Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Marekani Afrika afungua mazoezi ya kijeshi baina ya US na Tanzania

Kwani tuliwahi kisimama lini? Au unaamini Tanzania kuna wakati wowote iliwahi kumpinga Marekani na nchi za magharibi na ikafanikiwa?
Kwa hiyo, kama huwezi shindana. Ungana nao. Hawa mafedhuli wako after kitu. Hata demokrasia ni sehemu tu ya kuhakikisha maslahi yao yanalindwa na fimbo kwa wale wanaowazingua.
 
Nyerere hakutaka jwtz iwe na umoja na USA alijua marekani wana Tabia za kuchunguza udhaifu kisha kuleta shida baadae akawakataa kwenye idara za kijeshi lakini alishirikiana nao katika nyanja zingine kabsa
Kilichomponza ni ujamaa, ila suala la mafunzo ni la kawaida tu kwa sasa.
 
Kamanda wa Kamandi ya Afrika ya Jeshi la Marekani (AFRICOM) Jenerali Stephen Townsend, alikuwa na ziara ya siku mbili nchini Tanzania, tarehe 27 na 28 Julai, ambapo alikutana na maafisa waandamizi wa jeshi na kufungua mazoezi ya kwanza ya pamoja ya kijeshi ya nchi hizi mbili toka mwaka 2017...
Ahsante sana Rais wetu Mama Samia kwa kuimarisha uhusiano wetu na ndugu na rafiki zetu Wamarekani.

God bless relationship between USA and TANZANIA.
 
Ilianza kuonekana ndege imekaa tuu pale uwanja wa ndege taarifa ikatoka inaleta vifaa vya ubalozi wiki chache baadae tunaskia Tanzania imepokea msaada wa chanjo kutoka marekani chanjo imefika tuu ghafla marekani anafanya mazoezi ya pamoja na. Majeshi yetu naweza nikawa na akili fupi kwa mitazamo ya wengi lakini kwa akili ndogo tuu naiona shida kubwa sana mbeleni ninahofu na dunia ya wakati ujao zile movie za ma vampire nadhani ni wakati wa mabadiriko ya mwanadamu
mkuu we tayari ni vampire...wala hauhitaji kuisubiri hiyo dunia.....😀😀😀😀
 
Kamanda wa Kamandi ya Afrika ya Jeshi la Marekani (AFRICOM) Jenerali Stephen Townsend, alikuwa na ziara ya siku mbili nchini Tanzania, tarehe 27 na 28 Julai, ambapo alikutana na maafisa waandamizi wa jeshi na kufungua mazoezi ya kwanza ya pamoja ya kijeshi ya nchi hizi mbili toka mwaka 2017...
wanataka kuleta military base kama kule somalia na Uganda
 
Ilianza kuonekana ndege imekaa tuu pale uwanja wa ndege taarifa ikatoka inaleta vifaa vya ubalozi wiki chache baadae tunaskia Tanzania imepokea msaada wa chanjo kutoka marekani chanjo imefika tuu ghafla marekani anafanya mazoezi ya pamoja na. Majeshi yetu naweza nikawa na akili fupi kwa mitazamo ya wengi lakini kwa akili ndogo tuu naiona shida kubwa sana mbeleni ninahofu na dunia ya wakati ujao zile movie za ma vampire nadhani ni wakati wa mabadiriko ya mwanadamu
Siku ile tulipo hoji juu ya hiyo ndege kukaa pale uwanjani jioni yake ikaongezeka ingine 1 nawa lipakua mzigo na kupata escort ya polisi wetu bila ya kujua wamebeba nini.
 
Tukijadili hili swala kwa maslahi ya taifa tufikirie kuhusu kesho yetu. Tusidhani tuko salama sana.

Nachokiona ni kutaka kuuza nchi kwa maslahi y na tamaa za madaraka.
Marekani wakiamua mtawala wa nchi fulani atawale milele bila vurugu inawezekana. Aliweza kuigeuza Saudu Arabia kuwa ya kifalme wakati ilikuwa na utaratibu mwingine wa kiutawala.

Kwa tabia za hawa marais wa nchi zetu pale wanapoona tishio ktk uongozi wao wako tayari kuweka nchi rehani ili wasaidiwe ulinzi na mataifa yenye nguvu. hilo kwa nchi ya USA, Ufaransa na Urusi wako vizuri sana.

Ktk nchi zote duniani ambako Marekani kwa visingizio vya udumavu au tishio la usalama waliingiza vikosi vyao vya kijeshi( US miltary bases) nchi hizo hazikubaki salama hadi leo hazijatengamaa.

Mifano iko mingi michachi ni kama Somalia, Afighanistan, Uganda na Ethiopia.

Maeneo mengi waliingia kwa sababu za kupambana na ugaidi. Hadi leo nchi hizo hazitawaliki, hazina amani, ugaidi na uharifu wa kibinadamu na rasilimali umeongezeka mara dufu.

Tangu habari za Mboww kukamatwa kwa movie ya Ugaidi tunaona Mabeberu wakimiminika nchini. Kibachonishtua ni hawa makamanda wa AFCOM.

Je mama anataka kuweka rehani nchi ili wale maadui wa ndani wasimzingue? je tutasalimika??
 
Marekani wako more “strategically”. Sasahivi, maadui wake wakubwa ambao ameamuwa kupambana nao ni mchina na mrusi. Vita vya ugaidi wameachana navyo. Maana ndivyo viliwa keep busy mchina na mrusi wakawa wanaendelea kujikita na kujinafasi ulimwenguni kote.

Kuondoka Afghanistan na Iraqi ni uthibitisho tosha kuwa sasa wamehamisha na kubadili mwelekeo kukabiliana na warusi na wachina. Haufuatilii mikwaruzo kwenye China seas na Black Sea respectively?
 
Marekani wako more “strategically”. Sasahivi, maadui wake wakubwa ambao ameamuwa kupambana nao ni mchina na mrusi. Vita vya ugaidi wameachana navyo. Maana ndivyo viliwa keep busy mchina na mrusi wakawa wanaendelea kujitakia na kujinafasi ulimwenguni kote.

Kuondoka Afghanistan na Iraqi ni uthibitisho tosha kuwa sasa wamehamisha na kubadili mwelekeo kukabiliana na warusi na wachina. Haifuatilii mikwaruzo kwenye China seas na Black Sea respectively?
lakini ndio kusema wameachana na harakati za kulinda haki, uhuru na demokrasia duniani?
 
Back
Top Bottom