Mkuu wa Majeshi Nigeria anena kuhusu Magaidi

Alwaz

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,080
10,741
Mkuu wa majeshi wa Nigeria Lt Gen Tukur Yusuf Buratai amesema magaidi nchini humo wataendelea kuwepo hata baada ya miaka 20 ijayo.

Maelezo hayo ameyatoa kwenye ukurasa wake wa twitter baada ya kutokwa kwa mauwaji ya watu 43 yanayosemekana yalitekelezwa na Bokoharam. Maoni yake hayo yamekuja sambamba na wito wa baadhi ya wanasiasa wanaotaka Luteni huyo avuliwe madaraka kwa kushindwa kumaliza tatizo la matendo ya kigaidi.

Mkuu huyo wa majeshi bila kutoa ufafanuzi amesema kuna kutokufahamika kuliko wazi kwa maana ya ugaidi na mambo yanayofungamana nayo. Akazidi kusema kuwa ipo haja ya kuchukua hatua za pamoja na uwajibikaji ulio mpana.

1607015278145.png

Wakati huo huo polisi wa nchi hiyo wamelazimika kuwafanyia paredi wahalifu waliowashika baada ya kuzuka sokomoko kweny mitandao ya kijamii kwa kutoridhishwa na picha iliyotolewa awali na jeshi hilo ambapo watu wengi walitilia shaka picha hiyo wakisema ilikuwa na ishara za kutengenezwa.

Hii ni mwendelezo wa malalamiko ya wananchi wa nchi hiyo kwa askari na kutilia shaka baadhi ya matukio yanayotokea nchini humo. Hata hivyo haijulikani iwapo paredi hiyo iliwahusisha wahalifu wale wale waliotiliwa shaka na wananchi au ni watuhumiwa wengine katika kuzima sintofahamu za wananchi hao juu ya utendaji wa jeshi hilo.
 
Huyu mkuu atakuwa anajuwa kwa undani kinachotokea kuhusiana na ugaidi ila kutokana na nidhamu za kijeshi hawezi kutoa ufafanuzi.Ndio maana anasema watu wawajibike kwa pamoja. Na ikifika hapo huenda akatolewa kafara kwa kuonekana yeye ndiye mzembe na ili ugaidi usimalizike.
 
Afrika hakuna vikosi imara vya counterinsurgency. Wote waogawaoga na waliokosa nidhamu. Nilisoma stori ya jamaa wa Guatemala wanaitwa Kabil. Wakiingia msituni hawatoki mpaka waasi waishe. Watakula nyoka na vyura mpaka kieleweke humo.
Motto wao wanasema; nikisonga mbele nifuate, nikisimama, nihimize nisonge, nukirudi nyuma niue.
Sasa Nigeria wanajua msitu waliko boko haramu lakini wanalenga kwa mbali.

mo
 
Nigeria inasumbuliwa na rushwa

We lini umesikia hapa Tanzania kuna wakubwa jeshini wapo na kesi za ufisadi ? Sasa Nigeria ni kila siku utasikia kwenye vyombo vya habari Jenerali fulani katiwa hatiani kala kiasi fulani fedha za umma


Mnadhimu mkuu wa Jeshi la ardhini ambae aliondolewa madarakani wakati buhari anaingia Ikulu alirudisha fedha nyingi tu baada ya kubumbuluka kuwa kapiga
 
Afrika hakuna vikosi imara vya counterinsurgency. Wote waogawaoga na waliokosa nidhamu. Nilisoma stori ya jamaa wa Guatemala wanaitwa Kabil. Wakiingia msituni hawatoki mpaka waasi waishe. Watakula nyoka na vyura mpaka kieleweke humo.
Motto wao wanasema; nikisonga mbele nifuate, nikisimama, nihimize nisonge, nukirudi nyuma niue.
Sasa Nigeria wanajua msitu waliko boko haramu lakini wanalenga kwa mbali.

mo
Sio sahihi kuwa nchi zote Afrika zina askari waoga.Kule Guetemala wanapigana na tatizo halisi na kila askari anapata ushujaa.Huku kwetu ni matatizo hiyo mpaka askari wanaona kama wamerogwa hawaoni kitu.
 
Nigeria inasumbuliwa na rushwa

We lini umesikia hapa Tanzania kuna wakubwa jeshini wapo na kesi za ufisadi ? Sasa Nigeria ni kila siku utasikia kwenye vyombo vya habari Jenerali fulani katiwa hatiani kala kiasi fulani fedha za umma


Mnadhimu mkuu wa Jeshi la ardhini ambae aliondolewa madarakani wakati buhari anaingia Ikulu alirudisha fedha nyingi tu baada ya kubumbuluka kuwa kapiga
Ya Abdulrahman Shimbo unayajua?
 
Wewe una amini Tanzania hakuna rushwa wala ufisadi huko jeshini?
Nigeria inasumbuliwa na rushwa

We lini umesikia hapa Tanzania kuna wakubwa jeshini wapo na kesi za ufisadi ? Sasa Nigeria ni kila siku utasikia kwenye vyombo vya habari Jenerali fulani katiwa hatiani kala kiasi fulani fedha za umma


Mnadhimu mkuu wa Jeshi la ardhini ambae aliondolewa madarakani wakati buhari anaingia Ikulu alirudisha fedha nyingi tu baada ya kubumbuluka kuwa kapiga
 
Wewe una amini Tanzania hakuna rushwa wala ufisadi huko jeshini?
Maneno ya hisia tuu?

Nigeria it as if a usual business ni mara kwa mara utasikia Jenerali fulani katiwa hatiani kesi ya ufisadi alipiga kiasi kadhaa


Mi kwa Tanzania mpaka leo hii sijawahi sikia mwanajeshi wa vyeo vya ujenerali katiwa hatiani ufisadi
 
Tungekua na watu wanajitambua kwa angalau asilimia 20% ungesikia mengi mkuu..fikiria tu kwa sasa sheria zinavyovunjwa wazi wazi na hakuna anayehoji basi jua hata huko jeshi kuna mengi tu yanaendelea ila hakuna pa kusemea wala wa kuwachunguza maana hatuna vyombo huru nchi hii kuanzia bunge,mahakama na taasisi nyingine nyeti.
Maneno ya hisia tuu?

Nigeria it as if a usual business ni mara kwa mara utasikia Jenerali fulani katiwa hatiani kesi ya ufisadi alipiga kiasi kadhaa


Mi kwa Tanzania mpaka leo hii sijawahi sikia mwanajeshi wa vyeo vya ujenerali katiwa hatiani ufisadi
 
Afrika hakuna vikosi imara vya counterinsurgency. Wote waogawaoga na waliokosa nidhamu. Nilisoma stori ya jamaa wa Guatemala wanaitwa Kabil. Wakiingia msituni hawatoki mpaka waasi waishe. Watakula nyoka na vyura mpaka kieleweke humo.
Motto wao wanasema; nikisonga mbele nifuate, nikisimama, nihimize nisonge, nukirudi nyuma niue.
Sasa Nigeria wanajua msitu waliko boko haramu lakini wanalenga kwa mbali.

mo
Spirit ya hatari sana hii...
 
Mada nzuri imekosa wachangiaji wengi
Nashangaa sana watu wanashindwa kuona kitu kama hiki kuzungumzwa na mkuu wa majeshi.Wachangiaji wengi wanavutiwa na maneno ya vijiweni kuhusu ugaidi.
 
Jeshi Lao ni very corrupt, mwaka 2016 aliekuwa security adviser alipiga $68m na wenzake huku zikiwa zimeombwa kwa kununulia helicopters, fighter jets na mabomu ili kupambana na BH
Tatizo lao nchi imejaa wapiga dili sana na wajanja wajanja
 
Jeshi Lao ni very corrupt, mwaka 2016 aliekuwa security adviser alipiga $68m na wenzake huku zikiwa zimeombwa kwa kununulia helicopters, fighter jets na mabomu ili kupambana na BH
Tatizo lao nchi imejaa wapiga dili sana na wajanja wajanja
Ee bwana we ! hayo mawazo yako ni ya kuzuga zuga tu.Hizo pesa wacha ziliwe kwa sababu haingii akilini kwamba kuna fungu la kununua mabomu na helicopter kwa ajili ya kupambana na mwehu na kizuu kama Abubakari Shekau.Mtu asiyefahamika vyema.
Hawa mabeberu wanaoshikilia propaganda za ugaidi sasa wameishika vibaya kusini mwa Afrika na wana hamu ya kufungua tawi la ugaidi na kulipa jina lao na waseme limekula kiapo kwa ISIS au Alqaeda.Ukiondoa Tanzania nchi za kusini mwa Afrika zina idadi ndogo ya waislamu lakini bado inaelezwa magaidi wana nguvu sana hata kushinda majeshi ya nchi hizo na sasa ziko kwenye mjadala ya kutafuta misaada .
 
Back
Top Bottom