Mkuu wa mkoa amtoa ofisini chini ya ulinzi mwenyekiti wa baraza la ardhi na nyumba

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,359
Nimestushwa na habari iliyotoka katika gazeti la Nipashe Jumamosi tarehe 17 April 2010, ukurasa wa tatu kuwa mkuu wa mkoa Kigoma ametuma mapolisi na maafisa wa usalama wa taifa kufunga na kumtoa nje ya ofisi chini ya ulinzi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Kigoma bwana R. J. Kim.

Mkuu wa mkoa huyo alichukua hatua hiyo kutokana na mwenyekiti huyo kupinga maagizo yake mara kwa mara kama mwakilishi wa Rais.

Ni maoni yangu kuwa Baraza la Ardhi na Nyumba ni mahakama iliyoundwa chini ya kifungu 167 cha Sheria ya Ardhi (LAND ACT) Ambayo inampa waziri muhusika wa masuala ya Ardhi kuunda mahakama hiyo chini ya kifungu 22 cha sheria Mahakama za migogoro ya Ardhi ( Land Dispute Courts Act ).Cap 216.

Mabaraza hayo ni mahakama yenye uwezo wa kutatua migogoro yote ya ardhi baada ya kupokea ushahidi kwa kiapo toka pande zote mbili na maamuzi yake yanaweza kutenguliwa na Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi. Kwa mantiki hiyo hii ni mahakama ambayo haipaswi kisheria kuingiliwa, kuagizwa chochote hata na raisi achilia mbali mkuu wa mkoa. Kwa maana kuwa linapotoa maamuzi baraza linatakiwa kufuata sheria za nchi hususani sheria za mikataba, ardhi, ushahidi na mwenendo wa kesi za madai.

Kitendo kilichofanywa na mkuu wa mkoa kama ni cha kweli ( hakijakanushwa mpaka leo) inabidi kilaaniwe kwa kila hali. Chama cha Wanasheria Tanzania, asasi za kiraia zinazoshughulikia masuala ya sheria na wanaharakati wote hawatakiwi kufumbia macho ukiukwaji huu mkubwa na uvunjifu wa msingi wa uhuru wa chombo kinachotoa haki tutoingiliwa na mtu yoyote yule.

Kama mkuu wa mkoa anafanya hivyo leo na hakuna watu wanaolaani kitendo hicho ni kitu gani kitamzuia waziri kesho kuingia mahakamani na kumtoa hakimu aliyetoa maamuzi asiyoyapenda kuhusiana na wizara yake? Kitu gani kitamzuia Rais kukaidi au kudharau amri halali ya mahakama.

Huko tunakoenda ni wapi????
 
Ndo tatizo la kuwa na viongozi wasiojua hata mipaka ya utawala wao.This is purely contempt of court and dwindling of the faith of the public in the effectiveness of the system.
 
Mwacheni rafiki ya mkulu wa nchi, inasikitisha kiongozi mkuu kutofahamu mipaka ya kazi zake halafu eti anataka kugombea ubunge kwao uf*#shiiii...
 
Ndio shida ya kuwapa watu Kazi za uongozi kwa kulipa upendeleo/ au umakini badala ya kuangalia qualifications, qualities na experience ya mtu kama anaimudu kazi hiyo

ama kweli - mambo ya kazi - unaleta MAJESHI???? shame!!!!
 
Hawa Wakuu wa Mikoa ubabe wanaupata wapi?



