa? Kesho Sumaye akigeuka na kuamua kuwa transexual na wewe utajigeuza pia?

Jueni kutenganisgha mipaka ya Siasa na maisha binafsi, kama ardhi ya kwake Sumaye binafsi na siyo mali ya Chama cha chadema kwa nini ikuwashe wewe? isitoshe kama akiuza au akibakia nayo au akilipwa fidia wewe haupati hata sumni na wala hatachangia hiyo fedha na chadema na wala hatakwambia kama ameuza au amelipwa fidia sasa yote haya ya nini?
 
Sasa wewe ardhi ya Sumaye inakuhusu nini? Umeshasema ardhi ya Sumaye ni kwa nini usimwachuie mwenyewe aipiganie, kwa sababu ni mali yake binafsi yeye ndiyo anajua alivyoipata na siyo wewe! Au ndiyo kila kitu Siasa? Kesho Sumaye akigeuka na kuamua kuwa transexual na wewe utajigeuza pia?

Jueni kutenganisgha mipaka ya Siasa na maisha binafsi, kama ardhi ya kwake Sumaye binafsi na siyo mali ya Chama cha chadema kwa nini ikuwashe wewe? isitoshe kama akiuza au akibakia nayo au akilipwa fidia wewe haupati hata sumni na wala hatachangia hiyo fedha na chadema na wala hatakwambia kama ameuza au amelipwa fidia sasa yote haya ya nini?
Nimesema watu nyinyi (Lizaboni&Co Ltd) sijibizani nao).
 
Utawala wa sheria lazima uzingatiwe. Leo wamevamia shamba la Sumaye kwa kuwa yupo CDM. Kesho wakivamia la kigogo wa CCM itabidi waachwe tu.

The rule of LAW ikipuuzwa, kuna hatari huko mbele. I am pro JPM, but i will assess each situation on its merit.
 
Utawala wa sheria lazima uzingatiwe. Leo wamevamia shamba la Sumaye kwa kuwa yupo CDM. Kesho wakivamia la kigogo wa CCM itabidi waachwe tu.

The rule of LAW ikipuuzwa, kuna hatari huko mbele. I am pro JPM, but i will assess each situation on its merit.
Asante maana wengi wakiwa CCM au pro JPM huwa hawaoni umuhimu wa kutenda haki.
 
Nimesema watu nyinyi (Lizaboni&Co Ltd) sijibizani nao).


Oh, kumbe unachuki binafsi na watu usiowafahamu? Pole sana mimi mbona hata sikufahamu na najibu hoja kama ilivyoandikwa na wala siyo kwa sababu binadamu xyz ameandika kwa maana huyo binadamu simfahamu wala simjui, ningejibu kwa yoyote yule ambaye angeandika upuuzi kama huwo!

Basi una maisha magumu sana kama unachukulia mambo ya JF personal na kuanza kununia watu usiowafahamu wala wasiokufahamu na isitoshe wanatumia majina bandia, basi kazi unayo, Duh!
 
Msituletee machafuko kwa kisingizio cha hapa kazi tu tunataka sheria ifuate mkondo vinginevyo itafika siku watu watavamia nyumba za marais wastaafu kwa kisingizio wanazo nyumba zaidi ya moja wananchi hawana makazi hizi siasa nyepesi za kutaka kuwafurahisha watu zitatuletea shida
 
Hata mimi nilimshangaa sana DC maana alisikiliza tu upande mmoja akaja na yale maazimio yake.

Hakuna anayejua kama aliwahi kuongea na Sumaye, akasikia naye ana lipi la kusema kuhusiana na umiliki wa hiyo ardhi.

Ni hatari sana kwa kiongozi anayepaswa kutenda haki kwa wote anapoegemea upande mmoja wakati wa kutoa maamuzi.
 
Hata mimi nilimshangaa sana DC maana alisikiliza tu upande mmoja akaja na yale maazimio yake.

Hakuna anayejua kama aliwahi kuongea na Sumaye, akasikia naye ana lipi la kusema kuhusiana na umiliki wa hiyo ardhi.

Ni hatari sana kwa kiongozi anayepaswa kutenda haki kwa wote anapoegemea upande mmoja wakati wa kutoa maamuzi.
it is apity kuwa anahimiza uvunjaji wa sheria!
 
Swala la ardhi likipelekwa kisiasa litaleta shida
Sina chama but kwa hilo na mengine yanayofanana na hilo sheria ifate mkondo wake.
Ukiruhusu hilo, unaweza kusikia watu wamevamia eneo lako kinyume na sheria
 
Inasikitisha kuwa DC wa Kinondoni anawapa matumaini wavamizi wa ardhi ya Sumaye kuwa Lukuvi ataumaliza mgogoro huo na wanashangilia kwa matumaini.

DC mnahubiri kutovunja sheria wakati huo huo mnawapa wavamizi waliovunja sheria za nchi kuwa "Hapa kazi tu" itawapa makazi hapo.

Si sahihi! Simtetei Sumaye, concern yangu ni uvunjaji wa sheria kuwafurahisha wavunja sheria kwa manufaa ya kisiasa.

Hata kama Sumaye amehamia upinzani, nadhani haki zake hazibadiliki kwa vile kaende upinzani.

Tunayasema haya kwa vile trend hii itakwenda kwa wote walio upinzania na broadly kugusa haki za msingi za binadamu.
Ole wao wanaotuzia tusifanye kazi! hawataona ufalme wa mbinguni...na ardhi ya TZ itakuwa jahanamu kwao....
 
Hii hali ikiachwa iendelee itapelekea uvunjifu wa amani siku za usoni.Ni viongozi wengi ambao wanakosa fursa chama tawala wanapenda kuhamia upinzani,hiyo ni hali ya kawaida katika kusaka fursa,sasa kama wakihamia upinzani wana fanyiwa figisu figisu na utawala,hapo haki za msingi zinakiukwa na wasimamia haki.
Hali hii itaibadili sura na sifa nzuri ya Tanzania tuliyoaminishwa kwa miongo kadha
Dah.. Sasa hii ardhi ni ya Chadema??? CCM?? au Sumaye?? Mbona unajichanganya dogo :)
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom