KunjyGroup
JF-Expert Member
- Dec 7, 2009
- 352
- 26
i
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema, naye amekiri kuwa kuwakamata mafisadi ni kazi ngumu.
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema, naye amekiri kuwa kuwakamata mafisadi ni kazi ngumu.
Na Boniface Meena
UCHUNGUZI wa Sh42.6 bilioni zilizochotwa kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) bado unaonekana kuwa mgumu baada ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema kurejea kauli zilizowahi kutolewa kuwa inawawia vigumu kuwatia hatiani watuhumiwa. Fedha hizo ni sehemu ya Sh133 bilioni zilizoibwa kwenye akaunti hiyo ya BoT kati ya mwaka 2005/06.
Watuhumiwa waliohusika kwenye wizi huo wa Sh42 bilioni hawakuweza kufikishwa mahakamani, wakati wengine zaidi ya 20 wamefikishwa mahakamani na kesi zao zinaendelea.
Hatuwezi mulaum Mwema sabab anaambiwa wakukamatwa. 'EPA guys, don't! DECI, kamata leo hii. Kagoda, don't dare! ....' Tz yetu hiyo. Je tutafika?