Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda na Mjasiriamali Carol Ndosi, wana bifu la kimya kimya?

Mdg wangu na x Makongo mwenzangu Carol pole sana. Nikupe ushauri kiungwana kabisa. Unapenda siasa na hasa uanaharakati ambao si rafiki sana na serikali hasa watawala.

Hufanyi vibaya ni haki yako ya msingi na pengine ndio wito uliopewa na Mungu kusemea wengine. Lakini kwa nchi zetu hizi maskini na aina ya watawala wetu huwezi kufanya biashara zako kwa amani hata kama ni halali kwa kiwango kipi huku maneno, maandiko yako si rafiki kabisa kwa watawala.

Inawezekana hujamtukana Makonda wala kufanya ubaya wowote lakini umejijengea sura isiyo rafiki na watawala akiwemo huyo Makonda. Usidanganywe dunia hii sijui haki, usawa n.k hasa huku Africa kuna gharama lazima ulipe pale unapochagua namna ya kuishi na watawala/wanasiasa.

Wewe kujiondoa ACT na kutojiingiza kwenye siasa si "toba" kwao maana hata akina Maria Sarungi wanasema hawana vyama lakini mkondo wa maoni yao upo wazi sana na pengine wapo tayari kulipa gharama yake na ndivyo inavyopaswa ukiamua kusimamia jambo.

Wafanyabiashara wakubwa na walipa kodi wazito waki finance upande wa pili wanafinywa na kutiwa "adabu" kidogo itakuwa wewe!!! Kwani hujui kwanini CMG wanapata kibali kirahisi? Kwani umezaliwa juzi Carol hadi ushangae? Huoni wanavyounga mkono juhudi?

Dunia haiko hivyo utachanganyikiwa mdg wangu! Jifunze namna ya kuishi na watawala ili kulinda mkate wako au ingia kwenye harakati upambanie wananchi ukiwa tayari pia kwa matokeo yake na utapata heshima kubwa tu vizazi na vizazi!

Usitake kula huku na huku, harakati kidogo na biashara kidogo kwasababu tu ni haki yako, si Africa mdg wangu utakosa kote! Unafikiri Mengi amepenya vipi tawala zote? Hukujifunza hata manguli kama Rostam kuacha siasa enzi za JK na kuacha kabisa hata kuchangia/kutoa comment kuhusu siasa zetu ili alinde maslahi yake?

Asikudanganye binadamu yoyote jifunze kuwa mroma ukiwa roma full stop kama unataka usiumie kama ilivyo sasa. Kaa chini ujitafakari unataka uelekeo upi wa maisha yako then move on. Africa yenye uhuru wa kiwango hicho si ya leo wala kesho, jipambanue na pambana kwa kukubaliana na matokeo pia.

Hii ndio Afrika na wala si Tanzania tu au awamu hii tu au CCM tu! Hata kama wangeshinda Chadema lazima ujue namna ya kuishi nao kama unapenda kuendelea na biashara zako smoothly.

Ushauri wako, pamoja na kwamba unaweza kumsaidia yeye binafsi (japo kuna uwezekano mkubwa tu sio mawazo mapya kwake au umemfunza jambo asilojua) hauna msaada wowote kwa mtu yeyote pro progress. Huwezi kukubali kuwepo na upindishwaji wa haki kwenye hili au yanayofanana na hili tangu vizazi halafu ushauri wako uwe kuchagua moja kati ya haki yake ya maoni au biashara. Progress itatoka wapi akifuata njia ya Rostam na Mengi?

Tunakubali kuwa jamii isiyoprogress na hatuna jinsi bali tuwaachie watoto wetu mifumo iliyo zao la mapungufu ya wazazi wetu?

My guess is she knows what she's doing japo kuna wanaomuona naive humu. Habari za biashara zilizofail baada ya wamiliki wao kuonyesha misimamo fulani si mpya. Kuna tabia ya viongozi kudismiss malalamiko ya watu kwa kusema "alete ushahidi taratibu za ufanyaji kazi wa serikali zinajulikana". Kama Rostam na wenzake hawakulalamika basi hayatokei.