______________________________________________
War is caused by undefended wealth
- Ernest Hemingway
 
Yes, kuna kazi ukipewa bwana unakuwa above the law!!! Huu ni mfan mdogo tu wa nonsense zinazoendelea ambazo haziangalii nguvu ya kila muhimili wa nchi. Kwahiyo kama akiambiwa kitu akakataa basi ni kutumia mabavu kumtoa? Sio kutumia sheria?
 
mkuu wa mkoa kaharibu kama ni kweli, hana mamlaka ya kutoa order mahakamani ila, ana haki ya kupewa order na mahakama kama ametenda ndivyosivyo. "utamwambia nini mkuu wa mkoa, kama amiri jeshi wa nchi ndie aliyemteua kwa sifa hiyo ya kuingilia mahakama. "huu ni mwendelezo wa ubabe wa serikali kutoka kwenye kukwapua haki za wafanyakazi sasa wanakwapua haki za mahakama" pili huyu mkuu wa mkoa hana washauri kweli "ofisi yake ina mtaalamu anayejulikana kwa cheo cha MSHAURI WA ARDHI NA UPIMAJI' YUPO KILA OFISI YA RASI.
hatuwezi kwenda mbele hivi
 
CHA KUSIKITISHA ZAIDI NA KUSTAAJABISHA ZAIDI MHESHMIWA MWENYEKITI huyo wa Baraza mpaka leo yupo benchi kaletwa Mwenyekiti mwingine kumreplace mwenyekiti huyo aliyedhalilishwa namna hiyo, Nadhani Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi wanastahili kuamka na kutetea haki zao kama walimu walivyokuja juu walimu wenzao kuchapwa bakora na DC Naali, hata kama huyo Mheshmiwa alikuwa amefanya makosa ya aina gani hakuna any justification whatsover kwa nchi yenye utawala wa sheria kwenda kumfurusha akiwa ktk judicial proceedings thats is purely contempt of court, na hatujasikia hatua aliyochukuliwa huyo RC asiyejua utawala wa sheria anafaa kuwa RC wa wanyama wa porini where there are no laws! a Tribunal is a Court, conducting judicial proceedings. Wenyeviti amkeni kama Walimu waliochapwa na DC, hakuna wa kuwatetea kila mtu amekaa kimya ni wachache sana wameshtuka, leo kafurumishwa Chairman of a Tribunal, kesho Magistrate keshokutwa Judge, mwisho kama IDD AMIN, Jugde anatoa hukumu anauwawa, SIMBAKALIA na NDULI IDD AMIN hawana tofauti kwa kitendo hiki! Rule of Law inabomolewa jamani!
 
Nimestushwa na habari iliyotoka katika gazeti la Nipashe Jumamosi tarehe 17 April 2010, ukurasa wa tatu kuwa mkuu wa mkoa Kigoma ametuma mapolisi na maafisa wa usalama wa taifa kufunga na kumtoa nje ya ofisi chini ya ulinzi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Kigoma bwana R. J. Kim.

Mkuu wa mkoa huyo alichukua hatua hiyo kutokana na mwenyekiti huyo kupinga maagizo yake mara kwa mara kama mwakilishi wa Rais.

Ni maoni yangu kuwa Baraza la Ardhi na Nyumba ni mahakama iliyoundwa chini ya kifungu 167 cha Sheria ya Ardhi (LAND ACT) Ambayo inampa waziri muhusika wa masuala ya Ardhi kuunda mahakama hiyo chini ya kifungu 22 cha sheria Mahakama za migogoro ya Ardhi ( Land Dispute Courts Act ).Cap 216.

Mabaraza hayo ni mahakama yenye uwezo wa kutatua migogoro yote ya ardhi baada ya kupokea ushahidi kwa kiapo toka pande zote mbili na maamuzi yake yanaweza kutenguliwa na Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi. Kwa mantiki hiyo hii ni mahakama ambayo haipaswi kisheria kuingiliwa, kuagizwa chochote hata na raisi achilia mbali mkuu wa mkoa. Kwa maana kuwa linapotoa maamuzi baraza linatakiwa kufuata sheria za nchi hususani sheria za mikataba, ardhi, ushahidi na mwenendo wa kesi za madai.

