Mkuu wa Majeshi, Venance Mabeyo ameamua kuanza kuivunja Katiba ya nchi?

Naona CDF yupo sawa kabisa wajibu wa jeshi sio kupambana na kulinda mipaka ya nchi tu kutoka kwa maadui wa nje huku likishuhudia hali ya amani ikiharibika nchini, bali pia kuzuia viashiria vyote vya uvunjifu wa amani ndani ya nchi. Yapo mambo yanayofanywa na watu ndani ya nchi ambayo yanaweza kupelekea nchi kuingia kwenye machafuko na uvunjifu wa amani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama unadai Jeshi la wananchi ndilo lenye wajibu wa kutafsiri sheria kujua ni nani anatoa kauli za uchochezi, ngoja nikuulize swali dogo tu, hivi na Jeshi la Polisi nalo litafanya kazi gani??

Kutofuatwa kwa sheria za nchi kwa makusudi kwa watawala ndiko kunakoweza kuleta machafuko nchini. OVA
 
Mwisho wa siku huwa wakiona mambo yamekuwa magumu wanaanza kuwakimbilia wana nchi kujifanya wako pamoja nao, ndo maana wasudani kusini walikataa mambo hayo wakamwambia nawewe hatukutaki akabaki kimyaaa, nibora kufikiria kuliko kufikirishwa

sumsung galaxy s10 oreo 8.0
 
Mwisho wa siku huwa wakiona mambo yamekuwa magumu wanaanza kuwakimbilia wana nchi kujifanya wako pamoja nao, ndo maana wasudani kusini walikataa mambo hayo wakamwambia nawewe hatukutaki akabaki kimyaaa, nibora kufikiria kuliko kufikirishwa

sumsung galaxy s10 oreo 8.0
Ndiyo zao, CCM ni mabingwa wa maigizo!
 
Ninachosema ni kuwa Mkuu wa majeshi ni lazima afahamu mipaka yake ya kikazi

Yeye na Jeshi lake wanapaswa wabaki (barracks) na kutulindia mipaka yetu ili tusivamiwe na maadui

Siyo wajibu wake kutafsiri kauli za kichochezi zinazotolewa na wanasiasa.

Wajibu huo awaachie mahakama, waliopewa mamlaka ya kutafsiri sheria nchini
unaweza ukaweka mipaka ya mkuu wa majeshi au mipaka ya jeshi kwenye kazi zake?? orodhesha mipaka miwili tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimebahatika kumsikiliza sehemu flani alikuwa pale vwawa Mkoa wa Momba, aisee kichefu chefu yaani siasa zimemjaa uccm ccm tu nilikwazika sana.
 
Nimebahatika kumsikiliza sehemu flani alikuwa pale vwawa Mkoa wa Momba, aisee kichefu chefu yaani siasa zimemjaa uccm ccm tu nilikwazika sana.
Yaani ni kitu cha hatari sana kwa CDF kujiingiza kwenye siasa!

Kama anaelekea kuipenda sana siasa, atuvulie magwanda yetu ya Jeshi na avae magwanda ya kijani ili tukapambane naye vizuri kwenye majukwaa ya kisiasa
 
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu, mkuu wa majeshi nchini, Venance Mabeyo, akiwapiga mkwara watanzania, kuwa wao kama Jeshi la wananchi nchini, wanafuatilia kwa karibu kile alichokiita kuwa ni kauli za kichochezi zenye nia ya kuleta machafuko nchini

Wajibu wa Jeshi la Wananchi nchini

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 147(3) imesema wazi kuwa itakuwa marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chochote cha siasa nchini, na jukumu lao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu, kuhakikisha kuwa hatuvamiwi na nchi yeyote jirani. Mwisho wa kunukuu

Katiba ya nchi inasema wazi kuwa mwanajeshi yeyote hatakiwi kujiunga na chama chochote cha kisiasa na imeeleza kuwa wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu ili tusivamiwe. Sasa nilichokisikia kutoka kwa mkuu wa majeshi ndiyo wajibu wake kikatiba??