If for no other reason let this serve to crystallise these occurrences
 
Ushauri mzuri huu aufanyie kazi. Huwezi shindana na dola uka win lazima uumie
Mdg wangu na x Makongo mwenzangu Carol pole sana. Nikupe ushauri kiungwana kabisa. Unapenda siasa na hasa uanaharakati ambao si rafiki sana na serikali hasa watawala.

Hufanyi vibaya ni haki yako ya msingi na pengine ndio wito uliopewa na Mungu kusemea wengine. Lakini kwa nchi zetu hizi maskini na aina ya watawala wetu huwezi kufanya biashara zako kwa amani hata kama ni halali kwa kiwango kipi huku maneno, maandiko yako si rafiki kabisa kwa watawala.

Inawezekana hujamtukana Makonda wala kufanya ubaya wowote lakini umejijengea sura isiyo rafiki na watawala akiwemo huyo Makonda. Usidanganywe dunia hii sijui haki, usawa n.k hasa huku Africa kuna gharama lazima ulipe pale unapochagua namna ya kuishi na watawala/wanasiasa.

Wewe kujiondoa ACT na kutojiingiza kwenye siasa si "toba" kwao maana hata akina Maria Sarungi wanasema hawana vyama lakini mkondo wa maoni yao upo wazi sana na pengine wapo tayari kulipa gharama yake na ndivyo inavyopaswa ukiamua kusimamia jambo.

Wafanyabiashara wakubwa na walipa kodi wazito waki finance upande wa pili wanafinywa na kutiwa "adabu" kidogo itakuwa wewe!!! Kwani hujui kwanini CMG wanapata kibali kirahisi? Kwani umezaliwa juzi Carol hadi ushangae? Huoni wanavyounga mkono juhudi?

Dunia haiko hivyo utachanganyikiwa mdg wangu! Jifunze namna ya kuishi na watawala ili kulinda mkate wako au ingia kwenye harakati upambanie wananchi ukiwa tayari pia kwa matokeo yake na utapata heshima kubwa tu vizazi na vizazi!

Usitake kula huku na huku, harakati kidogo na biashara kidogo kwasababu tu ni haki yako, si Africa mdg wangu utakosa kote! Unafikiri Mengi amepenya vipi tawala zote? Hukujifunza hata manguli kama Rostam kuacha siasa enzi za JK na kuacha kabisa hata kuchangia/kutoa comment kuhusu siasa zetu ili alinde maslahi yake?

Asikudanganye binadamu yoyote jifunze kuwa mroma ukiwa roma full stop kama unataka usiumie kama ilivyo sasa. Kaa chini ujitafakari unataka uelekeo upi wa maisha yako then move on. Africa yenye uhuru wa kiwango hicho si ya leo wala kesho, jipambanue na pambana kwa kukubaliana na matokeo pia.

Hii ndio Afrika na wala si Tanzania tu au awamu hii tu au CCM tu! Hata kama wangeshinda Chadema lazima ujue namna ya kuishi nao kama unapenda kuendelea na biashara zako smoothly.
 
Mimi niulize tu, ina maana hakuna kanuni za kisheria zinazotoa mwongozo juu ya haya masuala? Yaani ni utashi na matamko tu ya RC au? Maana hii inaleta kunyenyekeana pasipo na ulazima, kama mtu ametimiza vigezo na masharti basi RC ni nani aseme otherwise?
 
Hivi hii ni account ya twitter ya Mh RC kweli? Alibadili kutoka ile ya jina la mtoto wake?
 
Safi sana kama wanakunyoosha..ulishawahi kuandika barua kuwa nchi haina uhuru mi nikashangaa sana wakati huwa unafanya matamasha yako hadi usiku...huwa mnakurupuka..iko hivi ukiwa mfanyabiashara ni mawili,either ukae kimya au uungane na watawala period..kina fatuma karume walikudanganya..wale ni wanataaluma..umevuruga hadi timu yako ya nyama choma sababu ya kujifanya mwanaharakati..dunia ina kanuni zake mama..waachie kina ruge na kina majjizo waingize hela za kufaidi na familia zao..
Ndiyo maana Afrika ni bara la giza tunahitaji miaka mingine 500 kuwa na akili, yani mtu anashangili mtu kubaniwa kisa ana mawazo tofauti yani anasema kabisa ukiwa mfanya biashara huna haki ya kutoa maoni tofauti na serikali...... Ndo maana mbunge wa Ugermany katoa wazo la afrika kuwa colonized voluntarily
 
