Sevenjr
Member
- Aug 3, 2018
- 32
- 127
Anaanza kwa kuelezea; "Mwaka 2012 niliteuliwa kwa mara ya kwanza kuwa Mkuu wa Wilaya na kituo cha kuanzia kazi kilikuwa ni Korogwe.
Wakati huo nilikuwa Kijana zaidi ya sasa. Walimu ni watumishi ninao wapenda sana wakati wote wa Uongozi wangu. Wakati wote wa Uongozi wangu nimekuwa mtetezi wao.
Siku moja nikiwa Wilayani Korogwe nilielekeza niitiwe kikao cha Walimu wote ili niweze kusikiliza changamoto zao ili kwa ushirikiano pamoja na viongozi wenzangu tuzipatie ufumbuzi wa pamoja Kwenye kikao kile kuna Mwalimu alichelewa na alionekana amekunywa kidogo.
Nikamuuliza, Mwalimu kwanini umechelewa kwenye kikao changu? Akaniambia "Mkuu, usinizingue maana mimi nimeshachoka na maisha." Nikamwambia "huna adabu" na kumuagiza OCD amuweke ndani saa 24.
Kama ilivyo kawaida, kesho yake nikaagiza aletwe ofisini ili nimsikilize, akumbuka Mpendwa Mwalimu aliniambia yafuatayo "Mkuu, nihurumie mtumishi wako.
Jana wakati napata wito wako nilikuwa nimemfumania Mke wangu amelala na mwanaume mwingine kwenye kitanda chetu nyumbani.
Sikuona tena thamani ya maisha na nilitamani kujiua Ili kupotezea nikaona bora nijitundike pombe za kienyeji ili angalau nijisahaurishe matatizo."
"Wakati nipo njwii ndio napokea simu ya wito wako,
"Mkuu, Mimi ni wa kusaidiwa na si kuadhibiwa, naomba msamaha".
Kisa cha pili ni "Nilipokua Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma mwaka 2015/2016,
Anasimulia "Siku moja nilimuagiza Mkurugenzi aniandalie kikao cha ghafla cha watendaji wa vijiji na kata.
Kwenye kikao kile watendaji wawili walichelewa kwa zaidi ya masaa 5, nikaagiza wawekwe ndani masaa 24."
Baada ya saa 24 nikaelekeza waletwe ofisini ili nipate utetezi wao.
Mmoja alikuwa ni mtendaji wa Kijiji cha Sibwesa kwenye kata ya Kalya ambako ni Kilomita 422 kutoka makao makuu ya Wilaya ya Uvinza eneo la Lugufu.
Mtendaji kwenye maelezo yake aliniambia "Mkuu nakiri kupokea wito wako wa dharura, lakini kwa masaa 6 nisingeweza kuwahi kutokana na umbali wa Km 422 kutoka kijiji kwangu na makao makuu."
Akaendelea kujitetea "Kutoka kijijini kwangu ambako ni Barabara ya vumbi lazima nipande pikipiki umbali wa Km kama 30 hivi, halafu nipande Boti kisha nipande basi ndio nipate hiace ya kufika Wilayani."
"Kwa hakika hata sikupewa nauli na gharama si chini ya laki moja ambayo ni karibu nusu ya mshahara wangu.
Lakini kwasababu ya wito wa Mkuu nilitumia gharama zangu binafsi na kukimbazana ili niwe nimetii maagizo yako.
Cha kusikitisha nilipofika tu hata kabla ya kunisikiliza ukaagiza niwekwe ndani saa 24."
Akaniambia, "Mkuu mimi nadhani pale ulinionea na ulitumia mamlaka yako vibaya".
Kisa cha tatu "Nilipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma mwaka 2015/2016 nilielekeza Mkurugenzi aniandalie kikao cha haraka cha watendaji wa kata na vijiji.
Kwenye kikao hicho mtendaji wa kata ya Itebula alichelewa kufika kikaoni na bila ya kumsikiliza nikaelekeza awekwe ndani kwa saa 24 kama ilivyo kawaida kesho yake nikaagiza aletwe ofisini kwangu kwa ajili ya utetezi.
Mtumishi yule alipofika ofisini akaanza kujitetea kwa kuniambia "Mkuu, wakati napata wito wa kikao chako nilikuwa hospitali na Mke wangu.
