Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Scotland: Rais Samia ametuangusha

Hapo umepotosha. Dira ya Rais Samia iko wazi kabisa sema nyie mnaomuabudu yule DIKTETA mnabisha kama sehemu ya ibada.

Dira ya Samia ni kujenga uchumi utakaoleta financial inclusion kwa raia wake kupitia uwekezaji toka nje, biashara na nchi jirani huku tukizingatia utawala wa Sheria na haki.

Tanzania ilikuwa ni kisiwa wakati wa Mwendazake. Mama anafungua Tanzania kiuchumi
Mkuu 'Stuxnet' umejibu kwa staha, kwa hilo nitaheshimu, lakini umekosea kuniweka kwenye hilo kundi la DIKTETA.

Kuhusu hiyo unayoiita "dira ya mama", hilo tunaweza kulijadili kwa kina. Binafsi sikubaliani na utegemezi wa kuja kuendelezwa na mtu mwingine. Tutajiendeleza kwa juhudi zetu. Hii haina maana kwamba hatutashirikiana na wengine kutoka nje kwa heshima na maslahi yetu yakiwa ndio kipaumbele.
Usitake kupotosha kwa kudai kwamba ninaposisitizia juhudi zetu kujiendeleza ndio iwe maana ya kwamba sitaki ushirikiano na wengine.
 
Nashangaa huku Dar watu wanajenga na kukata miti kila mahali frame wamesahau umuhimu wa miti ndio maana joto linazidi, ukienda Morogoro Hali inasikitisha Yani watu wamekata miti midogo na hawaipandi hata kidogo. Serikali ije na sheria kila nyumba lazima ipandwe miti Ili kulinda nchi na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Sasa dar ukipanda miti kwenye eneo la 20*20 utapata hata sehemu ya kupaki baiskeli?
 
Yaani nilipomsikia anazungumzia kupewa misaada na analialiatu sisi nchi masikini nikajiuliza haya kama ni masikini dunia haijaanza leo wala yeye hajaanza kuzurula huko alikuwepo muzurulaji mahili Kikwete hakuna tulichopata! Anasema anakusanya trilion almost mbili kwa mwezi pamoja na tozo! Kwa kweli anapoteza rasilimali kwenda kulialia kwa watu ambao wanasimamia masirahi yao!
kinachoniuma zaidi ni kuomba misaada ya kutunza mzingira halafu huku yetu tunayaharibu maksudi
 
Wafugaji wamejaa maporini wanafyeka misitu/mapori eti wanyama wao wasipotee, hakuna anaejali! Wenye mamlaka wako bize na machinga! Bado mapori ya akiba/tengefu kwa ajili ya kuhifadhi mazingira mnawagawia wananchi wafyeke waishi! Ina maana Mwalimu alikuwa mjinga kuyatenga? Aisee yaani afrika haina viongozi ndiyo maana tramp alikuwa anawadharau sana! Yaani ni mizigo! Ndiyo haibebeki! Mapori yanateketea halafu wanaenda ulaya sijui kusema nini! Sisi wakulima tunasikitika sana!
Unaishi Karagwe nini!
 
Mkuu 'Stuxnet' umejibu kwa staha, kwa hilo nitaheshimu, lakini umekosea kuniweka kwenye hilo kundi la DIKTETA.

Kuhusu hiyo unayoiita "dira ya mama", hilo tunaweza kulijadili kwa kina. Binafsi sikubaliani na utegemezi wa kuja kuendelezwa na mtu mwingine. Tutajiendeleza kwa juhudi zetu. Hii haina maana kwamba hatutashirikiana na wengine kutoka nje kwa heshima na maslahi yetu yakiwa ndio kipaumbele.
Usitake kupotosha kwa kudai kwamba ninaposisitizia juhudi zetu kujiendeleza ndio iwe maana ya kwamba sitaki ushirikiano na wengine.
Hata ukiwa na juhudi zako nzuri na raslimali zote kama utakuwa huna multitateral na bilateral cooperation na nchi zingine huwezi kupiga hatua.

Hamna mtu anabeza juhudi binafsi za nchi na wananchi wake
 
Masalia ya utumwa akili utumwa ndio urithi ulio tamalaki. Elimu mazingira tena elimu shirikishi bottom-up, ushiriki wa viongozi tena kuwa mfano, usimamizi, sera thabiti, citing sustainable development goals hasa vipengele vya mazingira, kuhimitiza utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya nyakati zilizopita, na kuainisha mafanikio ya tanzania katika utekelezaji wa maazimio hayo na mipango thabiti iliopo kwa sasa na baadae, kuweka mfano bayana wa tunachofanya tanzania kwa muktadha wa maudhui at hand.

Wenye akili wapo lakini je wanaheshimika, kujumuishwa, kuaminiwa, kushirikishwa na kupewa nafasi za kuwasaidia viongozi.

Unapewa pesa baada kuonesha na kuainisha relevant proposals au projects zinazovutia watoa pesa.
Neno hilo
 
Wanabodi,



Kama mtanzania, inawezekana umepata nafasi kufuatilia yanayojiri nchini Scotland kwenye mkutano unaohusu mabadiliko ya tabia nchi. Mkutano huu umehudhuriwa na viongozi wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alihutubia mkusanyiko huo.

Tofauti na nchi kama China, Marekani na India, Tanzania haihusishwi sana kwa kuwa chanzo cha mabadiliko ya tabia nchi. Umuhimu wa kuhudhuria mkutano huo ni kujumuika na viongozi wengine katika kujadili suala hili na kuwa na mchango unaoweza kuleta manufaa chanya kwa miaka mingi ya baadaye.

View attachment 1996340

Nimebahatika kuanglia hotuba zote za Rais Samia na kwa bahati mbaya au nzuri, aligusia zaidi kwenye umuhimu wa nchi zilizoendelea kuzisaidia nchi ambazo hazijaendelea kifedha ili kuweza kukabiliana na tatizo hili la mabadiliko ya tabia nchi.

Labda inawezekana kwamba ni kweli Tanzania inahitaji misaada hiyo lakini kwa upande wa pili haipendezi kuona kwamba mawazo haya ya kuendelea kupata misaada imetawala katika vichwa vya viongozi wetu. Kauli kama hizo zinaweza zisizae matunda.

Ingependeza sana kama Rais Samia angejizatiti zaidi katika kuongelea umuhimu wa kuwa na "balance" katika shughuli za maendeleo, maslahi ya binadamu na mikakati ya kulinda mazingira. Kama Tanzania, angezungumzia changamoto zinazo sababishwa na mabadiliko ya tabia nchi na mipango yetu haswa katika kipindi ambacho tunatamani uchumi wa viwanda.

Kwa nchi zilizoendelea, umuhimu wa sayansi katika kuvumbua njia mpya zisizo chochea uharibifu wa mazingira zinazoweza kutumika kwenye sekta mbali mbali

Mungu ni mwema, wakati wote

Hotuba safi kabisa imetolewa na yule mama wa Barbados. Huyo mama nimeona ni kiongozi anayejitambua na siyo wa kwetu ambaye ameonekana kuhangaikia kujulikana. Ni kama amekwenda kujitangaza ili ajulikane. Ni makosa yake na makosa ya kutafuta wasaidizi wabovu.
Hii ndo hotuba
 
Hapo umepotosha. Dira ya Rais Samia iko wazi kabisa sema nyie mnaomuabudu yule DIKTETA mnabisha kama sehemu ya ibada.

Dira ya Samia ni kujenga uchumi utakaoleta financial inclusion kwa raia wake kupitia uwekezaji toka nje, biashara na nchi jirani huku tukizingatia utawala wa Sheria na haki.

Tanzania ilikuwa ni kisiwa wakati wa Mwendazake. Mama anafungua Tanzania kiuchumi
Kinachojadiliwa ni hotuba yake Glasgow. Una maana yeye kila anakokwenda anatafuta pesa ya msaada? Suala la mazingira siyo jambo la kurukia tu na kuandikiwa hotuba. Alistahili awe na watu welevu wanaojua dynamics za mikutano ile. Sisi kama TZ tuna alama kubwa sana ya climate change; Kilimanjaro na Z'bar kama sehemu ya visiwa vinavyozama. Huo ungekuwa mtaji mkubwa sana wa kuwafanya viongozi wengine wasikilize. Kwa nini yeye ameishia kuzungumzia theories za climate change kwa watu wanaojua kuliko yeye?