Kitendo kilichofanywa na mkuu wa mkoa kama ni cha kweli ( hakijakanushwa mpaka leo) inabidi kilaaniwe kwa kila hali. Chama cha Wanasheria Tanzania, asasi za kiraia zinazoshughulikia masuala ya sheria na wanaharakati wote hawatakiwi kufumbia macho ukiukwaji huu mkubwa na uvunjifu wa msingi wa uhuru wa chombo kinachotoa haki tutoingiliwa na mtu yoyote yule.

Kama mkuu wa mkoa anafanya hivyo leo na hakuna watu wanaolaani kitendo hicho ni kitu gani kitamzuia waziri kesho kuingia mahakamani na kumtoa hakimu aliyetoa maamuzi asiyoyapenda kuhusiana na wizara yake? Kitu gani kitamzuia Rais kukaidi au kudharau amri halali ya mahakama.

Huko tunakoenda ni wapi????


Wana JF tuwe makini tujadilipo masuala humu ndani. Mkuu huyu wa Mkoa alifanya hivyo (inavyosemekana) baada ya kujulikana kuwa anashindwa kutoa haki kwa Wananchi masikini wa Vijijini. Kwani inasemekana kila kesi iliyokuwa inahusisha tajiri na masikini kuhusu ardhi ilikuwa lazima tajiri atashinda tu!

Pili, Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi SIYO Mahakimu! wao ni wenye viti tu na ajira zao ziko kwa katibu Mkuu wizara ya Ardhi! kwahiyo kujadili humu kuwa kaingilia mamlaka ya Mahakama ni kujadili usicho kijua. Ulizeni kabla ya kutoa hoja humu ndani.

Ahsanteni, nadhani nimeeleweka.
 
Natamani ningekuwa Kikwete ningemfukuza huyo mkuu wa mkoa nilie mchagua mimi mwenyewe. Kashindwa kazi
 
Nimestushwa na habari iliyotoka katika gazeti la Nipashe Jumamosi tarehe 17 April 2010, ukurasa wa tatu kuwa mkuu wa mkoa Kigoma ametuma mapolisi na maafisa wa usalama wa taifa kufunga na kumtoa nje ya ofisi chini ya ulinzi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Kigoma bwana R. J. Kim.

Mkuu wa mkoa huyo alichukua hatua hiyo kutokana na mwenyekiti huyo kupinga maagizo yake mara kwa mara kama mwakilishi wa Rais.

Ni maoni yangu kuwa Baraza la Ardhi na Nyumba ni mahakama iliyoundwa chini ya kifungu 167 cha Sheria ya Ardhi (LAND ACT) Ambayo inampa waziri muhusika wa masuala ya Ardhi kuunda mahakama hiyo chini ya kifungu 22 cha sheria Mahakama za migogoro ya Ardhi ( Land Dispute Courts Act ).Cap 216.

Mabaraza hayo ni mahakama yenye uwezo wa kutatua migogoro yote ya ardhi baada ya kupokea ushahidi kwa kiapo toka pande zote mbili na maamuzi yake yanaweza kutenguliwa na Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi. Kwa mantiki hiyo hii ni mahakama ambayo haipaswi kisheria kuingiliwa, kuagizwa chochote hata na raisi achilia mbali mkuu wa mkoa. Kwa maana kuwa linapotoa maamuzi baraza linatakiwa kufuata sheria za nchi hususani sheria za mikataba, ardhi, ushahidi na mwenendo wa kesi za madai.

Kitendo kilichofanywa na mkuu wa mkoa kama ni cha kweli ( hakijakanushwa mpaka leo) inabidi kilaaniwe kwa kila hali. Chama cha Wanasheria Tanzania, asasi za kiraia zinazoshughulikia masuala ya sheria na wanaharakati wote hawatakiwi kufumbia macho ukiukwaji huu mkubwa na uvunjifu wa msingi wa uhuru wa chombo kinachotoa haki tutoingiliwa na mtu yoyote yule.

