Mkuu wa Mkoa Mwanza atangaza Shilingi bilioni 1.45 zilizodaiwa ‘kupigwa’ zimerejeshwa

DodomaTZ

Member
May 20, 2022
71
107
Miezi minne tangu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Robert Gabriel aagize wanawake, vijana na wenye ulemavu waliotokomea na Shilingi bilioni 4.9 za mikopo ya halmashauri kuzirejesha tayari shiingi bilioni 1.45 zimerejeshwa na vikundi hivyo.

Gabriel alitoa agizo hilo Aprili 25 mwaka huu huku akisema Sh4.9 bilioni ziliyodaiwa kutojulikana ilipo ni sehemu ya Sh8.9 bilioni zilizotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika halmashauri nane za mkoa huo.

Gabriel amewaambia waandishi wa habari kuwa kurejeshwa kwa fedha hizo kumechangiwa na ufuatiliaji uliofanywa na kamati aliyoiunda kufuatilia suala hilo na utoaji wa elimu kwa wanufaika juu ya faida za kukopa na kurejesha fedha hizo.

Amesema kasi ya urejeshaji wa fedha hizo inaridhisha na kuwataka wasimamizi wa ukopeshaji kutorudia makosa ya ukiukwaji wa kanuni, sheria na taratibu za utoaji fedha hizo katika mwaka huu wa fedha ili walengwa mahususi ndiyo wanufaike.

"Ni mapinduzi makubwa na mwelekeo chanya kwamba vikundi vimeanza kurejesha baada ya kushindwa kufanya hivyo kwa zaidi ya miaka mitatu, twende kwa kina tusirudie makosa fedha hizi ziende kwa makundi yaliyokusudiwa," amesema Gabriel.

Ameongeza; "Kuna vikundi vimeitwa lakini havikufika tunavipa muda kuanzia wiki ijayo nitaanza kukutana na vikundi ambavyo havijaanza kabisa kurejesha ili kuhakikisha fedha zote za marejesho zinarudi na kuingia kwenye mzunguko ili kuikomboa jamii yetu na kuleta matokeo chanya,"

Pia amevitaka vikundi ambavyo vilihama Mkoa wa Mwanza vikiwa vimeshakopa fedha hizo kuzirejesha mara moja huku kamati zikipaswa kuendelea kufuatilia maboresho ili masharti na kanuni yazingatiwe fedha hizo zilete matokeo chanya.

Baada ya kurejeshwa kwa kiasi hicho cha fedha mkoa huo unakuwa na kiasi cha shilingi bilioni 2.37 ambazo ziko tayari kwa kukopeshwa ambapo vijana na vikundi vyenye ndoto na malengo vimetakiwa kujitokeza kuandaa maandiko mradi kupata fedha hizo ziwaletee mapinduzi na siyo kuishia kuzitafuna.
 
Upumbavu Mkubwa unaofanywa ni kwamba Ili upate hizo pesa za Halmshauri LAZIMA uwe Mwana CCM. Hapa ndio wamechemka na hili suala limefanyika Tanza-nia nzima. Huwezi kuipata hio fursa kama wewe sio CCM.

Wacha ziliwe na mtakuja kufungwa.... shenzi
 
Katiba mpya itasimamia vema fedha za serikali na kuzibwa mianya ya upigaji KWA kuwekwa mifumo itakayo monitor fedha hizo!

Wala Rais hatokuwa na access ya MOJA kwa MOJA ya kimaamuzi kuhusu fedha za umma!wala kamishna wa TRA wala wanasiasa!!

Mleta mada nakushauri uimbe wimbo huu;-

"Rasimu ya Warioba irudi mezani Sasa iwe Katiba mpya"
 
Mikopo hii ni ya kisiasa zaidi kwani huwalenga wanaccm na viongozi, pesa hizo huwa haziwafikii walengwa kwani hutolewa kwenye majina ya kutunga.
 
Mkuu wa Mkoa alete data tujue:

Vikundi Gani Hasa vimekopeshwa.

Majina na wanufaika wa vikundi hivyo.

Trend ya urejeshaji na ufuatiliaji.

Hizo propaganda asilete humu.
 
Upumbavu Mkubwa unaofanywa ni kwamba Ili upate hizo pesa za Halmshauri LAZIMA uwe Mwana CCM. Hapa ndio wamechemka na hili suala limefanyika Tanza-nia nzima. Huwezi kuipata hio fursa kama wewe sio CCM.

Wacha ziliwe na mtakuja kufungwa.... shenzi
Hii tabia ya kipumbavu wame iingiza hadi kwa makarani wa sensa. Kama huna kadi ya Ccm hupati chance.
Nimewaambia familia yangu siku ya sensa nawapeleka beach. Maana Ccm labda wana fanya sensa ya wanachama wao na sii sensa ya Taifa. Hata tukuta nyumbani. Waache ujinga
 
"Ni mapinduzi makubwa na mwelekeo chanya kwamba vikundi vimeanza kurejesha baada ya kushindwa kufanya hivyo kwa zaidi ya miaka mitatu, twende kwa kina tusirudie makosa fedha hizi ziende kwa makundi yaliyokusudiwa," amesema Gabriel.
Politics

Kuna mambo ya msingi ukisema serikali iyafanye utasikia serikali haina fedha
Lakini mwanasiasa akitaka promo anazungumzia jambo lilelile kwa kinyume
 
Hii tabia ya kipumbavu wame iingiza hadi kwa makarani wa sensa. Kama huna kadi ya Ccm hupati chance.
Nimewaambia familia yangu siku ya sensa nawapeleka beach. Maana Ccm labda wana fanya sensa ya wanachama wao na sii sensa ya Taifa. Hata tukuta nyumbani. Waache ujinga
Saaafi sana, yes nadhani niliwahi kuandika mahali hapa kuwa nafasi za sensa ni za wale wako na kadi za CCM au wanajua kuwa Wana mrengo wa Kijani. Hii taarifa alinipaga Mtendaji wa Kata Mojawaapo huko huko Dar kwenu.
 
Mkuu wa Mkoa alete data tujue:

Vikundi Gani Hasa vimekopeshwa.

Majina na wanufaika wa vikundi hivyo.

Trend ya urejeshaji na ufuatiliaji.

Hizo propaganda asilete humu.
Wote ni CCM kama alivyofanya January Makamba kuzindua kampeni ya kitaifa ya kutumia Gas kwa kuwatumia UWT na Taifa Gas ....bogus
 
Wote ni CCM kama alivyofanya January Makamba kuzindua kampeni ya kitaifa ya kutumia Gas kwa kuwatumia UWT na Taifa Gas ....bogus
Wanaleta MAPAMBIO wakati Hali ya maisha ya weng inazid kuwa mbaya huku wachache wakinufaika.
 
Wanaanzia ujinga huku
 

Attachments

  • 20220719_113532.jpg
    20220719_113532.jpg
    85.7 KB · Views: 5
Back
Top Bottom