Mke wangu ni mjamzito na alipata matatizo ya Mimba, muda ule napata wito alikuwa chumba cha upasuaji. Kwa kuheshimu wito wako Mkuu nilimwacha mke wangu hospital nikakimbia kuja kwako.
Nilidhani nikifika utanipa pole na kuona nimeheshimu wito wako, badala yake ukaniweka ndani. Leo nimepata taarifa kuwa hali ya Mke wangu na mtoto aliyeko tumboni ni mbaya zaidi.
Mkuu, tukio hili sitalisahau kwenye maisha yangu na mimi nadhani ulininyanyasa na kunionea kwasababu ya unyonge wangu.
Hakika hapa umetumia ubabe na madaraka yako vibaya".
"Kwa hakika nilitamani kulia. Nilijisikia vibaya sana Nilimuomba radhi mtumishi huyu ikiwa ni pamoja na kumrudishia nauli pamoja na mwenzie wa kijiji cha Sibwesa kata ya Kalya."
Kisa hiki ni cha kweli na kilinifanya niache mchezo wa kuwaweka ndani watumishi. Nikaona haja ya kuwasikiliza watumishi kabla ya kuwahukumu.
Mwalimu Nyerere alitunga kitabu cha "Tujisahihishe" ili kuwakumbusha viongozi umuhimu wa kujikosoa.
Anamaliza kwa kusema "Watumishi wenzetu wa chini yetu ni binadamu na Wana changamoto nyingi kama binadamu wengine."
Busara ni kuwapa fursa ya kujitetea kabla ya kuwahukumu.
Hekima ni kushughulikia changamoto zao kwa kufuata kanuni za utumishi wa Umma.
Kupitia kanuni za Utumishi wa umma watapata wasaa wa kujieleza kabla ya kuchukuliwa hatua za "kinidhamu" na "kisheria".
Usione siku hizi siweki watumishi ndani ukadhani sina Mamlaka.
Tena siku hizi mamlaka ni Makubwa zaidi kuliko siku za nyuma, lakini nimetambua kuwa Elimu haina mwisho na nimekubali kujifunza "Uongozi".
Nimeamua kujikosoa pamoja na kufanyia kazi maoni ya wanao nikosoa.
Sisi viongozi vijana bado ni wanafunzi wa Uongozi Kila siku tunajifunza na kupata uzoefu.
"Hakika uzoefu ni mwalimu mzuri!"
Wakati huo nilikuwa Kijana zaidi ya sasa. Walimu ni watumishi ninao wapenda sana wakati wote wa Uongozi wangu. Wakati wote wa Uongozi wangu nimekuwa mtetezi wao.
Siku moja nikiwa Wilayani Korogwe nilielekeza niitiwe kikao cha Walimu wote ili niweze kusikiliza changamoto zao ili kwa ushirikiano pamoja na viongozi wenzangu tuzipatie ufumbuzi wa pamoja Kwenye kikao kile kuna Mwalimu alichelewa na alionekana amekunywa kidogo.
Nikamuuliza, Mwalimu kwanini umechelewa kwenye kikao changu? Akaniambia "Mkuu, usinizingue maana mimi nimeshachoka na maisha." Nikamwambia "huna adabu" na kumuagiza OCD amuweke ndani saa 24.
Kama ilivyo kawaida, kesho yake nikaagiza aletwe ofisini ili nimsikilize, akumbuka Mpendwa Mwalimu aliniambia yafuatayo "Mkuu, nihurumie mtumishi wako.
Jana wakati napata wito wako nilikuwa nimemfumania Mke wangu amelala na mwanaume mwingine kwenye kitanda chetu nyumbani.
Sikuona tena thamani ya maisha na nilitamani kujiua Ili kupotezea nikaona bora nijitundike pombe za kienyeji ili angalau nijisahaurishe matatizo."
"Wakati nipo njwii ndio napokea simu ya wito wako,
"Mkuu, Mimi ni wa kusaidiwa na si kuadhibiwa, naomba msamaha".
Kisa cha pili ni "Nilipokua Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma mwaka 2015/2016,
Anasimulia "Siku moja nilimuagiza Mkurugenzi aniandalie kikao cha ghafla cha watendaji wa vijiji na kata.
Kwenye kikao kile watendaji wawili walichelewa kwa zaidi ya masaa 5, nikaagiza wawekwe ndani masaa 24."
Baada ya saa 24 nikaelekeza waletwe ofisini ili nipate utetezi wao.