Kama mkuu wa mkoa anafanya hivyo leo na hakuna watu wanaolaani kitendo hicho ni kitu gani kitamzuia waziri kesho kuingia mahakamani na kumtoa hakimu aliyetoa maamuzi asiyoyapenda kuhusiana na wizara yake? Kitu gani kitamzuia Rais kukaidi au kudharau amri halali ya mahakama.

Huko tunakoenda ni wapi????

Kiukweli kabisa katika mfumo wa sasa wa serikali za mitaa na tawala za mikoa hawa Wakuu wa Mikoa na Wilaya hawana kazi! Ni nafasi ya watu kulipana fazila na kuwapa ajira zinazotafuna kodi yetu watu fulani katika kuwaasaidia kushiriki vizuri katika mchakato endelevu wa kutafuna rasilimali za nchi hii!

Nafasi hizi ni za kufutiliwa mbali!
 

Objective

To ensure effective and efficient resolution of Land and Housing Disputes.
The activities of the Unit are:
· To oversee and support operations of District Land and Housing Tribunals.
· Manage record of cases registered in District Land and Housing Tribunals.
· To facilitate establishment of new District Land and Housing Tribunals in the country.
· Prepare action plans, progress reports and budget for the unit.
The Unit is led by Registrar assisted by Assistant Registrars. There will be seven District Land and Housing Tribunal zones
For more details,
Contact Us:

Telephone +255 22 2113165/ 2121241-9 Extension 2263
Brochures
DETAILS OF MORE OFFICES
OFISI ZA MABARAZA YA ARDHI NA NYUMBA
SEHEMU ZILIZOPO AN WANI NA NAMBA ZA SIMU
NA
MABARAZA
MAHALI ZILIPO OFISI
ANWANI
NAMBA YA SIMU
1.
ARUSHA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 3194 ARUSHA
2548570
2.
BABATI
MKUU WA MKOA
S.L.P. 621 BABATI
2530669
3.
BUKOBA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 38, BUKOBA
2220342
4.
CHATO
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 118, CHATO
-
5.
DODOMA
HALMASHAURI DODOMA
S.L.P. 4409 DODOMA
2321558
6.
GEITA
IDARA YA ARDHI WILAYA YA GEITA
S.L.P. 645 GEITA
2520050
7.
IFAKARA
MKUU WA WILAYA
S.L.P.195 IFAKARA
2625046
8
ILALA
MKUU WA WILAYA
S.L.P.3616 DSM
28630445
9
IRINGA
JENGO LA UKAGUZI WA HESABU MKABALA NA OFISI YA MANISPAA
S.L.P. 1191 IRINGA
2701450
10
KARATU
JENGO LA OFISI YA POLISI WILAYA
S.L.P. 5 KARATU
2534032
11
KIGOMA
MKUU WA MKOA
S.L.P.1322 KIGOMA
2804777
12
KINONDONI
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 2616 DSM
2170054
13
LINDI
MKUU WA MKOA
S.L.P. 1084 LINDI
2202098
14
MBEYA
JENGO LA IDARA YA MAJI LA ZAMANI
S.L.P.2984 MBEYA
2504218
15
MBINGA
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 144 MBINGA
2640030
16
MOROGORO
ARDHI MKOA
S.L.P. 143 MOROGORO
2614121
17
MOSHI
ARDHI MKOA
S.L.P. 397 MOSHI
2751232
18
MTWARA
ARDHI MKOA
SL.P. 365 MTRWARA
2334236
19
MUSOMA
IDARA YA MAJI
S.L.P. 63 MUSOMA
2620695
20
MWANZA
C.C.M. MKOA MWANZA
S.L.P. 2790 MWANZA
2541868
21
NJOMBE
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 7 NJOMBE
2782023
22
KIBAHA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 30008 KIBAHA
2402257
23
RUNGWE
HALMASHAURI YA WILAYA
S.L.P. 151 TUKUYU
2552225
24
SAME
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 354 SAME
2758190
25
SHINYANGA
MAHAKAMA YA WILAYA
S.L.P. 29 SHINYANGA
2763263
26
SIMANJIRO
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 9519 SIMANJIRO
2555704
27
SINGIDA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 1511 SINGIDA
2502241
28
SONGEA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 707 SONGEA
2602268
29
SUMBAWANGA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 36 SUMBAWANGA
2801059
30
TABORA
MKUU WA MKOA
S.L.P. 1763 TABORA
2605870
31
TANGA
ARDHI MKOA
S.L.P. 5058 TANGA
2642622
32
TARIME
HALMASHAURI YA WILAYA
S.L.P. 394 TARIME
2690045
33
TEMEKE
MKUU WA WILAYA
S.L.P. 2616 DSM
28850212
34
KONDOA
HALMASHAURI YA WILAYA
S.L.P. 223 KONDOA
2360309
35
KOROGWE
JENGO LA KUJITEGEMEA KARIBU NA MAHAKAMA YA WILAYA
S.L.P.
KOROGWE
2640507
36
IRAMBA
JENGO LA KUJITEGEMEA KARIBU NA OFISI YA MKUU WA WILAYA
S.L.P.
2502175
37
MASWA
JENGO LA IDARA YA MAJI (WILAYANI)
S.L.P. 5 MASWA
2750256
38
UKEREWE
JENGO LA MALIASILI
(UKEREWE MJINI)
S.L.P. 2790, MWANZA
2515056
39
MKURANGA
IDARA YA ELIMU (HALMASHAURI YA WILAYA)
S.L.P. 10 MKURANGA
-
District Land and Housing Tribunal Unit | Ministry of Lands and Human Settlements DevelopmentWenyeviti wa Mabara za ya Ardhi ya Nyumba ya Wilaya yanaanzishwa na Waziri mwenye dhamana ya Ardhi (Kifungu cha 22 cha Sheria ya Mahakama (Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi) Na. 2 ya mwaka 2002). Japo Sheria inataja mabaraza hayo kuwa mahakama (Courts),lakini kiutendaji wenyeviti wa mabara hayo ni sawa na watendaji wengine wa umma ambao hawapo katika mfumo wa kawaida wa mahakama ambapo wangestaili kuwa na kinga za kisheria kama ilivyo kwa mahakimu ili wasiingiliwe katika utendahi wao . Kinga waliyonayo tu ni ile ya kulindwa (immunity) kwa vitendo vyovyote watakavyofanya wakiwa wanatimiza majukumu yao (Kifungu cha 55 cha Sheria ya Mahakama (Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi) Na. 2 ya mwaka 2002). Kifungu cha 25 ambacho kinatoa mamlaka kwa Waziri kumteau Mwenyekiti, ambae anapaswa kufanya kazi kwa muda usiozidi miaka mitatu (3), kinampa pia Mkuu wa Mkoa mamlaka ya kumwapisha Mwenyekiti huyo tofauti na ilivyo kwa mahakama za kawaida. Mkuu wa Mkoa pia anahusika katika zoezi la kuteua wazee wa Baraza (Assessors) (kifungu cha 26).


Unaweza kuona katika rekodi za Wizara ya Ardhi hapo juu, hata Ofisi za Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya zipo kwenye Majengo ya Ofisi za Mikoa. Labda hili linaweza kumpa mamlaka Mkuu wa Mkoa kumfanya chochote Mwenyekiti kwa kuona kuwa ni mtu aliyechini yake kama ilivyo kwa watendaji wengine wa Umma.
 
Wana JF tuwe makini tujadilipo masuala humu ndani. Mkuu huyu wa Mkoa alifanya hivyo (inavyosemekana) baada ya kujulikana kuwa anashindwa kutoa haki kwa Wananchi masikini wa Vijijini. Kwani inasemekana kila kesi iliyokuwa inahusisha tajiri na masikini kuhusu ardhi ilikuwa lazima tajiri atashinda tu!

