beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Daniel Chongolo ameagiza polisi kata ya Kijitonyama kuwakamata wanaume wanaonunua machangudoa.
Chongolo ametoa agizo hilo leo Jumanne Novemba 6, 2018 kwa mkuu wa kituo cha polisi Kijitonyama, Said Lujuo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya Msingi Kisiwani.
Kauli hiyo ya Chongolo ameitoa baada ya mkazi mmoja wa mtaa wa Nzasa kulalamikia suala la biashara ya ukahaba kukithiri kwenye mtaa anaoishi.
“Ikifika jioni tunashindwa kutoka nje na watoto wetu maana mambo yanayofanyika ni aibu, machangudoa wamejaa na hata tukipiga simu polisi wanawakamata na kuwaachia ndani ya muda mfupi,” amesema mkazi huyo.
Akizungumzia hilo, Lujuo amesema polisi huwa wanawakamata machangudoa lakini faini wanazotozwa ni ndogo na wanazilipa kwa haraka na kuachiwa.
“Pia hawa watu wana vigogo wao ndio wanawawezesha na kuwalipia faini ili waendelee kuwepo,” amesema.
Kufuatia hilo, Chongolo ameagiza wakamatwe na wanaume na wawekwe hadharani.
“Wakikamatwa wanaume na kuwekwa hadharani itakuwa funzo kwa wengine na makahaba hao watakosa wateja.”
“Polisi nendeni kwenye huo mtaa na mie nitakuja kuangalia hali ilivyo,” amesema Chongolo.
Chanzo; Mwananchi
Chongolo ametoa agizo hilo leo Jumanne Novemba 6, 2018 kwa mkuu wa kituo cha polisi Kijitonyama, Said Lujuo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya Msingi Kisiwani.
Kauli hiyo ya Chongolo ameitoa baada ya mkazi mmoja wa mtaa wa Nzasa kulalamikia suala la biashara ya ukahaba kukithiri kwenye mtaa anaoishi.
“Ikifika jioni tunashindwa kutoka nje na watoto wetu maana mambo yanayofanyika ni aibu, machangudoa wamejaa na hata tukipiga simu polisi wanawakamata na kuwaachia ndani ya muda mfupi,” amesema mkazi huyo.
Akizungumzia hilo, Lujuo amesema polisi huwa wanawakamata machangudoa lakini faini wanazotozwa ni ndogo na wanazilipa kwa haraka na kuachiwa.
“Pia hawa watu wana vigogo wao ndio wanawawezesha na kuwalipia faini ili waendelee kuwepo,” amesema.
Kufuatia hilo, Chongolo ameagiza wakamatwe na wanaume na wawekwe hadharani.
“Wakikamatwa wanaume na kuwekwa hadharani itakuwa funzo kwa wengine na makahaba hao watakosa wateja.”
“Polisi nendeni kwenye huo mtaa na mie nitakuja kuangalia hali ilivyo,” amesema Chongolo.
Chanzo; Mwananchi