Mkutano wa SADC: Hongera kwa Uhamasishaji, Watanzania Tumehamasika Tusiishie Kuhamasikia Mkutano Tuu Tukashindwa kuchangamkia fursa za Soko la SADC

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,443
113,452
Wanabodi,

Leo nimepata tena fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo natoa angalizo kuhusu kuchangamkia fursa za Mkutano wa SADC na Maonyesho ya SADC, kwanza kwa vile maonyesho haya ya SADC, yamegongana na maonyesho ya Nane Nane ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Simiyu, ombi langu la kwanza ni tusiache mbachao kwa msala upitao, Maonyesho ya Nane Nane ni mbachao, Maonyesho ya SADC ni msala upitao, uhamasishaji wa maonyesho ya SADC, pia uende sambamba na uhamasishaji maonyesho ya Nane Nane, maana kwa sisi huku Nyakabindi Simiyu, zaidi ya kuzinduliwa na Makamo wa rais Mhe. Samia Suluhu, nimewaona mawaziri wawili tuu, na manaibu wawili, inamaana wengine wote ni SADC?.

Hoja yangu kuu katika bandiko hili ni kwanza kutoa pongezi kwa kazi kubwa na kazi nzuri inayofanywa kuhamasisha mkutano huu wa SADC ambao umerudi tena kufanyika nchini Tanzania baada ya miaka 16. Kiukweli uhamasishaji ni mkubwa, na Watanzania tumehamasika, na kila kada kujipanga kuchangamkia fursa za mkutano huu, kitu muhimu kuliko hata kuchangamkia fursa ni sisi Watanzania na Tanzania yetu kama nchi, inachangamkia vipi fursa za soko la SADC lenye watu milioni 450?.

Pia naomba kutoa angalizo muhimu kwa viongozi wetu, kuhusu conference tourism katika kuwapatia wafanyabiashara fursa za mkutano huu, naombeni sana msiwape too much expectations wengine wakakopa kwa kutegemea zitarudi, hili ninilishuhudia kwenye mkutano wa Sullivan, ulikuwa ni mkutano wa fursa, wakazi wa Arusha wakajitoa kwelikweli, mwisho wa siku kuna wafanyabiashara waliishia kulia na kujuta, haswa kwa kuzingatia hii mikutano ya ngozi nyeusi ni tofauti na mikutano ya ngozi nyeupe, targets ya ngozi nyeusi ni save, save save, wakati ngozi nyeupe ni spend spend spend. Sikubahatika kupata mrejesho wowote ni fursa zipi za Sullivan, Tanzania tulifanikiwa kuzipata.

Mimi nilipata bahati ya kuwemo kwenye kundi la waandishi wa habari wa Tanzania, waliopelekwa nchini Marekani kuelimishwa kuhusu fursa za soko la AGOA. Shirika la misaada la watu wa Marekani USAID wakagharimia viongozi wa wizara ya Viwanda na Biashara, viongozi wa BET (sasa Tantrade), na viongozi wa vyama vya vya wafabiashara mtambuka chini ya TCCIA, CTI na kundi kubwa la wafanyabiashara zaidi ya 100, kwenda nchini Marekani kuonyeshwa bidhaa zinazotakiwa ili kuchangamkia fursa za soko la AGOA.

Kule tulionyeshwa soko la Marekani linataka bidhaa gani, zenye ubora gani, viwango gani, ufungashaji gani na taratibu za kufuata, soko hilo ni kubwa na linahitaji bidhaa nyingi za kila aina zaidi ya 1000 kutoka Tanzania zikiwemo bidhaa za kiutamaduni, vinyago, mapambo, maua.

Wamarekani wakafanya hivyo hivyo kwa Kenya, Uganda, Ghana, Rwanda na Burundi na nchi mbalimbali.