Huyo Karo ni wa ajabu Sana. Unaomba a favor from a politician halafu at the same time unapiga majungu? How convenient. Na lazima ajue There is no place in this world a businessman unaweza kusurvive while kwenye mitandao na vijiwe vya supu ya Utumbo unaongelea vibaya politicians. It's either you dance their music mkono uingie kinywani hata kama hupendi or uache biashara uendelee kutukana vizuri labda utashiba hayo maneno
Well said walahi
Ukoo mzima chadrama huyo mdada walahi
 
Ndiyo maana Afrika ni bara la giza tunahitaji miaka mingine 500 kuwa na akili, yani mtu anashangili mtu kubaniwa kisa ana mawazo tofauti yani anasema kabisa ukiwa mfanya biashara huna haki ya kutoa maoni tofauti na serikali...... Ndo maana mbunge wa Ugermany katoa wazo la afrika kuwa colonized voluntarily

Ni wewe na kizazi chako ndio mko hivyo na mtakuwa hivyo milele walahi
Usituingize wafrica kwenye hilo lilaana lenu walahi nakuapia!
 
naona ccm mnaparurana , Makonda aliyekuwa na bifu na kapuku wema unamshangaa vipi kuwa na bifu na Carol , kauli kwamba ni ni mpinga serikali si ya kweli , ulevi wa madaraka ndio chanzo

Carol ni chadrama na ukoo wake wote walahi, walimfuata El, Sinare walahi
 
Jibu la RC wa Dar, Paul Makonda kwa Mjasiriamali na Mdau wa Maendeleo, Carol Ndosi leo kupitia ukurusa wa Twitter baada ya kumuandikia barua linasema mengi.

Inavyoonekana, kuna mgongano wa kimaslahi kati ya Mjasiriamali huyo na Gavana wa Jiji la Biashara asiyekaukiwa headlines, Paul Makonda.

Nini tatizo? Kwa takribani miaka miwili sasa, Carol hafanyi tamasha lake la Nyamachoma kama ilivyozoelekea jijini humo. Na, amewahi kunukuliwa akilalamika kwamba mamlaka zinambania kwa sababu ambazo wengine wenye matamasha wanaruhusiwa kufanya. Double standards?

Sasa, baada ya kimya ama pengine jitihada za kimya kimya, naona Carol ameamua kumuandikia barua ya wazi kwa RC Makonda na kuiweka mitandaoni;

Carol Ndosi alimuandikia barua Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda.

Barua ya Wazi kwako Mheshimiwa Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

Salaam Kaka.

Ni matumaini kuwa ni mzima wa afya na unaendelea kulitumikia taifa. Naomba niwasilishe barua hii, nikitambua wazi kuwa inawezekana kabisa usijibu, au jibu likatufedhehesha zaidi nafsi zetu. Nimefunga na kusali leo kuomba hata kama ni kulisemea hili, basi iwe kwenye maneno ambayo hayatopokelewa kama shambulizi na wala lisije kuendeleza mlolongo wa visasi kama wengi wamekua wakiniaminisha. After all, mimi ni mkazi wa mkoa wako, if anything that should count for something. Allow me to tell like it is, as I believe I always do.

Naamini ni haki yangu kama Mtanzania kusema pale ninapoona sijatendewa haki, na si mimi tu, naandika kwa niaba ya wafanyakazi 33 wa Nyama Choma Festival na watoa huduma, wafanyabiashara na washiriki wote zaidi ya 200 waliokua wanategemea kwa kiasi kikubwa tamasha hili lililokua linafanyika mara 3 kwa mwaka mkoani kwako.

Ni siku nyingi tangu ofisi yako imesikia kutoka kwetu, yaani Waandaji wa Tamasha la Nyama Choma Festival, tangu tulivyokuja mwanzoni mwa mwaka huu (March 2018) na kusisitiziwa na ofisi yako tukufu kuwa bado uamuzi ni ule ule kuhusu matumizi ya Leaders Grounds.

