"Mkuu" anaingilika labda washauri wamejijengea uoga au kutokujiamini

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Binafsi nadhani "mkuu" kabisa anaingilika na anashaurika vizuri tu.

Tatizo lipo kwenye mazoea ya ushauri waliyonayo washauri kwa maana ya wale wanaoteuliwa kumsaidia kwenye wizara mbalimbali.

Mshauri anapozoea kushauri kisiasa kwa nia ya kumpamba yule anayemshauri basi upo uwezekano wa kujikuta anaishi kama mpambe badala ya mshauri kwa maana ya msaidizi mkuu wa utekelezaji wa sera na mambo nyeti ya kitaifa.

Nimegundua kuwa "mkuu" anapenda zaidi substance kwenye ushauri wa mtu zaidi ya blah blah za kisiasa, hataki upambe anataka ushauri ili na yeye aweze kutoa maagizo kutokana na upana wa ushauri anaopewa.

Anaweza kuwa na udhaifu kwa maana ya wakati mwingine uwepo wa jazba, lakini anasikiliza zaidi ujazo wa hoja ya mtoa hoja na sio tabia ya kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa.

Wasaidizi wake wanao mtihani wa kujifunza kuwa na tabia ya kujiamini wakati wanapowakilisha hoja, wengi ndio zile shahada za uzamivu hivyo ni lazima waijue sanaa wa uwakilishaji wa hoja zao.

Mshauri wa "mkuu" kabisa ambaye unaamini katika uwezo wako na elimu yako kwanini ushindwe kuwa na ushawishi wakati unawakilisha hoja zako?.

Naamini washauri watakuwa wameshajifunza kitu fulani ndani ya huu mwaka wa kwanza wa awamu ya tano.
 
Walilalamika Mh. Kikwete alikuwa dhaifu mtu wa kuchekacheka. Mungu si Athuman akatupatia mtu asiyechekacheka bado wanalalamika.

Hii inanikumbusha kisa cha Mussa na wana wa Israel. Vyovyote iwavyo tutafika nchi ya ahadi. Tufunge mikanda na tuwe wavumilivu.

[HASHTAG]#HapaKaziTu[/HASHTAG].
 
Walilalamika Mh. Kikwete alikuwa dhaifu mtu wa kuchekacheka. Mungu si Athuman akatupatia mtu asiyechekacheka bado wanalalamika.

Hii inanikumbusha kisa cha Mussa na wana wa Israel. Vyovyote iwavyo tutafika nchi ya ahadi. Tufunge mikanda na tuwe wavumilivu.

[HASHTAG]#HapaKaziTu[/HASHTAG].
Ni kweli kabisa mkuu, safari lazima iendelee iwe tunampenda dereva au hatumpendi, gari haliwezi kulala porini lazima lifike mjini.
 
Ni kweli mkuu anashaurika lakini ni kwa yale anayopenda kusikia yeye. Inawezekana ni udhaifu wake kibinadamu, pata picha unamshauri kitu asichopenda hata kama ni ukweli unadhani atakupa nafasi? Ndio maana unaona kuna lile suala la mkuu wa wilaya kuwatoa wananchi kwenye eneo rais alilotangaza rais wapewe wananchi. Hapa unajaribu kutoa hisia zako na sio uhalisia.
 
Tatizo watanzania niwasahaulifu mno
Watu walilia mtu asiye yumbishwa
Wala kuchelewa kutoa maamuzi,
Huyu siyo dhaifu kama walivyo zoea kusema
Huyu ni Jembe la kazi
Hana Wikend wala diku ya kazi,
Yeye ni Watanzania na Tanzania kwanza.
 
Ni kweli mkuu anashaurika lakini ni kwa yale anayopenda kusikia yeye. Inawezekana ni udhaifu wake kibinadamu, pata picha unamshauri kitu asichopenda hata kama ni ukweli unadhani atakupa nafasi? Ndio maana unaona kuna lile suala la mkuu wa wilaya kuwatoa wananchi kwenye eneo rais alilotangaza rais wapewe wananchi. Hapa unajaribu kutoa hisia zako na sio uhalisia.
Mkuu suala la mkuu wa wilaya ni mmojawapo wa masuala mengi ambayo yananukuliwa au kueleweka vibaya.

Ujumbe ni kwamba wafanyabiashara wahamie kwenye maeneo yao baada ya uongozi wa wilaya kujihakikishia kwamba mahali tayari panafaa kwa ajili ya biashara.
Zipo issues nyingine zisizoandikika hapa, ambazo mkuu amekutana na ushauri uliokwenda shule na akalielewa somo vizuri sana.
 
Mkuu suala la mkuu wa wilaya ni mmojawapo wa masuala mengi ambayo yananukuliwa au kueleweka vibaya.

Ujumbe ni kwamba wafanyabiashara wahamie kwenye maeneo yao baada ya uongozi wa wilaya kujihakikishia kwamba mahali tayari panafaa kwa ajili ya biashara.
Zipo issues nyingine zisizoandikika hapa, ambazo mkuu amekutana na ushauri uliokwenda shule na akalielewa somo vizuri sana.

Mkuu hizo ni hekaya, ni zipi hizo zisizoandikika? Halafu siku hizi kumekuwa sana na hako kamsemo ka kunukuu vibaya. Ni kweli watu wanaelewa au kunukuu vibaya kwa hivyo? Ni hivi, rais ni mtendaji mzuri ila aliyeweka itikadi za chama mbele, ndio maana anashauriwa na watu wenye nidhamu za woga na unafiki. Wachache wanaothubutu kumwambia ukweli asiopenda anawapa hard time mpaka inabidi wampotezee.
 
  • Thanks
Reactions: 999
Mkuu hizo ni hekaya, ni zipi hizo zisizoandikika? Halafu siku hizi kumekuwa sana na hako kamsemo ka kunukuu vibaya. Ni kweli watu wanaelewa au kunukuu vibaya kwa hivyo? Ni hivi, rais ni mtendaji mzuri ila aliyeweka itikadi za chama mbele, ndio maana anashauriwa na watu wenye nidhamu za woga na unafiki. Wachache wanaothubutu kumwambia ukweli asiopenda anawapa hard time mpaka inabidi wampotezee.
Kwanini uwe ni ukweli asiopenda?, halafu ukweli asioupenda unawezaje kutoka kwa mtu ambaye amemteua yeye mwenyewe aje kumsaidia.

Mkuu wapo wakuu wa mamlaka ambao mkuu akisikiliza ushauri wao wa kitaalam unaotolewa bila ya uoga, huwa anakubaliana nao mia kwa mia. Suala ni kujiamini kwa mtoa ushauri na sio mtoa ushauri asiyejiamini anatoa ushauri kwa wasiwasi halafu kisingizio chake eti mkuu ni mbabe.

Kama substance unayo na unacho kiburi cha elimu yako kwanini uongee kwa wasiwasi?.
 
Kwanini uwe ni ukweli asiopenda?, halafu ukweli asioupenda unawezaje kutoka kwa mtu ambaye amemteua yeye mwenyewe aje kumsaidia.

Mkuu wapo wakuu wa mamlaka ambao mkuu akisikiliza ushauri wao wa kitaalam unaotolewa bila ya uoga, huwa anakubaliana nao mia kwa mia. Suala ni kujiamini kwa mtoa ushauri na sio mtoa ushauri asiyejiamini anatoa ushauri kwa wasiwasi halafu kisingizio chake eti mkuu ni mbabe.

Kama substance unayo na unacho kiburi cha elimu yako kwanini uongee kwa wasiwasi?.

