Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,359
Nimestushwa na habari iliyotoka katika gazeti la Nipashe Jumamosi tarehe 17 April 2010, ukurasa wa tatu kuwa mkuu wa mkoa Kigoma ametuma mapolisi na maafisa wa usalama wa taifa kufunga na kumtoa nje ya ofisi chini ya ulinzi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Kigoma bwana R. J. Kim.
Mkuu wa mkoa huyo alichukua hatua hiyo kutokana na mwenyekiti huyo kupinga maagizo yake mara kwa mara kama mwakilishi wa Rais.
Ni maoni yangu kuwa Baraza la Ardhi na Nyumba ni mahakama iliyoundwa chini ya kifungu 167 cha Sheria ya Ardhi (LAND ACT) Ambayo inampa waziri muhusika wa masuala ya Ardhi kuunda mahakama hiyo chini ya kifungu 22 cha sheria Mahakama za migogoro ya Ardhi ( Land Dispute Courts Act ).Cap 216.
Mabaraza hayo ni mahakama yenye uwezo wa kutatua migogoro yote ya ardhi baada ya kupokea ushahidi kwa kiapo toka pande zote mbili na maamuzi yake yanaweza kutenguliwa na Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi. Kwa mantiki hiyo hii ni mahakama ambayo haipaswi kisheria kuingiliwa, kuagizwa chochote hata na raisi achilia mbali mkuu wa mkoa. Kwa maana kuwa linapotoa maamuzi baraza linatakiwa kufuata sheria za nchi hususani sheria za mikataba, ardhi, ushahidi na mwenendo wa kesi za madai.
Kitendo kilichofanywa na mkuu wa mkoa kama ni cha kweli ( hakijakanushwa mpaka leo) inabidi kilaaniwe kwa kila hali. Chama cha Wanasheria Tanzania, asasi za kiraia zinazoshughulikia masuala ya sheria na wanaharakati wote hawatakiwi kufumbia macho ukiukwaji huu mkubwa na uvunjifu wa msingi wa uhuru wa chombo kinachotoa haki tutoingiliwa na mtu yoyote yule.
Kama mkuu wa mkoa anafanya hivyo leo na hakuna watu wanaolaani kitendo hicho ni kitu gani kitamzuia waziri kesho kuingia mahakamani na kumtoa hakimu aliyetoa maamuzi asiyoyapenda kuhusiana na wizara yake? Kitu gani kitamzuia Rais kukaidi au kudharau amri halali ya mahakama.
Huko tunakoenda ni wapi????
Mkuu wa mkoa huyo alichukua hatua hiyo kutokana na mwenyekiti huyo kupinga maagizo yake mara kwa mara kama mwakilishi wa Rais.
Ni maoni yangu kuwa Baraza la Ardhi na Nyumba ni mahakama iliyoundwa chini ya kifungu 167 cha Sheria ya Ardhi (LAND ACT) Ambayo inampa waziri muhusika wa masuala ya Ardhi kuunda mahakama hiyo chini ya kifungu 22 cha sheria Mahakama za migogoro ya Ardhi ( Land Dispute Courts Act ).Cap 216.
Mabaraza hayo ni mahakama yenye uwezo wa kutatua migogoro yote ya ardhi baada ya kupokea ushahidi kwa kiapo toka pande zote mbili na maamuzi yake yanaweza kutenguliwa na Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi. Kwa mantiki hiyo hii ni mahakama ambayo haipaswi kisheria kuingiliwa, kuagizwa chochote hata na raisi achilia mbali mkuu wa mkoa. Kwa maana kuwa linapotoa maamuzi baraza linatakiwa kufuata sheria za nchi hususani sheria za mikataba, ardhi, ushahidi na mwenendo wa kesi za madai.
Kitendo kilichofanywa na mkuu wa mkoa kama ni cha kweli ( hakijakanushwa mpaka leo) inabidi kilaaniwe kwa kila hali. Chama cha Wanasheria Tanzania, asasi za kiraia zinazoshughulikia masuala ya sheria na wanaharakati wote hawatakiwi kufumbia macho ukiukwaji huu mkubwa na uvunjifu wa msingi wa uhuru wa chombo kinachotoa haki tutoingiliwa na mtu yoyote yule.
Kama mkuu wa mkoa anafanya hivyo leo na hakuna watu wanaolaani kitendo hicho ni kitu gani kitamzuia waziri kesho kuingia mahakamani na kumtoa hakimu aliyetoa maamuzi asiyoyapenda kuhusiana na wizara yake? Kitu gani kitamzuia Rais kukaidi au kudharau amri halali ya mahakama.
Huko tunakoenda ni wapi????