Mkuu mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro alitabiriwa na Mzee Ndesamburo asema Mbunge Lucy Owenya

tramadol

JF-Expert Member
Oct 10, 2015
5,383
4,317
Mama Anna Mghwira Mkuu mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro aitembelea familia ya Ndesamburo na kutoa pole kwa wafia kwa kusaini kitabu cha maombolezo alipowasili mkoani hapo kuanzia kazi baada ya kuapishwa.

Katika maongezi yake na wana familia ndipo Mbunge wa viti maalum ambaye ni mtoto wa Marehemu Ndesamburo, Mh Lucy Owenya alipomwambia Mh Anna Mghwira kuwa hata mzee Ndesamburo ktk uhai aliwahi kusema kuwa kuna siku atateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa tena wa Kilimanjaro.

Maneno ya wazee huwa hayapiti hivi hivi tu bila kutimia mara nyingi.

Chanzo: Tanzania Daima

Sijui hapa Mzee Ndesamburo aliona nini na kwanini aliongea maneno hayo kuhusu Mh Anna Mghwira!
 
hujui hata ulichoandika....... Lucy Owenya ni mkwe wa marehemu Ndesa?? unapotunga story jaribu hata kuweka angalau kaukweli kwa asilimia 0.000001
 
Mama Anna Mghirwa Mkuu mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro aitembelea familia ya Ndesamburo na kutoa pole kwa wafia kwa kusaini kitabu cha maombolezo alipowasili mkoani hapo kuanzia kazi baada ya kuapishwa.

Katika maongezi yake na wana familia ndipo Mbunge wa vitu maalumu ambaye ni mtoto wa Marehemu Ndesamburo Mh Lucy Owenya alipomwambia Mh Anna Mghirwa kuwa hata mzee Ndesamburo ktk uhai aliwahi kusema kuwa Kuna siku atateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa tena wa Kilimanjaro.

Maneno ya wazee huwa hayapiti hivi hivi tu bila kutumia Mara nyingi.

Sijui hapa Mzee Ndesamburo aliona nini na kwanini aliongea maneno hayo kuhusu Mh Anna Mghirwa!!
Aibuu mkuu....ukiwa muongo sharti ujue kile unachodanganya...sasa ona
ulivyoumbuka..
 
Aibuu mkuu....ukiwa muongo sharti ujue kile unachodanganya...sasa ona
ulivyoumbuka..
Hakuna kudanganywa ktk hiyo story ni taarifa sahihi.Bajeti ya jana imenichanganya Kuna kipengele kimoja kimenibana sana.
 
Back
Top Bottom