Kilichofuatia ziara hiyo, wafanyabishara wa Tanzania, wakahamasika sana, na waliporejea tuu nyumbani Tanzania, orders zikaanza kumiminika. Kuna kikundi cha akinamama wasuka mikeka ya majani, wakapewa order ya kupeleka 40ft contena la mikeka hiyo inayosukwa akinamama wa vijijini mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Wakinamama wale na kikundi chao, walitembea na hiyo order wakitafuta mtaji wa kuitekeleza hadi ika expire. Ukishindwa ku deliver order ndani ya siku 90, order ina expire, sasa inakuwa wazi kwa kila mwenye uwezo, yaani an open order.

Baada ya siku 90 kupita kwa Tanzania kushindwa kudeliver, makampuni ya jirani zetu Kenya, walikuja nchini, wakaenda Pwani, Lindi na Mtwara wakawalipa wale wamama na kuinunua mikeka yote kwa bei ya karibu na bure na kuisafirisha hadi Nairobi, wakaipakia kwenye makontena na kuifikisha sokoni Marekani, mikeka yenye certificate of origin ya Tanzania, lakini imeingizwa sokoni na Wakenya, huku sisi Watanzania tumelala. Hivi ndivyo inavyofanyika kwa vinyago vyetu, madini yetu, mazao yetu.

Huu ni mfano mmoja tuu wa jinsi sisi Watanzania tunashindwa kuchangamkia fursa za masoko, hadi AGOA ya awamu ya kwanza ya kipindi cha miaka 10 kimepita, Tanzania tumeshindwa kabisa kutumia kikamilifu fursa hizo, huku jirani zetu wakijivinjari kwa kuzinunua bidhaa zetu na wao ndio wanazifikisha sokoni. Sasa AGOA imeongeza miaka 10 mingine, na bado sisi Tanzania kama nchi, bado hatujaweza kuchangamkia fursa za soko la AGOA.

Hali ni hivyo hivyo kwa soko la Afrika Mashariki, Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa fursa za kila kitu, ndio nchi inayoongoza kwa utajiri wa kila kitu, kuanzia vivutio vya utalii, maliasili, madini, vyanzo vya maji, ardhi ya kutosha kwa kilimo, udongo wenye rutuba, na sasa tuna gesi asili na soon tutagundua mafuta.

Tanzania tunapakana na nchi 8, kati ya hizo, nchi 6 ni land locked, zisizo na bahari, hivyo sekta tuu ya usafiri na usafirishaji ingeweza kututoa kimasomaso toka kwenye lindi hili la umasikini uliotopea, lakini sivyo. Kufuatia Tanzania kuwa na bandari ya Dar es Salaam, Kariakoo ilikuwa kitovu cha biashara ya bidhaa kwa nchi za Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi na DRC, lakini sasa, mzingo unashukia bandari ya Dar, unasafirishwa kwenda Uganda, halafu wafanyabishara wa nchi hizo sasa wananunulia Uganda. Hivyo Tanzania tuna kila sababu ya kuwa ni nchi tajiri sana kwa kuchangamkia tuu fursa, lakini hali sii hivyo, bado tunaendelea na umasikini tulionao, ukijiuliza kwanini Tanzania ni masikini, huwezi kupata jibu sahihi.

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema “umasikini mkubwa zaidi na umasikini mbaya zaidi ni umasikini wa fikra”, fikra ni kama kauli, huumba, ukijifikiria kuwa wewe ni masikini, ni kweli unakuwa masikini kweli, ndio maana msimamo wa Rais Magufuli na kauli yake kuwa Tanzania sio masikini bali ni nchi tajiri na tunakwenda kuwa a donor country , inapaswa kuungwa mkono na watu wote wenye mapenzi mema na nchi yetu Tanzania yetu, tuache kabisa kujiita masikini tukajikuta tunajiumbia umasikini, tuanze kujiita Tanzania ni nchi tajiri ili kujiumbia utajiri.