Mkutano kama ule unaanza kueleza madhara ya climate change? Unamueleza nani asiyejua?
 
Hata mimi nilitegemea hivyo kwamba kwa kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni agenda ambayo imeonekana kuwa changamoto, je sisi japo ni nchi changa kiuchumi tuna idea gani tofauti na maalum ambayo mataifa tajiri yangeweza kuipokea au kuichota na kuitumia kupunguza au kutatua changamoto hiyo?
Kweli kabisa
 
Mleta mada naomba ujielekeze kwa usahihi...
Lisemwalo lipo... Hizo nchi zilizoendelea "zinaiba" sana rasilimali za dunia kujiendeleza! Na pia katika mchakato wa kufanya hivyo zinafanya uzalishaji mkubwa wa gesijoto na kufanya uchafuzi mwingi unaosambaa ulimwenguni kote!
Sikia; kwamba nchi tajiri zilizoendelea zitoe fedha kusaidia nchi maskini na zinazoendelea ni suala la makubaliano rasmi yaliyokuwepo toka enzi za Kyoto Protocol na sasa Paris Agreement. Hivyo #SSH kuweka msisitizo huo kwenye hotuba zake ni kuwakumbusha hao wakubwa majukumu yao kwenye makubaliano rasmi yaliyopo.
Itakuwa ni ajabu kama unaona tatizo kwenye kuwadai uwekezaji wa fedha hizo!
Hiyo ndiyo climate politics! #SSH yupo sahihi!
Ni ujinga kuwakamua wananchi maskini wa Tanzania ili kutoka kwao fedha zipatikane za uwekezaji na ujenzi wa miundombinu (hizo akili zilizikwa pamoja na JPM).
Matajiri wa dunia hii wana pesa ambazo walizipora kutoka kwetu. Matajiri wa dunia hii wamesababisha mabadiliko ya tabianchi kwa viwango visivyomithilika! Matajiri wa dunia hii wanauwezo mkubwa wa kustahimili majanga yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi tofauti na maskini wa dunia hii! HIVYO wanapaswa kubanwa wazirudishe kwa namna nzuri na endelevu ya kuzikwamua na kuziendeleza nchi maskini kujihimu na mabadiliko ya tabianchi!
Na huo ndo msimamo wa dunia kwa sasa unaoangazia masuala ya climate finance and adaptation fund kwa kuwataka nchi tajiri kutoa zaidi fedha na technolojia!
Kama unapingana nao basi huyajui vizuri mabadiliko ya tabianchi na madhara yake.

NB: Tafadhali rejea reports mbalimbali za UN, UNFCCC, IPCC, KYOTO PROTOCOL, PARIS AGREEMENT, n.k!
Mama #SSH hakwenda kutembeza mabakuli. Kwa muda mrefu mikutano ya UNFCCC COP imekuwa ni sehemu ya kuzibana nchi tajiri kutimiza makubaliano yaliyopo.
[ ] Nina amini kwamba madhumuni ya mkutano unaoendelea nchini Scotland ni kuweza kujadili changamoto mbali mbali zinazohusu mabadiliko ya tabia nchi. Ni jambo kubwa kuweza kuwa kusanya viongozi wote walio hudhuria na kwasababu hiyo vipaumbele lazima vilihusu kupata solutions kutatua tatizo hili. Umeelezea kuhusu ulazima wa nchi zilizo endelea kusaidia kifedha nchi zinazo endelea lakini sidhani kama mkutano huo ulikuwa muafaka kuwa kumbusha kuhusu "Jukumu" hilo. Instead huo ulikuwa muda wa kujenga hoja nzito, kuwa na taarifa mbali mbali kuhusu tatizo hili na kuwa na mchango ambao unatekelezeka na kudumu katika mawazo ya viongozi wengine.
 
Wanabodi,



Kama mtanzania, inawezekana umepata nafasi kufuatilia yanayojiri nchini Scotland kwenye mkutano unaohusu mabadiliko ya tabia nchi. Mkutano huu umehudhuriwa na viongozi wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alihutubia mkusanyiko huo.