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) inaeleza wazi kuwa kila mwananchi yuko huru kutoa maoni yake, kuhusiana na uendeshaji wa nchi yake

Katiba hiyo hiyo ya nchi imeeleza wazi kuwa chombo pekee cha kutafsiri sheria ni mahakama na ndiyo wanaoweza kusema kuwa kauli iliyotolewa na mwanasiasa fulani ni ya kichochezi au laa

Sasa, kwa Mkuu wa majeshi nchini kupiga mkwara mzito kuwa eti Jeshi lake halitavumilia kauli yoyote ya kichochezi, siyo kuivunja Katiba ya nchi waziwazi na kuingilia mhimili wa mahakama kiutendaji?

Wao wanajeshi wanapaswa wabaki (barracks) na wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu na hawapaswi hata kidogo kuingilia mambo ya kisiasa nchini, kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wanataka kuleta machafuko nchini.

Mungu ibariki Tanzania
Walituonyesha mkuu was Tiss ,sasa CDF WAMEAMUa kuacha kutumia akili na busara wanatumia nguvu...
Hakuna jeshi Wala majeshi ya kuishinda nguvu ya umma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninachosema ni kuwa Mkuu wa majeshi ni lazima afahamu mipaka yake ya kikazi

Yeye na Jeshi lake wanapaswa wabaki (barracks) na kutulindia mipaka yetu ili tusivamiwe na maadui

Siyo wajibu wake kutafsiri kauli za kichochezi zinazotolewa na wanasiasa.

Wajibu huo awaachie mahakama, waliopewa mamlaka ya kutafsiri sheria nchini
Wanatumika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunajua kuwa Katiba ya nchi inampiga marufuku Mkuu wa majeshi nchini, kujiingiza kwenye mambo ya kisiasa

Kama yeye Venance Mabeyo "anatamani" kuwa mwanasiasa, tunamwomba kwanza avue magwanda yetu ya Jeshi, ili avae nguo za kijani, ili aweze kupambana katika ulingo wa kisiasa
Hapo utakuta upo kwenye list ya wanaotafutwa na HUYU mabeyovery very cheap .
Anajishusha hadhi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kila siku anakubali kuitwa kwenye mikutano ya kisiasa na anakubali tu aelewe kuwa anashiriki siasa.Wanaomuita wanataka awatishe watu anapoonekana.Naye ameshauingia mtego wa wanasiasa na kujikuta anaenda kinyume na katiba.CDF kuonekana kila siku na genge la wanasiasa haileti afya njema katika nchi inayoshiriki siasa za vyama vingi.Ni vema atulie asijivunjie heshima na kuanza kupata tamaa ya uongozi wa kisiasa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ni yeye Mkuu wa majeshi ndiye anayeweza kutafsiri kauli za kichochezi??

Katiba inasema ni mhimili wa mahakama pekee ndiyo uliopewa mamlaka ya kutafsiri sheria nchini
Nchi ikichafuka wenye wajibu wakupambana ni nani? Kinga ni bora kuliko tiba halafu kama wewe unafahamu sana katiba si ukafungue kesi sasa mbona unalalamika huku jf.
 
Nchi ikichafuka wenye wajibu wakupambana ni nani? Kinga ni bora kuliko tiba halafu kama wewe unafahamu sana katiba si ukafungue kesi sasa mbona unalalamika huku jf.
Mbona umetaharuki?Nchi imechafukia wapi?Kama unaona alivyoandika humu JF amekosea sasa weye unafanya nini humu?Nenda kaungane nao huko mabarabarani.
 
Hilujui kutafsiri hotuba ama wewe ni mnafiki. Mkuu wa majeshi anayo haki kusema alichokisema, na hakuingilia siasa ya vyama. Uchochezi unaweza kuwa mipakani, na watu wakutaka kutuharibia amani ya nchi yetu.