Mmoja alikuwa ni mtendaji wa Kijiji cha Sibwesa kwenye kata ya Kalya ambako ni Kilomita 422 kutoka makao makuu ya Wilaya ya Uvinza eneo la Lugufu.
Mtendaji kwenye maelezo yake aliniambia "Mkuu nakiri kupokea wito wako wa dharura, lakini kwa masaa 6 nisingeweza kuwahi kutokana na umbali wa Km 422 kutoka kijiji kwangu na makao makuu."
Akaendelea kujitetea "Kutoka kijijini kwangu ambako ni Barabara ya vumbi lazima nipande pikipiki umbali wa Km kama 30 hivi, halafu nipande Boti kisha nipande basi ndio nipate hiace ya kufika Wilayani."
"Kwa hakika hata sikupewa nauli na gharama si chini ya laki moja ambayo ni karibu nusu ya mshahara wangu.
Lakini kwasababu ya wito wa Mkuu nilitumia gharama zangu binafsi na kukimbazana ili niwe nimetii maagizo yako.
Cha kusikitisha nilipofika tu hata kabla ya kunisikiliza ukaagiza niwekwe ndani saa 24."
Akaniambia, "Mkuu mimi nadhani pale ulinionea na ulitumia mamlaka yako vibaya".
Kisa cha tatu "Nilipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma mwaka 2015/2016 nilielekeza Mkurugenzi aniandalie kikao cha haraka cha watendaji wa kata na vijiji.
Kwenye kikao hicho mtendaji wa kata ya Itebula alichelewa kufika kikaoni na bila ya kumsikiliza nikaelekeza awekwe ndani kwa saa 24 kama ilivyo kawaida kesho yake nikaagiza aletwe ofisini kwangu kwa ajili ya utetezi.
Mtumishi yule alipofika ofisini akaanza kujitetea kwa kuniambia "Mkuu, wakati napata wito wa kikao chako nilikuwa hospitali na Mke wangu.
Mke wangu ni mjamzito na alipata matatizo ya Mimba, muda ule napata wito alikuwa chumba cha upasuaji. Kwa kuheshimu wito wako Mkuu nilimwacha mke wangu hospital nikakimbia kuja kwako.
Nilidhani nikifika utanipa pole na kuona nimeheshimu wito wako, badala yake ukaniweka ndani. Leo nimepata taarifa kuwa hali ya Mke wangu na mtoto aliyeko tumboni ni mbaya zaidi.
Mkuu, tukio hili sitalisahau kwenye maisha yangu na mimi nadhani ulininyanyasa na kunionea kwasababu ya unyonge wangu.
Hakika hapa umetumia ubabe na madaraka yako vibaya".
"Kwa hakika nilitamani kulia. Nilijisikia vibaya sana Nilimuomba radhi mtumishi huyu ikiwa ni pamoja na kumrudishia nauli pamoja na mwenzie wa kijiji cha Sibwesa kata ya Kalya."
Kisa hiki ni cha kweli na kilinifanya niache mchezo wa kuwaweka ndani watumishi. Nikaona haja ya kuwasikiliza watumishi kabla ya kuwahukumu.
Mwalimu Nyerere alitunga kitabu cha "Tujisahihishe" ili kuwakumbusha viongozi umuhimu wa kujikosoa.
Anamaliza kwa kusema "Watumishi wenzetu wa chini yetu ni binadamu na Wana changamoto nyingi kama binadamu wengine."
Busara ni kuwapa fursa ya kujitetea kabla ya kuwahukumu.
Hekima ni kushughulikia changamoto zao kwa kufuata kanuni za utumishi wa Umma.
Kupitia kanuni za Utumishi wa umma watapata wasaa wa kujieleza kabla ya kuchukuliwa hatua za "kinidhamu" na "kisheria".
Usione siku hizi siweki watumishi ndani ukadhani sina Mamlaka.
Tena siku hizi mamlaka ni Makubwa zaidi kuliko siku za nyuma, lakini nimetambua kuwa Elimu haina mwisho na nimekubali kujifunza "Uongozi".
Nimeamua kujikosoa pamoja na kufanyia kazi maoni ya wanao nikosoa.
Sisi viongozi vijana bado ni wanafunzi wa Uongozi Kila siku tunajifunza na kupata uzoefu.
"Hakika uzoefu ni mwalimu mzuri!"