Mkuu Wa Wilaya Avutana Mashati na Walinzi Wa Night Club

Daraja Makofia

JF-Expert Member
Mar 30, 2015
695
901
Habari za Jumapili Wanajamvi.

Jana usiku jijini Dodoma kuliandaliwa onyesho la msanii wa muziki wa Bongo Fleva Nay wa Mitego kwenye Klabu ya Usiku maarufu Royal Village Au Club Seven.

Kama raia wa kawaida, niliamua na mimi nihudhurie ndipo nikajongea maeneo hayo muda wa saa saba kasoro usiku.

Kiingilio cha onyesho hilo kilikuwa ni Shilingi Elfu Kumi (10,000/=) tu. Na tickets za kuingia ndani zilikuwa zikiuzwa kwenye gari(Noah) la Royal Village pale geti la kuingia Club Seven na Ngalawa Bar.

Wakati naulizia taratibu za ununuzi wa tiketi ya kuingia kwenye onyesho hilo, ukazuka mzozo pale getini kati ya walinzi na watu ambao sikuwatambua kwa muda ule. Niliposogea karibu, nikapokelewa na tukio la dada mmoja akipigwa kofi la haja na mlinzi(bouncer) aliyejazia misuli. Kwa muonekano huyo dada alikuwa amelewa na alikuwa akizozana na walinzi huku akitaka kuingia ndani. Baadae nilikuja kufahamishwa kuwa dada na vijana wengine kama wanne hivi walikuwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mh. Patrobas Katambi.

Hali ilivyokuwa inaonekana, chanzo cha mgogoro huo ni kuwa msafara wa Mkuu wa Wilaya ulitaka kuingia ukumbini hapo bila ya kulipia kiingilio. Na pia msafara huo ulijitambulisha kibabe pale getini.

Ila tendo la yule mlinzi (bouncer) kumtia banzi yule dada, halikumfurahisha Mheshimiwa. Ndipo nae akaanza kuhamaki na kutaka kushikana na yule bouncer huku watu wakiwavuta wasipigane.

Ilifikia wakati Mheshimiwa alivua koti lake la suti na kubakia na t-shirt ya rangi ya ugoro yenye nembo kubwa ya taifa ya rangi kwa mbele. Hapa ilikuwa inamaanisha Mheshimiwa alikuwa anajiweka tayari kwa ajili ya kupambana na mlinzi aliyempiga mtu wake.

Baadae alikuja kiongozi wa eneo lile na akaamua kumuondoa yule mlinzi. Kisha akaenda kuongea na Mheshimiwa kwa muda mrefu. Nadhani alikuwa akiomba radhi kwa yaliyotokea.

Baada ya hayo yote, nikaona ni bora nisinunue tiketi ya onyesho hilo ili kukwepa hasara pale Mheshimiwa atakapochukua hatua ya kulifungia onyesho hilo kwa sababu za kiusalama. Ndio! Yeye kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, anaweza kutoa amri ya kusitishwa kwa onyesho lile kisa tu dada aliyekuja nae kapigwa na bouncer.

Pia niliamua kuondoka kabisa eneo hilo na kuhamia eneo lingine. Hivyo sikujua nyuma huko walimalizana vipi.

Ushauri wangu kwa Wanasiasa Vijana
1. Mnapoenda kwenye maeneo ya starehe epukeni kuwa na kiburi cha cheo chako. Na uangalie wale ulioambatana nao wasije kukutia doa.
Fuateni mifano ya kina Joseph Haule (MB) na Joseph Mbilinyi (MB) wawapo maeneo haya, hutaweza fahamu kirahisi kama wapo. Hawaambatani na msululu wa watu wengi.

2. Ndg. Patrobas Katambi ilikuwa atumie akili ndogo tu ya kumuita au hata kumpigia simu Meneja wa eneo lile kuwa yeye na watu wake kadhaa wanataka kuhudhuria. Sidhani kama angekataliwa.

3. Epukeni ulevi wa madaraka kwa kutisha watu kwa kauli za "UNANIJUA MIMI NI NANI". Sio kila raia atakujua kuwa wewe ni Mkuu wa Wilaya.

NIMESHUKURU KUONA LILE BANZI LA MLINZI HALIJATUA USONI MWA MHESHIMIWA!!!

Naomba kuwasilisha.
 
Hilo kofi angechapwa huyo karai anayetaka kuingia ukumbuni bure

Sent using Jamii Forums mobile app
Busara ilitumika kumficha bouncer kwa kupitia mlango wa nyuma, vinginevyo athari za banzi zingemkuta Karai. Na muda huu bouncer angepewa kesi aina mpya na kesho mahakamani. Dhamana yake ingefungwa.

Kwa kifupi, bouncer angesota jela.
 
