Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Ernest Mangu awavisha nishani ya ARPCCOS Omari Mahita na Saidi Mwema

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
13680882_941092366001738_5325607477656018720_n.jpg

Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Ernest Mangu akimvisha nishani IGP mstaafu Omari Mahita, nishani ya Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa Nchi za Kusini mwa Afrika (ARPCCOS) kwa kuwa IGP wa kwanza Tanzania kuwa mwenyekiti wa shirikisho hilo na kuliletea sifa Jeshi la Polisi Tanzania kimataifa. IGP Mangu amemvisha nishani kwa niaba ya Mwenyekiti wa shirikisho hilo wa sasa. Tukio lilifanyika jana katika chuo cha taaluma ya Polisi Dar es Salaam
13718527_941091799335128_3365197063581915686_n.jpg

Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Ernest Mangu akimvisha nishani IGP mstaafu Saidi Mwema, nishani ya Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SARPCCO) kwa kuwahi kuwa mwenyekiti wa shirikisho hilo na kuliletea sifa Jeshi la Polisi Tanzania kimataifa. IGP Mangu amemvisha nishani kwa niaba ya mwenyekiti wa shirikisho hilo wa sasa. Tukio lilifanyika jana katika chuo cha taaluma ya Polisi Dar es Salaam. Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.
 
Nitawalinda wastaafu wote_na kubeba mizigo yao" Lugumi haiwezi kuguswa kamwe!
 
Nikimuona mahita nakumbuka mauaji ya zanzibar na wakimbizi kutoka Tanzania waliokimbilia kakuma Kenya, pia nakumbuka binti wa kazi wa mahita aliyezaa na mahita na manyanyaso aliyopata yule binti mpaka suala lile likaamuliwa mahakamani
 
Nikimuona mahita nakumbuka mauaji ya zanzibar na wakimbizi kutoka Tanzania waliokimbilia kakuma Kenya, pia nakumbuka binti wa kazi wa mahita aliyezaa na mahita na manyanyaso aliyopata yule binti mpaka suala lile likaamuliwa mahakamani
Ukishakumbuka what next?
 
Back
Top Bottom