Rejea tamko lako la tarehe 24.11.2017 ambapo ulitangaza kupiga marufuku matukio yanayoenda zaidi ya saa 12 jioni kufanyika viwanja vya Leaders Club. Ulisisitiza kuwa ulitoa ruhusa maalum kwa watayarishaji wa Tamasha la Fiesta kwa sababu maalum lakini ulisema na nanukuu ‘ni haki ya watu kwenye makazi hayo kulala’. Ulitoa rai kuwa ni kutokana na makazi ya watu na ubalozi kwenye eneo.


Tamko hili lilitolewa wiki moja kabla ya tarehe iliyopangwa na kutangazwa kufanyika tamasha letu la nyama choma festival. Tulipatwa na mshtuko mkubwa sana ukizingatia kuna fedha nyingi sana ambazo tayari tulikua tumeshaingia gharama kwenye maandalizi na zisingeweza kurejeshwa.

Rejea barua yetu tuliyokuandikia Desemba 2017 kuomba kama inawezekana na sisi kupewa kibali maalum, kwa masharti kama waliyopewa wenzetu wa Fiesta ya mwisho saa 6 Usiku (ingawa waliruhusiwa kupiga mziki hadi asubuhi). Nikukumbushe tu pia, tamasha letu halina tofauti sana na hilo la wenzetu waliloruhusiwa kwani letu pia huambatanisha burudani ya muziki ingawa main concept ni Nyama Choma za kila aina na biashara mbali mbali.



1*ljwPYI_mxxpgd7L43XND4g.jpeg

Tulifuatilia jibu wiki nzima ofisini kwako huku tukiwataarifu wateja wetu kuwa inabidi tuahirishe tamasha hadi pale ambapo tungepata mbadala. Majibu tuliyopewa sihitaji kukumbusha kwani naamini utakua unayakumbuka fika.

Nilipoona jitihada hizi hazijibiwi, ilibidi niombe msaada kwa kila ninayemfahamu aliye karibu na wewe atoe appeal on my behalf. Hili pia liligonga mwamba. Kwanza mmoja alinijibu kuwa hata hunifahamu. Naomba nikukumbushe mimi ni yule yule Carol tuliyokua tuna mawasiliano ya salaam, na pia ni yule yule niliyokuhoji kwenye kipindi cha siasa za siasa one on one wakati ukiwa Mkuu wa wilaya ya Kinondoni kwa lisaa lizima. Pia ni yule yule anayehusika na kutayarisha hili tamasha ambalo ulihudhuria 5 Desemba 2017 kama picha inavyoonyesha hapa



1*9saOmkKDKENy0Rw6FbdJsQ.jpeg

Hili tamasha la 5 Desemba lililofanyika Leaders lilikua la huzuni pia kwani wakati wa tamasha tulimpoteza mshiriki wetu, mhudhuriaji na supporter mkubwa sana wa tamasha letu, alikua kama mama yetu pia. Rest in Peace Mama Mzungu. Wakati tunashirkiana na kikosi cha polisi kutoa mwili na kuupeleka Muhimbili ulikuwepo na ulikua unasisitizia kama kuna lolote nahitaji kama msaada nikwambie. Sijui kama haya matukio ni kumbukizi tosha, mimi ni yule yule.
Nilijibiwa vitu tofauti,kuna wengine walisema kabisa ‘Carol, hapa pagumu sana’.Wengi walikuwa wananiuliza ‘kwani umemkosea nini’. Kitu ambacho hakikua kwenye kumbukumbu yangu kabisa kwani hata tuhuma zozote zilizokua zinasemwa juu yako hata kipindi kile cha ‘identity crisis’ sikuwahi kutia neno. Nilijihoji sana na kuwauliza wote niliokua nao karibu kama wana kumbukumbu yoyote. Mmoja alinijibu hivi…


1*0UgL2cVEGAY1JuE0rWH40A.jpeg



1*oR_ww-fmuE1o1_0QJmVFqQ.jpeg

Mwisho, nilipigwa simu saa 2 usiku, bahati mbaya nilikua nimeshalala kutokana na kusumbuliwa sana na Pressure wiki hiyo lakini asubuhi nilikutana na Ujumbe huu .