Huyo Likatambi alitakiwa azabuliwe kelbu moja hadi aitike "abee " na masikio yazibuke. Alizaliwa njiti huyo.
Mliomshika bouncer mtuombe radhi...kabisa huyu katambi na machali walimdhurumu mwanafunzi mwenzao wakiwa wanasoma SAUT kitivo cha sheria pesa yake baada ya kuwakopesha bila dhamana na riba ..Geofrey Minani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za Jumapili Wanajamvi.

Jana usiku jijini Dodoma kuliandaliwa onyesho la msanii wa muziki wa Bongo Fleva Nay wa Mitego kwenye Klabu ya Usiku maarufu Royal Village Au Club Seven.

Kama raia wa kawaida, niliamua na mimi nihudhurie ndipo nikajongea maeneo hayo muda wa saa saba kasoro usiku.

Kiingilio cha onyesho hilo kilikuwa ni Shilingi Elfu Kumi (10,000/=) tu. Na tickets za kuingia ndani zilikuwa zikiuzwa kwenye gari(Noah) la Royal Village pale geti la kuingia Club Seven na Ngalawa Bar.

Wakati naulizia taratibu za ununuzi wa tiketi ya kuingia kwenye onyesho hilo, ukazuka mzozo pale getini kati ya walinzi na watu ambao sikuwatambua kwa muda ule. Niliposogea karibu, nikapokelewa na tukio la dada mmoja akipigwa kofi la haja na mlinzi(bouncer) aliyejazia misuli. Kwa muonekano huyo dada alikuwa amelewa na alikuwa akizozana na walinzi huku akitaka kuingia ndani. Baadae nilikuja kufahamishwa kuwa dada na vijana wengine kama wanne hivi walikuwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mh. Patrobas Katambi.

Hali ilivyokuwa inaonekana, chanzo cha mgogoro huo ni kuwa msafara wa Mkuu wa Wilaya ulitaka kuingia ukumbini hapo bila ya kulipia kiingilio. Na pia msafara huo ulijitambulisha kibabe pale getini.

Ila tendo la yule mlinzi (bouncer) kumtia banzi yule dada, halikumfurahisha Mheshimiwa. Ndipo nae akaanza kuhamaki na kutaka kushikana na yule bouncer huku watu wakiwavuta wasipigane.

Ilifikia wakati Mheshimiwa alivua koti lake la suti na kubakia na t-shirt ya rangi ya ugoro yenye nembo kubwa ya taifa ya rangi kwa mbele. Hapa ilikuwa inamaanisha Mheshimiwa alikuwa anajiweka tayari kwa ajili ya kupambana na mlinzi aliyempiga mtu wake.

Baadae alikuja kiongozi wa eneo lile na akaamua kumuondoa yule mlinzi. Kisha akaenda kuongea na Mheshimiwa kwa muda mrefu. Nadhani alikuwa akiomba radhi kwa yaliyotokea.

Baada ya hayo yote, nikaona ni bora nisinunue tiketi ya onyesho hilo ili kukwepa hasara pale Mheshimiwa atakapochukua hatua ya kulifungia onyesho hilo kwa sababu za kiusalama. Ndio! Yeye kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, anaweza kutoa amri ya kusitishwa kwa onyesho lile kisa tu dada aliyekuja nae kapigwa na bouncer.

Pia niliamua kuondoka kabisa eneo hilo na kuhamia eneo lingine. Hivyo sikujua nyuma huko walimalizana vipi.

Ushauri wangu kwa Wanasiasa Vijana
1. Mnapoenda kwenye maeneo ya starehe epukeni kuwa na kiburi cha cheo chako. Na uangalie wale ulioambatana nao wasije kukutia doa.
Fuateni mifano ya kina Joseph Haule (MB) na Joseph Mbilinyi (MB) wawapo maeneo haya, hutaweza fahamu kirahisi kama wapo. Hawaambatani na msululu wa watu wengi.

2. Ndg. Patrobas Katambi ilikuwa atumie akili ndogo tu ya kumuita au hata kumpigia simu Meneja wa eneo lile kuwa yeye na watu wake kadhaa wanataka kuhudhuria. Sidhani kama angekataliwa.

3. Epukeni ulevi wa madaraka kwa kutisha watu kwa kauli za "UNANIJUA MIMI NI NANI". Sio kila raia atakujua kuwa wewe ni Mkuu wa Wilaya.

NIMESHUKURU KUONA LILE BANZI LA MLINZI HALIJATUA USONI MWA MHESHIMIWA!!!

Naomba kuwasilisha.
Katamhi huyu huyu aliyekuwa chadema?? daah, kweli mlaika akiishi na mashetani lazima nae awe shetani tu.
 
Back
Top Bottom