Nikiangalia kiwango cha uhamashaji mkutano huu na nguvu inayotumika kuuhamashisha mkutano huu, tukiitumia katika kuhamashisha kuchangamkia soko la SADC, uhamasishaji huo utakuwa na manufaa ya muda mrefu zaidi baada ya mkutano kumalizika.

Kinachofanya jirani zetu Wakenya, watushinde kwenye kuchangamkia fursa ni serikali yao kuingiza mkono wake kusaidia, hivyo sasa serikali awamu ya tano imeishaonyesha njia, kwanza kwa rais Magufuli kukaa na wafanyabiashara na kusikiliza kero zao ikiwemo kuchukua hatua za papo kwa papo. Bila mkono wa serikali katika kuweka mazingira wezeshi, wafanyabiashara wenyewe tuu kama wafanyabiashara, hatutaweza kuliteka soko la SADC lenye watu milioni 450, kama hili soko tuu la Africa Mashariki, Tanzania bado!, kwa sasa wanunuzi wakubwa wa mazao yetu ni jirani zetu na sio sisi.

Nawatakia maonyesho mema ya SADC na pia Nane Nane njema.

Paskali
 
Pamoja na kuihitaji serikali kutia mkono katika kuchangamkia fursa,lakini bado hata sisi wenyewe tumekuwa stagnant sana kuchangamkia fursa husika

Tulio wengi tunataka vitu vigumu vifanywe na wengine then sisi tuambiwe mavuno tayari ndiyo tuchangamkie,lakini utayari wa kuanza vitu vigumu ni mdogo sana!

Mfano mzuri ni huu,nimepita maeneo mengi yenye mabonde very productive(kilombero,Ukanda wa ziwa Rukwa,Mbarali) ni mabonde yenye rutuba ya hatari,lakini hatuyatumii ipasavyo kwa kisingizio kwamba serikali haijatusaidia kuweza kuyalima,unajiuliza wewe uwezo wako ku-explore hiyo fursa kabla kuomba support ya serikali ni kiasi gani mtu anatoa macho tu!

Anakuja mgeni kutoka duniani kwa jasho na damu,anaamua kuwekeza anapata mavuno yenye faida kubwa sana,anaondoka na utajiri wakati sisi tunaishia kushangaa shangaa na kuilalamikia serikali!

Tunahitaji mabadiliko makubwa sana kifikra kuweza kuchangamkia fursa za ndani na nje ya nchi!
Pascal Mayalla
 
Wanabodi,
leo nimepata tena fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nauzungumzia Maonyesho ya SADC, kwanza kwa vile maonyesho haya ya SADC, yamegongana na maonyesho ya Nane Nane ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Simiyu, ombi langu la kwanza ni tusiache mbachao kwa msala upitao, Maonyesho ya Nane Nane ni mbachao, Maonyesho ya SADC ni msala upitao, uhamasishaji wa maonyesho ya SADC, pia uende sambamba na maonyesho ya Nane Nane.

Hoja yangu kuu katika bandiko hili ni kwanza kutoa pongezi kwa kazi kubwa na kazi nzuri inayofanywa kuhamasisha mkutano huu wa SADC ambao umerudi tena kufanyika nchini Tanzania baada ya miaka 16. Kiukweli uhamasishaji ni mkubwa, na Watanzania tumehamasika, na kila kada kujipanga kuchangamkia fursa za mkutano huu, kitu muhimu kuliko hata kuchangamkia fursa ni sisi Watanzania na Tanzania yetu kama nchi, inachangamkia vipi fursa za soko la SADC lenye watu milioni 450?.

Pia naomba kutoa angalizo muhimu kwa viongozi wetu, katika kuwapatia wafanyabiashara fursa za mkutano huu, naombeni sana msiwape too much expectations wengine wakakopa kwa kutegemea zitarudi, hili ninilishuhudia kwenye mkutano wa Sullivan, ulikuwa ni mkutano wa fursa, wakazi wa Arusha wakajitoa kwelikweli, mwisho wa siku kuna wafanyabiashara waliishia kujuta, na sikubahatika kupata mrejesho wowote ni fursa zipi za Sullivan, Tanzania tulifanikiwa kuzipata.

Mimi nilipata bahati ya kuwemo kwenye kundi la waandishi wa habari wa Tanzania, waliopelekwa nchini Marekani kuelimishwa kuhusu fursa za soko la AGOA. Shirika la misaada la watu wa Marekani USAID wakagharimia viongozi wa wizara ya viwanda na biashara, viongozi wa BET (sasa Tantrade, na viongozi wa vyama vya vya wafabiashara mtambuka chini ya TCCIA, CTI na kundi kubwa la wafanyabiashara zaidi ya 100, kwenda nchini Marekani kuonyeshwa fursa za AGOA.

Kule tulionyeshwa soko la Marekani linataka bidhaa gani, zenye ubora gani, viwango gani, ufungashaji gani na taratibu za kufuata, soko hilo ni kubwa na linahitaji bidhaa zaidi ya 1000 kutoka Tanzania zikiwemo bidhaa za kiutamaduni, vinyago, mapambo, maua.

Wamarekani wakafanya hivyo hivyo kwa Kenya, Uganda, Ghana, Rwanda na Burundi na nchi mbalimbali.

Kilichofuatia ziara hiyo, wafanyabishara wa Tanzania, wakahamasika sana, na waliporejea tuu nyumbani Tanzania, orders zikaanza. Kuna kikundi cha akinamama wasuka mikeka ya majani, wakapewa order ya kupeleka 40ft contena la mikeka hiyo inayosukwa akinamama wa vijijini mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Wakinamama wale na kikundi chao, walitembea na hiyo order wakitafuta mtaji wa kuitekeleza hadi ika expire. Ukishindwa ku deliver order ndani ya siku 90, order ina expire, sasa inakuwa wazi kwa kila mwenye uwezo, yaani an open order.

Baada ya siku 90, makampuni ya jirani zetu Kenya, walikuja nchini, wakaenda Pwani, Lindi na Mtwara kuinunua mikeka yote na kuisafirisha hadi Nairobi, wakaipakia kwenye makontena na kuifikisha sokoni Marekani, mikeka yenye certificate of origin ya Tanzania, lakini imeingizwa sokoni na Wakenya, huku sisi Watanzania tumelala.

Huu ni mfano mmoja tuu wa jinsi sisi Watanzania tunashindwa kuchangamkia fursa za masoko, hadi AGOA ya awamu ya kwanza ya kipindi cha miaka 10 kimepita, Tanzania tumeshindwa kabisa kutumia fursa hizo, sasa AGOA imeongeza miaka 10 mingine, na bado sisi Tanzania kama nchi, bado hatujaweza kuchangamkia fursa za soko la AGOA.

Hali ni hivyo hivyo kwa soko la Afrika Mashariki, Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa utajiri wa kila kitu, kuanzia vivutio vya utalii, maliasili, madini, vyanzo vya maji, ardhi ya kutosha kwa kilimo, udongo wenye rutuba, na sasa tuna gesi asili na soon tutagundua mafuta, hivyo Tanzania tuna kila sababu ya kuwa ni nchi Tajiri, bado tunaendelea na umasikini tulionao, ukijiuliza kwanini Tanzania ni masikini, huwezi kupata jibu sahihi.

Umasikini mkubwa zaidi na umasikini mbaya zaidi ni umasikini wa fikra, fikra ni kama kauli huumba, ukijifikiria kuwa wewe ni masikini, ni kweli unakuwa masikini kweli, ndio maana msimamo wa Rais Magufuli na kauli yake kuwaTanzania sio masikini bali ni nchi Tajiri, unapaswa kuungwa mkono na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania yetu, tuache kabisa kujiita masikini tukajikuta tunajiumbia umasikini, tuanza kujiita Tanzania ni nchi tajiri ili kujiumbia utajiri.

Nikiangalia kiwango cha uhamashaji mkutano huu na nguvu inayotumika kuuhamashisha mkutano huu, tukiitumia katika kuhamashisha kuchangamkia soko la SADC, uhamasishaji huo utakuwa na manufaa ya muda mrefu zaidi baada ya mkutano kumalizika.

Kinachofanya jirani zetu Wakenya, watushinde kwenye kuchangamkia fursa ni serikali yao kuingiza mkono wake kusaidia, hivyo sasa serikali awamu ya tano imeishaonyesha njia, kwanza kwa rais Magufuli kukaa na wafanyabiashara na kusikiliza kero zao ikiwemo kuchukua hatua za papo kwa papo. Bila mkono wa serikali katika kuweka mazingira wezeshi, wafanyabiashara wenyewe tuu kama wafanyabiashara, hatutaweza kuliteka soko la SADC lenye watu milioni 450, kama hili soko tuu la Africa Mashariki, Tanzania bado!, kwa sasa wanunuzi wakubwa wa mazao yetu ni jirani zetu na sio sisi.

Nawatakia maonyesho mema ya SADC na pia Nane Nane njema.

Paskali

Unapomuuzia mwafirka mwenzio toka msumbiji kinyago? kweli uehamasika
 
Anakuja mgeni kutoka duniani kwa jasho na damu,anaamua kuwekeza anapata mavuno yenye faida kubwa sana,anaondoka na utajiri wakati sisi tunaishia kushangaa shangaa na kuilalamikia serikali!

Tunahitaji mabadiliko makubwa sana kifikra kuweza kuchangamkia fursa za ndani na nje ya nchi

Unataka tuchangamkie fursa, ugeni ulikuwa na watu wangapi? Hao watu wakitoka kwenye kikao, si wanaenda walikofikia!! Hizo fursa mnasema tu, au pia na wewe ni moja wa wanaoliunga!!??
 
Paskali acha tu kaka yangu, nakumbuka kuna mjomba wangu alikuja kwa mzee akamkopa baada ya ile hamasa ya mkutano wa Sullivan, kwamba kuna fursa. Mzee akampatia kwa makubaliano ya kurejesha mkopo na riba kidogo. Hasara aliyopata mjomba wangu mpaka leo mzee anamchukia mama yangu. Hawa viongozi wanaotangaza hizi fursa kwangu nawaona kama matapeli wanaohalalisha imprest. JK na viongozi wa serikali yake waliokuwa wanahamasisha watu kuhusu mkutano wa Sulivan kwamba ni fursa ni wangapi mpaka leo wanafanya biashara kupitia fursa ile zaidi ya kuandika mawaraka?

Juzi nimesema hapa kwenye uzi uliokuwa unasema eti Makonda awapatia ulaji wauza vinyago kwa kufunga mtaa! Ule ni utapeli kama utapeli mwingine, nikasema kama Makonda anaona ni fursa kweli apeleke container la vinyago kisha mkutano ukiisha alete mrejesho wa faida aliyopata. Ingekuwa hiyo mikutano ina fursa kweli ungeona hizo biashara zikifanywa na viongozi wa serikali na wa vyombo vya dola. Fursa pekee ya kweli hapa nchini kwetu ni madaraka ya kisiasa. Ndio maana angalia kiongozi yoyote akiwa madarakani mambo yake yanavyokuwa safi, na anatumia mbinu yoyote hata ya mauji ili apate hayo madaraka. Na akitoka kwenye madaraka mambo yake yanakuwa wastani na sanasana mabaya. Hata yale aliyokuwa anahubiri kwamba ni fursa hathubutu kuyafanya, na akiyafanya anaishia kufail.

Ninasisitiza, mtanzania yoyote asidanganywe na mwanasiasa yoyote eti kuna fursa kwenye huo mkutano. Fursa pekee ni malazi, usafiri na chakula ambazo bila hata debe la mwanasiasa yoyote hizo ni fursa automatically. Wageni 1,000 kwa Dar wapo kila siku bila debe ya mwanasiasa yoyote. Huo mkutano sana sana ni porojo zinapigwa maana ni ajenda za viongozi sio za wananchi, na wale watakaoona fursa za SADC bila hata debe la huo mkutano ni wale wale waonaji bila hata mkutano. Ukitaka kuamini ngoja siku mtu kama Makonda au Kabudi wakitoka madarakani kama watakaa hata wapeleke mahindi ya kuchoma kwenye nchi za SADC.
 
Naona poti wako kakuchunia ile mbaya hata nafasi aliyopewa Mtatiro ingekufaa lkn wapiiiiii
Wanabodi,
leo nimepata tena fursa ya kuendelea na zile makala zangu za kwa Maslahi ya Taifa, leo nauzungumzia Maonyesho ya SADC, kwanza kwa vile maonyesho haya ya SADC, yamegongana na maonyesho ya Nane Nane ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Simiyu, ombi langu la kwanza ni tusiache mbachao kwa msala upitao, Maonyesho ya Nane Nane ni mbachao, Maonyesho ya SADC ni msala upitao, uhamasishaji wa maonyesho ya SADC, pia uende sambamba na maonyesho ya Nane Nane.

Hoja yangu kuu katika bandiko hili ni kwanza kutoa pongezi kwa kazi kubwa na kazi nzuri inayofanywa kuhamasisha mkutano huu wa SADC ambao umerudi tena kufanyika nchini Tanzania baada ya miaka 16. Kiukweli uhamasishaji ni mkubwa, na Watanzania tumehamasika, na kila kada kujipanga kuchangamkia fursa za mkutano huu, kitu muhimu kuliko hata kuchangamkia fursa ni sisi Watanzania na Tanzania yetu kama nchi, inachangamkia vipi fursa za soko la SADC lenye watu milioni 450?.

Pia naomba kutoa angalizo muhimu kwa viongozi wetu, katika kuwapatia wafanyabiashara fursa za mkutano huu, naombeni sana msiwape too much expectations wengine wakakopa kwa kutegemea zitarudi, hili ninilishuhudia kwenye mkutano wa Sullivan, ulikuwa ni mkutano wa fursa, wakazi wa Arusha wakajitoa kwelikweli, mwisho wa siku kuna wafanyabiashara waliishia kujuta, na sikubahatika kupata mrejesho wowote ni fursa zipi za Sullivan, Tanzania tulifanikiwa kuzipata.

Mimi nilipata bahati ya kuwemo kwenye kundi la waandishi wa habari wa Tanzania, waliopelekwa nchini Marekani kuelimishwa kuhusu fursa za soko la AGOA. Shirika la misaada la watu wa Marekani USAID wakagharimia viongozi wa wizara ya viwanda na biashara, viongozi wa BET (sasa Tantrade, na viongozi wa vyama vya vya wafabiashara mtambuka chini ya TCCIA, CTI na kundi kubwa la wafanyabiashara zaidi ya 100, kwenda nchini Marekani kuonyeshwa fursa za AGOA.

Kule tulionyeshwa soko la Marekani linataka bidhaa gani, zenye ubora gani, viwango gani, ufungashaji gani na taratibu za kufuata, soko hilo ni kubwa na linahitaji bidhaa zaidi ya 1000 kutoka Tanzania zikiwemo bidhaa za kiutamaduni, vinyago, mapambo, maua.

Wamarekani wakafanya hivyo hivyo kwa Kenya, Uganda, Ghana, Rwanda na Burundi na nchi mbalimbali.

Kilichofuatia ziara hiyo, wafanyabishara wa Tanzania, wakahamasika sana, na waliporejea tuu nyumbani Tanzania, orders zikaanza. Kuna kikundi cha akinamama wasuka mikeka ya majani, wakapewa order ya kupeleka 40ft contena la mikeka hiyo inayosukwa akinamama wa vijijini mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Wakinamama wale na kikundi chao, walitembea na hiyo order wakitafuta mtaji wa kuitekeleza hadi ika expire. Ukishindwa ku deliver order ndani ya siku 90, order ina expire, sasa inakuwa wazi kwa kila mwenye uwezo, yaani an open order.

Baada ya siku 90, makampuni ya jirani zetu Kenya, walikuja nchini, wakaenda Pwani, Lindi na Mtwara kuinunua mikeka yote na kuisafirisha hadi Nairobi, wakaipakia kwenye makontena na kuifikisha sokoni Marekani, mikeka yenye certificate of origin ya Tanzania, lakini imeingizwa sokoni na Wakenya, huku sisi Watanzania tumelala.

Huu ni mfano mmoja tuu wa jinsi sisi Watanzania tunashindwa kuchangamkia fursa za masoko, hadi AGOA ya awamu ya kwanza ya kipindi cha miaka 10 kimepita, Tanzania tumeshindwa kabisa kutumia fursa hizo, sasa AGOA imeongeza miaka 10 mingine, na bado sisi Tanzania kama nchi, bado hatujaweza kuchangamkia fursa za soko la AGOA.

Hali ni hivyo hivyo kwa soko la Afrika Mashariki, Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa utajiri wa kila kitu, kuanzia vivutio vya utalii, maliasili, madini, vyanzo vya maji, ardhi ya kutosha kwa kilimo, udongo wenye rutuba, na sasa tuna gesi asili na soon tutagundua mafuta, hivyo Tanzania tuna kila sababu ya kuwa ni nchi Tajiri, bado tunaendelea na umasikini tulionao, ukijiuliza kwanini Tanzania ni masikini, huwezi kupata jibu sahihi.

Umasikini mkubwa zaidi na umasikini mbaya zaidi ni umasikini wa fikra, fikra ni kama kauli huumba, ukijifikiria kuwa wewe ni masikini, ni kweli unakuwa masikini kweli, ndio maana msimamo wa Rais Magufuli na kauli yake kuwaTanzania sio masikini bali ni nchi Tajiri, unapaswa kuungwa mkono na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania yetu, tuache kabisa kujiita masikini tukajikuta tunajiumbia umasikini, tuanza kujiita Tanzania ni nchi tajiri ili kujiumbia utajiri.

Nikiangalia kiwango cha uhamashaji mkutano huu na nguvu inayotumika kuuhamashisha mkutano huu, tukiitumia katika kuhamashisha kuchangamkia soko la SADC, uhamasishaji huo utakuwa na manufaa ya muda mrefu zaidi baada ya mkutano kumalizika.

Kinachofanya jirani zetu Wakenya, watushinde kwenye kuchangamkia fursa ni serikali yao kuingiza mkono wake kusaidia, hivyo sasa serikali awamu ya tano imeishaonyesha njia, kwanza kwa rais Magufuli kukaa na wafanyabiashara na kusikiliza kero zao ikiwemo kuchukua hatua za papo kwa papo. Bila mkono wa serikali katika kuweka mazingira wezeshi, wafanyabiashara wenyewe tuu kama wafanyabiashara, hatutaweza kuliteka soko la SADC lenye watu milioni 450, kama hili soko tuu la Africa Mashariki, Tanzania bado!, kwa sasa wanunuzi wakubwa wa mazao yetu ni jirani zetu na sio sisi.

Nawatakia maonyesho mema ya SADC na pia Nane Nane njema.

Paskali
 
Thanks for info Mkuu.SADC population ni 450 m au 350?Mimi naona Fursa zipo but bureaucracies zipungue bidhaa zinakua na kodi au vibali kadhaa na bado boda kuna usumbufu bila rushwa unasumbuka Sana kugongewa passport.Pia Mozambique unyanyasaji Kwa WaTz ni mkubwa Sana na Tupo nao SADC.
 
Unataka tuchangamkie fursa, ugeni ulikuwa na watu wangapi? Hao watu wakitoka kwenye kikao, si wanaenda walikofikia!! Hizo fursa mnasema tu, au pia na wewe ni moja wa wanaoliunga!!??

Hana lolote, yeye anahuburi fursa, kisha anatembea na hirizi ili asifukuzwe kazi! Ukimwambia aache kazi akachamgamkie hizo fursa anaongea kwa soni eti biashara ina changamoto! Ukitaka kucheka nenda kawaambie hao viongozi wote wanaohubiri kuna fursa waache kazi watupishe sisi tusioona fursa, kisha wao wakamate hizo fursa uone kama hujafunguliwa kesi ya kuwa mchochezi na risasi juu. Nasisitiza tena, fursa pekee ya ukweli ni kuwa na madaraka ya kisiasa fullstop.
 
Hana lolote, yeye anahuburi fursa, kisha anatembea na hirizi ili asifukuzwe kazi! Ukimwambia aache kazi akachamgamkie hizo fursa anaongea kwa soni eti biashara ina changamoto! Ukitaka kucheka nenda kawaambie hao viongozi wote wanaohubiri kuna fursa waache kazi watupishe sisi tusioona fursa, kisha wao wakamate hizo fursa uone kama hujafunguliwa kesi ya kuwa mchochezi na risasi juu. Nasisitiza tena, fursa pekee ya ukweli ni kuwa na madaraka ya kisiasa fullstop.
Hapa ni kina bashite tu ndo wanafaidi na wenye koneksheni mjini
 
Thanks for info Mkuu.SADC population ni 450 m au 350?Mimi naona Fursa zipo but bureaucracies zipungue bidhaa zinakua na kodi au vibali kadhaa na bado boda kuna usumbufu bila rushwa unasumbuka Sana kugongewa passport.Pia Mozambique unyanyasaji Kwa WaTz ni mkubwa Sana na Tupo nao SADC.

Huo mkutano ni wa kurefresh mind, hamna lolote la maana litatekelezwa kwenye makubaliano yao. Tuna uzoefu na hiyo mikutano. Kwangu huwa naona ni utapeli kama utapeli mwingine.
 
Pamoja na kuihitaji serikali kutia mkono katika kuchangamkia fursa,lakini bado hata sisi wenyewe tumekuwa stagnant sana kuchangamkia fursa husika

Tulio wengi tunataka vitu vigumu vifanywe na wengine then sisi tuambiwe mavuno tayari ndiyo tuchangamkie,lakini utayari wa kuanza vitu vigumu ni mdogo sana!

Mfano mzuri ni huu,nimepita maeneo mengi yenye mabonde very productive(kilombero,Ukanda wa ziwa Rukwa,Mbarali) ni mabonde yenye rutuba ya hatari,lakini hatuyatumii ipasavyo kwa kisingizio kwamba serikali haijatusaidia kuweza kuyalima,unajiuliza wewe uwezo wako ku-explore hiyo fursa kabla kuomba support ya serikali ni kiasi gani mtu anatoa macho tu!

Anakuja mgeni kutoka duniani kwa jasho na damu,anaamua kuwekeza anapata mavuno yenye faida kubwa sana,anaondoka na utajiri wakati sisi tunaishia kushangaa shangaa na kuilalamikia serikali!

Tunahitaji mabadiliko makubwa sana kifikra kuweza kuchangamkia fursa za ndani na nje ya nchi!
Pascal Mayalla

Hayo mabonde very productive mbona ww hatukuoni ukiyalima ili yasilimwe na wageni toka nje? Ww unalinda tu ajira, lakini unashauri wenzako wakayalime hayo mabonde.
 
Soko la Sadc watanzania wafanyabiashara walishalichangamkia siku nyingi nenda pale soko la Sadc Lusaka Zambia uone wafanyabiashara watanzania walivyojaa.Fursa walishaiona siku nyingi waandishi ndio mnaona Leo?
 
Back
Top Bottom