1*B-A6kR01nAE04ObZXStong.jpeg

Nilipo mpigia simu Kaka yangu Lemutuz, kwanza alinitaarifu na ‘kunikanya’ kama Kaka. Alisema kuwa Umeniruhusu kwenda kufanya Tanganyika Packers na nifanye taratibu za kibali. Huwezi kuniruhusu kufanya Leaders kwani umeshatoa tamko na kama kiongozi ukitengua utaonekana hauna msimamo. Nilimshukuru kwa taarifa na kumwambia nitaanza taratibu za kupata uwanja wa Tanganyika Packers.

Hata hivyo kama wengine, nilimuuliza kama anafahamu kama nimewahi kukukosea, kwani hata nilivyoenda ofisini kwako sikuruhusiwa kukuona, jambo lililo si la kawaida ukizingatia utayari wa kiongozi wetu wa mkoa kuonana na wananchi wake kila siku.

Nilihoji ili kama ni kosa, niombe msamaha kwani mimi ni binadamu na si timilifu. Kaka Lemutuz alisema yeye hafahamu na akasema pia ‘kwanza amesema hata hakufahamu na wewe umekua caught kwenye cross fire tu’, nikamkumbusha hilo tamasha la 5 Desemba 2017 kwani walikua wote, na nilivyoenda kuwasabahi na kuwakaribisha kwenye tamasha walikua wamesimama wote. Akasema ‘anyway, inabidi uangalie sana unachoongea, you look like you are anti-government, mimi nakufollow twitter naona unavyoongea, am just telling you to be wise’.

Nilimshukuru kwa ushauri na kumwambia nitamtaarifu taratibu zinaendaje kupapata Tanganyika Packers. Hili pia lilikua na changamoto, na hadi tarehe 8 Desemba asubuhi, siku moja kabla ya tamasha kufanyika Tanganyika Packers tulikua hatujapewa kibali. Hatimaye kilitolewa na tukaendelea na tamasha. Halikua zuri kabisa. Rejea ‘Barua kwako Mjasiriamali unayeanza’ ambayo nilielezea changamoto tulizokutana nazo.




Mhe. Paul Makonda, naandika hii barua kwa kuwa nimetaarifiwa kuwa sasa viwanja vya leaders vinatumika tena, na utenguzi wa tamko umefanya wewe mwenyewe. Ni mwaka mzima sisi kama waandaji tumesitisha shughuli zetu za tamasha kwani ingawa tunafanya mikoa mingine, Dar es Salaam ndio ilikuwa inatuwezesha na kutupa mtaji wa kwenda huko kwingine.

Nilivyosikia tangazo la kwanza la wenzetu,wakitangaza kuwa tamasha lao linafanyika pale pale Leaders nilipata mchanganyiko wa hisia. Kwanza nilifurahi maana nilisema hatimaye, na kama wenzetu wameruhusiwa basi na sisi tutaruhusiwa. Lakini mara baada ya hapo nikapatwa na fedheha, nilipowakumbuka vijana wangu wote na watoa huduma waliokua wanatutegemea, kuwa wamekosa kipato kwa mwaka mzima.

Ni haki yangu kuuliza na kupewa sababu ambazo zimepeleka utenguzi huu na kama kuna mabadiliko yoyote ya sababu ulizotupa uliposema Leaders Grounds Hapafai. Ni ngumu kutokuamini utenguzi umefanyika coincidentally wakati wenzetu wamepanga tamasha lao. Ubinadamu unanifanya nihoji Je sisi la kwetu halina thamani au mchango wowote? Wao hawapigi mziki? makazi ya watu yamehamishwa Leaders sasa? Nawaelewesha vipi wenzangu kuwa haikua personal vendetta, au mimi ndio nilishindwa ‘kuget through’. Kama ni kunyanyua vipaji hata sisi tunanyanyua, kama ni kodi hata sisi tunalipa, na sio sisi tu, wote wanaoshiriki kwenye mnyororo wa thamani wa tamasha hili. Kama ni ajira na fursa, hata sisi tunatoa kupitia tamasha hili. Kwanini ilibidi tuteseke mwaka mzima kama mazingira hayajabadilika?

