nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Monday, 26 September 2011 20:51 |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Aziza Masoud RAIS Jakaya Kikwete anatarajiwa kufungua mkutano wa uwekezaji kwa Kanda ya Ziwa Tanganyika unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao. Mkutano huo wa siku nne utafanyika Oktoba 17 katika Mji wa Mpanda utahusisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma utaanza rasmi Oktoba 15 mpaka 18 mwaka huu ambao utaambatana na maonyesho ya vivutio mbalimbali vilivyopo katika ukanda huo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya alisema kuwa lengo la mkutano huo ni kuonyesha vivutio vilivyopo katika ukanda huo pamoja na mafanikio yaliyopatikana kwa wale walioanza kuwekeza. Watu watapata fursa ya kutembelea mabanda ya maonyesho katika eneo la mkutano yenye lengo la kuonyesha vivutio mbalimbali vilivyopo katika ukanda huu na mafanikio yaliyopatikana kwa wale walioanza kuwekeza, alisema Manyanya. Alisema kuwa sababu ya kufanya mkutano kwa ushirikiano wa mikoa hiyo mitatu ni kufanana kwa mazingira ya kijiografia ya mikoa hiyo katika sekta nyingi. Pia mikoa yote mitatu ipo pembezoni huku ikipakana na Ziwa Tanganyika na nchi za Zambia, Kongo, Rwanda na Burundi pamoja na kufanana kwa mila na desturi zao. Manyanya pia aliwataka wananchi kuwa wazalendo na kuwekeza katika mkoa huo kutokana na kuwa na vivutio vingi na kuacha fikra za nchi kuwekezwa na watu kutoka nje ya nchi. |