Mkuu elimu itakusaidia nini kwenye nchi hii. Nchi hii maisha yako yatanyooka iwapo una cheo mahali, hivyo hata kama una ukweli ambao utahatarisha cheo chako, lazima utaufyata mkia. Kama unadhani elimu ni mali kwanini hao wenye elimu wanaenda kwa waganga ili kupata madaraka, na wakifukuzwa kazi wanalia. Unamkumbuka yule mkuu wa mkoa aliyelia na kuomba asemehewa kisa ana familia kubwa inayomtegemea? Mbona hakufarahi na kusema ana elimu ataenda kujiajiri kama alivyokuwa akihimiza wengine alipokuwa madarakani?
 
  • Thanks
Reactions: 999
Mkuu elimu itakusaidia nini kwenye nchi hii. Nchi hii maisha yako yatanyooka iwapo una cheo mahali, hivyo hata kama una ukweli ambao utahatarisha cheo chako, lazima utaufyata mkia. Kama unadhani elimu ni mali kwanini hao wenye elimu wanaenda kwa waganga ili kupata madaraka, na wakifukuzwa kazi wanalia. Unamkumbuka yule mkuu wa mkoa aliyelia na kuomba asemehewa kisa ana familia kubwa inayomtegemea? Mbona hakufarahi na kusema ana elimu ataenda kujiajiri kama alivyokuwa akihimiza wengine alipokuwa madarakani?
Mkuu kila mtu anapitia kwenye makuzi yake, jinsi nilivyokuzwa mimi sivyo ulivyokuzwa wewe.

Ni kosa kutumia historia ya maisha ya mtu mmoja kwa kupima mafanikio au kuanguka kwa mtu mwingine.

Maisha huenda yakibadilika, usitegemee kumuona mtoto anayekuzwa leo hii akija kuwa na hulka sawasawa na zile zilizotukuza sisi wakati atakapoanza harakati za kuanza maisha.

Viongozi wenye wajibu wa kumshauri mkuu wa taifa wanayo kila sababu ya kujiamini wakati wanapofanya kazi yao. Vinginevyo upambe utawavunjia heshima na kuzikwaza juhudi za mkuu katika kubadilisha hali ya maisha ya watanzania.
 
Tatizo la wasukuma kwa sasa mnaamini Magufuli ni Mungu, hana anachokosea, wanaokosea ni washauri wake na watendaji...

Jana kuna mtu aliumwa na mbwa wakati wanahangaika kupata ile sindano ya mbwa ikaonekana madawa ya rabies ni mojawapo wa yale madawa yaliyoadimika na serikali ya anayeshaurika imeshindwa kuagiza madawa. Sina hakika kama yule mtoto wa watu maskini ya Mungu atapona. Madawa hakuna wajameni
 
  • Thanks
Reactions: 999
Tatizo la wasukuma kwa sasa mnaamini Magufuli ni Mungu, hana anachokosea, wanaokosea ni washauri wake na watendaji...

Jana kuna mtu aliumwa na mbwa wakati wanahangaika kupata ile sindano ya mbwa ikaonekana madawa ya rabies ni mojawapo wa yale madawa yaliyoadimika na serikali ya anayeshaurika imeshindwa kuagiza madawa. Sina hakika kama yule mtoto wa watu maskini ya Mungu atapona. Madawa hakuna wajameni
Mkuu punguza ukabila ili unachokiongea kiweze kuwa relevant katika dunia ya sasa.

Pia jitahidi uondokane na akili za lawama kwamba serikali ndio kila kitu. Wewe pia ni sehemu ya serikali, upeo wako, fikra zako, ni sehemu ya maamuzi ya serikali.
 