Mkuu wa Majeshi inatakiwa mara mojamoja sauti yake isikike ikinguruma, ili wale wanaotaka kuruletea machafuzi waogope, laki haina maana eti anawakabili watanzania wa vyama vya upinzani. Hakuna hilo
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu, mkuu wa majeshi nchini, Venance Mabeyo, akiwapiga mkwara watanzania, kuwa wao kama Jeshi la wananchi nchini, wanafuatilia kwa karibu kile alichokiita kuwa ni kauli za kichochezi zenye nia ya kuleta machafuko nchini

Wajibu wa Jeshi la Wananchi nchini

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 147(3) imesema wazi kuwa itakuwa marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chochote cha siasa nchini, na jukumu lao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu, kuhakikisha kuwa hatuvamiwi na nchi yeyote jirani. Mwisho wa kunukuu

Katiba ya nchi inasema wazi kuwa mwanajeshi yeyote hatakiwi kujiunga na chama chochote cha kisiasa na imeeleza kuwa wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu ili tusivamiwe. Sasa nilichokisikia kutoka kwa mkuu wa majeshi ndiyo wajibu wake kikatiba??

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) inaeleza wazi kuwa kila mwananchi yuko huru kutoa maoni yake, kuhusiana na uendeshaji wa nchi yake

Katiba hiyo hiyo ya nchi imeeleza wazi kuwa chombo pekee cha kutafsiri sheria ni mahakama na ndiyo wanaoweza kusema kuwa kauli iliyotolewa na mwanasiasa fulani ni ya kichochezi au laa

Sasa, kwa Mkuu wa majeshi nchini kupiga mkwara mzito kuwa eti Jeshi lake halitavumilia kauli yoyote ya kichochezi, siyo kuivunja Katiba ya nchi waziwazi na kuingilia mhimili wa mahakama kiutendaji?

Wao wanajeshi wanapaswa wabaki (barracks) na wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu na hawapaswi hata kidogo kuingilia mambo ya kisiasa nchini, kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wanataka kuleta machafuko nchini.

Mungu ibariki Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona umetaharuki?Nchi imechafukia wapi?Kama unaona alivyoandika humu JF amekosea sasa weye unafanya nini humu?Nenda kaungane nao huko mabarabarani.
Katiba inakupa mamlaka ya kwenda kushtaki mahakamani kama unaona general amekosea ukilalamika hapa haitakusaidia kitu badala yake utaishia kufarijiwa tu.
 
Hilujui kutafsiri hotuba ama wewe ni mnafiki. Mkuu wa majeshi anayo haki kusema alichokisema, na hakuingilia siasa ya vyama. Uchochezi unaweza kuwa mipakani, na watu wakutaka kutuharibia amani ya nchi yetu.

Mkuu wa Majeshi inatakiwa mara mojamoja sauti yake isikike ikinguruma, ili wale wanaotaka kuruletea machafuzi waogope, laki haina maana eti anawakabili watanzania wa vyama vya upinzani. Hakuna hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
Wacha kudanganya wewe, eti kwa tafsiri yako alikuwa anamaanisha kupambana na wale wanaotoa kauli za kichochezi mipakani!

Nimemsikia akisema kuna kauli tata zinazotolewa na wanasiasa na wao kama Jeshi la wananchi wamejipanga kupambana na watu hao kwa nguvu zote!

Hujaona tu namna mkuu wa majeshi alivyoanza kuvunja Katiba ya nchi??

Wao wanaopaswa wabakie "barracks" na jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kuwa mipaka ya nchi yetu ipo salama
 
1. Kulinda mipaka ya nchi yetu, kuhakikisha kuwa hatuvamiwi na maadui
2. Kubangua korosho kwa "maagizo" ya Amiri Jeshi Mkuu
je unafahamu namna mipaka inavyolindwa ili maadui wasivamie?? ukishaelewa jinsi inavyolindwa basi utafaham kauli alioitoa alikua sahihi ila kwa kua ww ni mwanasiasa tena nahisiwa upinzani ndio maana ukahitimisha kuwa kutumia muhemuko wa siasa,ilo la pili najua umelijibu kwa kutumia matako sio akili yakk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom