Mkuu wa Majeshi, Venance Mabeyo ameamua kuanza kuivunja Katiba ya nchi?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu, mkuu wa majeshi nchini, Venance Mabeyo, akiwapiga mkwara watanzania, kuwa wao kama Jeshi la wananchi nchini, wanafuatilia kwa karibu kile alichokiita kuwa ni kauli za kichochezi zenye nia ya kuleta machafuko nchini

Wajibu wa Jeshi la Wananchi nchini

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 147(3) imesema wazi kuwa itakuwa marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chochote cha siasa nchini, na jukumu lao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu, kuhakikisha kuwa hatuvamiwi na nchi yeyote jirani. Mwisho wa kunukuu

Katiba ya nchi inasema wazi kuwa mwanajeshi yeyote hatakiwi kujiunga na chama chochote cha kisiasa na imeeleza kuwa wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu ili tusivamiwe. Sasa nilichokisikia kutoka kwa mkuu wa majeshi ndiyo wajibu wake kikatiba??

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) inaeleza wazi kuwa kila mwananchi yuko huru kutoa maoni yake, kuhusiana na uendeshaji wa nchi yake

Katiba hiyo hiyo ya nchi imeeleza wazi kuwa chombo pekee cha kutafsiri sheria ni mahakama na ndiyo wanaoweza kusema kuwa kauli iliyotolewa na mwanasiasa fulani ni ya kichochezi au laa

Sasa, kwa Mkuu wa majeshi nchini kupiga mkwara mzito kuwa eti Jeshi lake halitavumilia kauli yoyote ya kichochezi, siyo kuivunja Katiba ya nchi waziwazi na kuingilia mhimili wa mahakama kiutendaji?

Wao wanajeshi wanapaswa wabaki (barracks) na wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu na hawapaswi hata kidogo kuingilia mambo ya kisiasa nchini, kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wanataka kuleta machafuko nchini.

Mungu ibariki Tanzania
 
Katiba iheshimiwe na watu wote, machafuko ya ndani kwenye nchi nyingi mara nyingi huwa yanaletwa na watawala kutofuata katiba.
Ninachosema ni kuwa Mkuu wa majeshi ni lazima afahamu mipaka yake ya kikazi

Yeye na Jeshi lake wanapaswa wabaki (barracks) na kutulindia mipaka yetu ili tusivamiwe na maadui

Siyo wajibu wake kutafsiri kauli za kichochezi zinazotolewa na wanasiasa.

Wajibu huo awaachie mahakama, waliopewa mamlaka ya kutafsiri sheria nchini
 
sometimes ukiwatisha watu unawafanya wajipange na kuwa aggressive zaidi. ni reaction ya kawaida ya wanyama na binadamu.
Tunajua kuwa Katiba ya nchi inampiga marufuku Mkuu wa majeshi nchini, kujiingiza kwenye mambo ya kisiasa

Kama yeye Venance Mabeyo "anatamani" kuwa mwanasiasa, tunamwomba kwanza avue magwanda yetu ya Jeshi, ili avae nguo za kijani, ili aweze kupambana katika ulingo wa kisiasa
 
Bahati mbaya si wote wataelewa unachomaanisha. Tumekuwa Taifa la kila nyanja kuna harufu ya kisiasa.
Wale wa miwani za jua tushazowea, sasa na hawa wanaingia huko huko.
Wakati mwingine nashindwa kuelewa dhamira yawatawala na ya utawala huu.
 
Tunajua kuwa Katiba ya nchi inampiga marufuku Mkuu wa majeshi nchini, kujiingiza kwenye mambo ya kisiasa

Kama yeye Venance Mabeyo "anatamani" kuwa mwanasisa, tunamwomba kwanza avue magwanda yetu ya Jeshi, ili avae nguo za kijani, ili aweze kupambana katika ulingo wa kisiasa
Jamaa kaona NDIYOOOO hazitoshi sasa anazisaka hasa, yaani kama hutaki kusema NDIYOOOO basi nyamaza, la sivyo utaitwa mchochezi.
Kwanza toka lini mwanajeshi akamkamata raia kwasabu ya kauli tu?
Mbona tunaona mara kwa mara Wasomali wanachaniza tu mipakani?
 
Hizo kauli za vitisho kabla ya kuzitoa aangalie nyakati,ile nadharia ya kuamini watz ni waoga wajinga waitafakari mara Mbili Mbili. Salama yao si vifaru wa mabomu hayo huwa mazito kuyatumia wakati ukifika, Salama yao iko kwenye kutenda haki kwa walipa kodi.Wakidhani wana nguvu kuliko umma wajitafakari.Gadafi ,Bashiru, Mugabe nk waliwekeza kwenye jeshi na hali kuwasaidia.Upepo wa Sudan utafika utakuja tu Africa Mashariki watafute makaravati ya kujifichia kama wataendelea kutenda dhuluma.
 
Tumemsikia wenyewe kwa masikio yetu, mkuu wa majeshi nchini, Venance Mabeyo, akiwapiga mkwara watanzania, kuwa wao kama Jeshi la wananchi nchini, wanafuatilia kwa karibu kile alichokiita kuwa ni kauli za kichochezi zenye nia ya kuleta machafuko nchini

Kwanza lazima tuelewe wajibu wa Jeshi la wananchi nchini

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 147(3) imesema wazi kuwa itakuwa marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chochote cha siasa nchini, na jukumu lao kubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu, kuhakikisha kuwa hatuvamiwi na nchi yeyote jirani. Mwisho wa kunukuu

Katiba ya nchi inasema wazi kuwa mwanajeshi yeyote hatakiwi kujiunga na chama chochote cha kisiasa na imeeleza kuwa wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu ili tusivamiwe. Sasa nilichokisikia kutoka kwa mkuu wa majeshi ndiyo wajibu wake kikatiba??

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) inaeleza wazi kuwa kila mwananchi yuko huru kutoa maoni yake, kuhusiana na uendeshaji wa nchi yake

Katiba hiyo hiyo ya nchi imeeleza wazi kuwa chombo pekee cha kutafsiri sheria ni mahakama na ndiyo wanaoweza kusema kuwa kauli iliyotolewa na mwanasiasa fulani ni ya kichochezi au laa

Sasa kwa Mkuu wa majeshi nchini kupiga mkwara mzito kuwa eti Jeshi lake halitavumilia kauli yoyote ya kichochezi, siyo kuivunja Katiba ya nchi waziwazi na kuingilia mhimiki wa mahakama kiutendaji??

Wao wanajeshi wanapaswa wabaki (barracks) na wajibu wao mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi yetu na hawapaswi hata kidogo kuingilia mambo ya kisiasa nchini, kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wanataka kuleta machafuko nchini

Mungu ibariki Tanzania
Kwani yeye peke take? Uongozi wote wa nchi yetu umeweka Katiba na sheria zote pembeni na kuongoza kwa amri na maagizo toka juu. Ni Awamu ya mipango, mikakati na michakato ya mikutanoni, kwenye semina na makongamano wananchi wakiachwa na matatizo yao wakitakiwa kuwa wazalendo na wapende nchi yao.
 
Tunajua kuwa Katiba ya nchi inampiga marufuku Mkuu wa majeshi nchini, kujiingiza kwenye mambo ya kisiasa

Kama yeye Venance Mabeyo "anatamani" kuwa mwanasiasa, tunamwomba kwanza avue magwanda yetu ya Jeshi, ili avae nguo za kijani, ili aweze kupambana katika ulingo wa kisiasa
Tatizo la nchi yetu hii ni siasa. Hata wasiotakiwa kufanya siasa nao hujiingiza ktk siasa.

Tatizo kubwa pia ni kuhakikisha kuwa vyombo vyote vya dola vinaongozwa na makada waaminifu kwa chama kimoja. Ndiyo maana kina Mabeyo uzalendo unawashinda wanajikuta wanafanya siasa hadharani. Kwa watawala kwao ni sherehe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kila siku anakubali kuitwa kwenye mikutano ya kisiasa na anakubali tu aelewe kuwa anashiriki siasa.Wanaomuita wanataka awatishe watu anapoonekana.Naye ameshauingia mtego wa wanasiasa na kujikuta anaenda kinyume na katiba.CDF kuonekana kila siku na genge la wanasiasa haileti afya njema katika nchi inayoshiriki siasa za vyama vingi.Ni vema atulie asijivunjie heshima na kuanza kupata tamaa ya uongozi wa kisiasa.
 
Screenshot_20190414-045935.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo kauli za vitisho kabla ya kuzitoa aangalie nyakati,ile nadharia ya kuamini watz ni waoga wajinga waitafakari mara Mbili Mbili. Salama yao si vifaru wa mabomu hayo huwa mazito kuyatumia wakati ukifika, Salama yao iko kwenye kutenda haki kwa walipa kodi.Wakidhani wana nguvu kuliko umma wajitafakari.Gadafi ,Bashiru, Mugabe nk waliwekeza kwenye jeshi na hali kuwasaidia.Upepo wa Sudan utafika utakuja tu Africa Mashariki watafute makaravati ya kujifichia kama wataendelea kutenda dhuluma.
Absolutely true

Hivi hawa watawala wetu hawajifunzi kile kilichotokea Zimbabwe na Sudan??

Akina Mugabe na Al Bashir waliwekeza kwa nguvu zote kwenye
Hivi huyu Jenerali Mabeyo anaisoma kweli hii Katiba yetu ya nchi??
 
64 Reactions
Reply
Back
Top Bottom