Pili, Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi SIYO Mahakimu! wao ni wenye viti tu na ajira zao ziko kwa katibu Mkuu wizara ya Ardhi! kwahiyo kujadili humu kuwa kaingilia mamlaka ya Mahakama ni kujadili usicho kijua. Ulizeni kabla ya kutoa hoja humu ndani.

Ahsanteni, nadhani nimeeleweka.

Aya yako ya kwanza inanistua kidogo, hao maskini waliokuwa wanashindwa ni kwa nini hawakukata rufaa kupinga hukumu zake, Kama unayosema ni kweli basi hiyo ya kuwa kila tajiri anashinda kesi iliyopo mbeleyake inaweza kuwa sababu ya rufaa kwenye mahakama kuu. Pamoja na yote hiyo haikuwa sababu ya kumtoa mwenyekiti ofisioni.

Pili, Pamoja na kuwa wenyeviti sio mahakimu na ajira zao ziko chini ya katibu mkuu ardhi, lakini wanafanya kazi za kimahakama, quasi judicial, na ni mahakama kwa kila hali. Wanafuata mwenendo wa kisheria kuendesha kesi zao, wanafuata sheria za ushahidi, rufaa zao zinaenda mahakama kuu etc hivyo mkuu wa mkoa hatakiwi kuingili utendaji kazi wao, wanatakiwa wawe huru kabisa.

Mabaraza hayo yameanzishwa chini ya sura 216 ya sheria kama zilivyorekebishwa mwaka 2002, kifungu 22 kinatamka kuwa:

" (1) The Minister shall subject to section 167 of the Land Act * and section 62 of the Village Land Act *, establish in each district, region or
zone, as the case may be, a court to be known as the District Land and Housing Tribunal.

(2) The Court established under subsection (1) shall exercise jurisdiction within the district, region or zone in which it is
established
.

Mkuu wa mkoa kuingilia utendaji wa ni kuingilia uhuru huo ni kosa kubwa sana.
 
@JAPUONY hujaeleweka na sidhani kama umejielewa unachosema WENYEVITI siyo MAHAKIMU ni Wenyeviti tu!!!!!?????!!!! wa Chama gani cha SIASA!!! wao wanatoa HUKUMU na siyo MAAZIMIO au REPORT!! HAKIMU ni yule anayehukumu ndiyo maana hukumu za Land Tribunal zinakatiwa Rufaa kwenda Mahakama Kuu na siyo kwa Waziri, unachosema hapo ni sawa na kusema JESHI LA MAJI/NAVY AU KIKOSI CHA MIZINGA SIYO JESHI jeshi ni infantry tu, wakati wote wamepitia mafunzo hayo hayo, Tribunal is a special Court dealing with specific cases ndiyo maana ikaitwa Tribunal na Sheria Land Act,1999, Land Disputes Courts Act, hata defintion ya sheria zetu nyingi inasema definition ya Court ina include Tribunal, hata mtumishi wa kawaida huondelewa kazini kwa utaratibu maalum bahati Mbaya Wenyeviti hawakuwa na kelele kama Walimu waliochapwa Bakora otherwise huyo Mkuu wa Mkoa angeenda nyumbani, tunachokaribisha hapa ni LAWLESSNESS TANZANIA na itakuja kwa watu wenye mawazo ya SIMBAKALIA nA wewe, sheria imesema ambaye haridhiki na Hukumu akate rufaa Mahakama Kuu na utaratibu wa Kumuondoa Ofisini Mwenyekiti upo ktk Sheria ya Ardhi, 1999 na siyo mabavu. RC huyo alimuondoa ofisini Mwenyekiti kwa kuwa na YEYE ALIANZISHA BARAZA LAKE HARAMU na kutoa Hukumu na alitaka Hukumu zake ziendane na za Mwenyekiti. DICTATORS bwana!
 
Back
Top Bottom