Mkuu wa jumuia ya nchi za kiarabu anasema wamepoteza imani kwa Marekani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279

Jumuiya ya nchi za kiarabu inatilia shaka nafasi ya Marekani kama mpatanishi katika mzozo wa mashariki ya kati.

Uamuzi wa Marekani kuitambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel "unazusha suala kuhusiana na mchango wake na jukumu lake katika kuimarisha utulivu na amani katika eneo hilo, amesema hayo katibu mkuu wa jumuia ya nchi za kiarabu, Ahmed Abu Gheith, katika mkutano wa dharura wa jumuia hiyo mjini Cairo.

Mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa jumuia ya nchi za kiarabu wameitolea wito Marekani ibatilishe uamuzi huo.Tangazo la rais wa Marekani Donald Trump "linavunja vibaya sana sheria za kimataifa".Wamesema mawaziri wa nchi za nje wa jumuia ya nchi za kiarabu.


DW
 
Kabisa Mkuu, pamoja na utajiri wao mkubwa sana lakini hawana umoja na huo udhaifu jamaa wanautumia vizuri sana kwa faida yao.

Divide and rule imeshawadhofisha hao wanajumuiya maana hata wao wenyewe wana migogoro na hawaelewani kiasi cha kuungana na kutetea mji wa Jerusalemu.

Yetu macho.
 
Kwani asipomwamini hilo litamcost vipi Donald Trump ?

Kwani hayo malalamiko yatawaathiri vipi Wamarekani na Waisrael ?
 
Saudia na Misri wameshawekwa sawa na Trump, kilichobaki ni lip-service tu kuwazuga wananchi wao kuwa wamechukia kumbe behind the scene hao watawala wameshakubaliana deal!
 
Wadau mm kwa hili naungana na msimamo wa nchi yangu, na pia naungana na waarabu kulaani kitendo cha huyu rais. Kwa uamzi huo anachochea mauaji mkubwa kwenye hii nchi. Tukumbuke ile ni ardhi ya wapalestina na sio wayahudi. So trump ni myahudi na ndo maana kapendelea ndugu zake
 
Back
Top Bottom