Tatizo watanzania niwasahaulifu mno
Watu walilia mtu asiye yumbishwa
Wala kuchelewa kutoa maamuzi,
Huyu siyo dhaifu kama walivyo zoea kusema
Huyu ni Jembe la kazi
Hana Wikend wala diku ya kazi,
Yeye ni Watanzania na Tanzania kwanza.
OK, sasa yuko hivyo mbona mnashindwa kumshauri? Mnamuogopa badala ya kumheshimu? Kiongozi wa nchi awaye yeyote anahitaji timu nzuri ya ushauri kwa kila nyanja ili afanikiwe. Sasa nyie kwa tabia zenu za kinafiki mnashindwa kumshauri ndio maana maamuzi mengi ni lawama tuu.
Madume unayakuta yamejipanga kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa badala kushauri. Unafiki tuu ndio wanaweza.
Magu bora kipigo angekielekeza kwa mawaziri wake kuliko Kule kwa nanihii
 
Tatizo la wasukuma kwa sasa mnaamini Magufuli ni Mungu, hana anachokosea, wanaokosea ni washauri wake na watendaji...

Jana kuna mtu aliumwa na mbwa wakati wanahangaika kupata ile sindano ya mbwa ikaonekana madawa ya rabies ni mojawapo wa yale madawa yaliyoadimika na serikali ya anayeshaurika imeshindwa kuagiza madawa. Sina hakika kama yule mtoto wa watu maskini ya Mungu atapona. Madawa hakuna wajameni
kuikuta aunt rabies gov hospitals ni neema other wise no kununua tuuuu na doz c chini ya 100,000/= huku kwetu
 
OK, sasa yuko hivyo mbona mnashindwa kumshauri? Mnamuogopa badala ya kumheshimu? Kiongozi wa nchi awaye yeyote anahitaji timu nzuri ya ushauri kwa kila nyanja ili afanikiwe. Sasa nyie kwa tabia zenu za kinafiki mnashindwa kumshauri ndio maana maamuzi mengi ni lawama tuu.
Madume unayakuta yamejipanga kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa badala kushauri. Unafiki tuu ndio wanaweza.
Magu bora kipigo angekielekeza kwa mawaziri wake kuliko Kule kwa nanihii
Usinge kuwa mnafiki
Ungeanza wewe kumshauri Mbowe asiuze Chagadema kwa Lifisadi
 
Kwanini uwe ni ukweli asiopenda?, halafu ukweli asioupenda unawezaje kutoka kwa mtu ambaye amemteua yeye mwenyewe aje kumsaidia.

Mkuu wapo wakuu wa mamlaka ambao mkuu akisikiliza ushauri wao wa kitaalam unaotolewa bila ya uoga, huwa anakubaliana nao mia kwa mia. Suala ni kujiamini kwa mtoa ushauri na sio mtoa ushauri asiyejiamini anatoa ushauri kwa wasiwasi halafu kisingizio chake eti mkuu ni mbabe.

Kama substance unayo na unacho kiburi cha elimu yako kwanini uongee kwa wasiwasi?.
Ungekuwa unajadili kwa kutuwekea mifano, pengine ungeweza kueleweka, hapa inaonekana unajadili hisia zako tu!
 
Usinge kuwa mnafiki
Ungeanza wewe kumshauri Mbowe asiuze Chagadema kwa Lifisadi
Chadema sio mama au baba yangu ila Tanzania ndio mambo yote kwangu. Leo nikiona Chadema hatuendani naiachilia mbali na kuwa chama chochote chenye kuendana na mawazo yangu lakini sio ccm.
Wewe unadhani kwa akili yako Mbowe angekuwa ana uwezo wa kuuza chama kuna watu makini kibao ndani ya Chadema nikiwapo mimi wangekubali kuendelea kuwapo humo? Hizo ni ngonjera zenu vuvuzela wa ccm baada ya kushindwa kuwa na hoja.
Back to the point Magufuli ni Rais kutokea chama chenu, mshaurini sio kumsifia kama mazuzu, hata yeye naona sasa ameshtuka kuwa sifa zenu ni za kijinga na akiharibikiwa mtamgeuka kama JK hivyo kaanza kuwatumbua ndani ya chama
 
Umekazana ooh Chadema mbowe kauza nenda kamuulize Makonda style yakujikomba ikoje maana unawashwa sana wew Dada!
 
Back
Top Bottom