Nimeambiwa hata mimi nikitaka kufanya sasa naruhusiwa..bahati mbaya tumechelewa sana kwani wadhamini wengi wameshafunga vitabu vyao na bila ya wao hatutaweza kufanikisha.

Nimesali sana kuwa tuweze kuendelea mwaka 2019 na hii ruhusa bado iwepo na tuweze kufanya tamasha kwa amani na kurudisha chanzo kingine cha ajira na vipato kwa mamia ya watu.

Yangu yalikua haya machache, na kama nilivyojihami, sitarajii jibu. Langu lilikua kukueleza tu jinsi ambavyo tuliathirika na tamko lako, na hisia zetu baada ya utenguzi mwaka huu. Pia kukusihi tu kuwa ingawa tunaweza kupishana mitazamo na mawazo, tunajitahidi sana kupitia nyanja mbali mbali kusukuma gurudumu la maendeleo nchini kwetu. Mimi kama Mtanzania najivunia sana nchi yangu and I remain loyal to my purpose which is to contribute to this country’s development. Mimi sio ADUI. Ni mwananchi mwenzako, ni Mama, ni mtoto, ni dada and most importantly, ni BINADAMU.

Naomba Bwana Yesu, Malaika wake na Roho Mtakatifu wakaseme na wewe, wakuonyeshe uchungu tuliopitia. Mwisho nikutakie uongozi mwema wa Mkoa wetu wa Dar, na ushiriki mwema kwenye tamasha linalokuja, natumai na sisi tukikukaribisha mwakani Insh’allah, utajumuika na sisi na kutuunga mkono kama wenzetu.

Namalizia na bandiko kutoka kwa Operations Manager wa Nyama Choma Festival- labda maneno yake pia yataleta mwanga zaidi kwenye hili.






Jibu la Makonda;

Nasikia kuna barua. Barua andika kwa Ofisi ya Mkuu wa mkoa. Humu mitandaoni ofisi haina anwani.
View attachment 943463


Swali la Msingi: Kama malalamiko ya Carol ni valid; kuna sababu zipi za msingi zinazomfanya RC Makonda 'kumbania' Mjasiriamali huyu?!

Mwaka bado haujaisha. Mungu hadhihakiwi. End
 
Tuone basi shepu ya huyo muombaji.isije kuwa inafaa kwa matumizi yetu yale.

Jibu nimelipTa kwenye ule mkanyo wa Lemutuzi kuhusu leaders club
 
Hata ningekuwa mm ndio Makonda nisingempa kibali huyo carol ndossi!
Nakumbuka aliandika waraka mrefu akizitaka jumuiya za kimataifa kuingilia kati Tanzania na akatuaminisha kuwa kuna hali mbaya sana Tanzania na soon inaweza kuwa kama somalia, yaani vita na hakuna amani, sasa leo hii anataka kuandaa tamasha kupitia serikali hyohyo! Unaandaje tamasha wakati unaamini hakuna amani? Mbuzi sana huyo carol
 
Hata ningekuwa mm ndio Makonda nisingempa kibali huyo carol ndossi!
Nakumbuka aliandika waraka mrefu akizitaka jumuiya za kimataifa kuingilia kati Tanzania na akatuaminisha kuwa kuna hali mbaya sana Tanzania na soon inaweza kuwa kama somalia, yaani vita na hakuna amani, sasa leo hii anataka kuandaa tamasha kupitia serikali hyohyo! Unaandaje tamasha wakati unaamini hakuna amani? Mbuzi sana huyo carol
Ndio maaana ya kusoma na kuwa na mawazo yenye manufaaa sio akili mgando kama zako na familiaa yako
 
MLIOPANGA KWENDA FIESTA TAMASHA LIMEFUTWA MKACHUKUE HELA ZENU WA SIMU SUBIRINI HUMO PESA ZENU
 
Back
Top Bottom