Tofauti na nchi kama China, Marekani na India, Tanzania haihusishwi sana kwa kuwa chanzo cha mabadiliko ya tabia nchi. Umuhimu wa kuhudhuria mkutano huo ni kujumuika na viongozi wengine katika kujadili suala hili na kuwa na mchango unaoweza kuleta manufaa chanya kwa miaka mingi ya baadaye.

View attachment 1996340

Nimebahatika kuanglia hotuba zote za Rais Samia na kwa bahati mbaya au nzuri, aligusia zaidi kwenye umuhimu wa nchi zilizoendelea kuzisaidia nchi ambazo hazijaendelea kifedha ili kuweza kukabiliana na tatizo hili la mabadiliko ya tabia nchi.

Labda inawezekana kwamba ni kweli Tanzania inahitaji misaada hiyo lakini kwa upande wa pili haipendezi kuona kwamba mawazo haya ya kuendelea kupata misaada imetawala katika vichwa vya viongozi wetu. Kauli kama hizo zinaweza zisizae matunda.

Ingependeza sana kama Rais Samia angejizatiti zaidi katika kuongelea umuhimu wa kuwa na "balance" katika shughuli za maendeleo, maslahi ya binadamu na mikakati ya kulinda mazingira. Kama Tanzania, angezungumzia changamoto zinazo sababishwa na mabadiliko ya tabia nchi na mipango yetu haswa katika kipindi ambacho tunatamani uchumi wa viwanda.

Kwa nchi zilizoendelea, umuhimu wa sayansi katika kuvumbua njia mpya zisizo chochea uharibifu wa mazingira zinazoweza kutumika kwenye sekta mbali mbali

Mungu ni mwema, wakati wote

Mipango bila pesa ni ubatili mtupu.
 
Hoja ya "balance" katika maendeleo, masilahi ya binadamu inaweza ikaongelewa na big potatoes tu Ile ya G8, na siyo shithole countries (kama alivyoziita Trump).

Wale emmitters wakubwa wa carbon dioxide yaani China, USA, European Union na China kupitia Greenhouse gas ndiyo wanapaswa kujadili hilo.

Namuona Rais SSH ame address real issue ambayo itatuongezea fedha za kuratibu mazingira kupitia COP 26 ambayo itatenga USD 19 Bilion kwa nchi 197 ambazo zimeridhia mkataba wa Paris juu ya mabadikiko ya tabia nchi.

Mara nyingine hata kimoyomoyo tukubali tu kuwa nchi iko kwenye reli sahihi mikononi mwa Rais SSH hata kama tuna tofauti za kiitikadi, kidini na kikanda
Una kubali kwamba fedha hizo zinapatikana bila kuonyesha mikakati inayo tekelezeka na kubaini uzito wa tatizo hilo nchini?
 
[ ] Nina amini kwamba madhumuni ya mkutano unaoendelea nchini Scotland ni kuweza kujadili changamoto mbali mbali zinazohusu mabadiliko ya tabia nchi. Ni jambo kubwa kuweza kuwa kusanya viongozi wote walio hudhuria na kwasababu hiyo vipaumbele lazima vilihusu kupata solutions kutatua tatizo hili. Umeelezea kuhusu ulazima wa nchi zilizo endelea kusaidia kifedha nchi zinazo endelea lakini sidhani kama mkutano huo ulikuwa muafaka kuwa kumbusha kuhusu "Jukumu" hilo. Instead huo ulikuwa muda wa kujenga hoja nzito, kuwa na taarifa mbali mbali kuhusu tatizo hili na kuwa na mchango ambao unatekelezeka na kudumu katika mawazo ya viongozi wengine.
Tafadhali fuatilia hapa umsikilize Waziri Mkuu wa Barbados....ameupiga mwingi sana! 👇👇


Kwa taarifa tu ni kuwa mkutano wa UNFCCC COP unatanguliwa na matoleo ya ripoti za kisayansi juu ya mabadiliko ya tabianchi. Fuatilia zaidi hapa:👇👇 https://www.ipcc.ch/

KWa asilimia kubwa hizo reports ndo zinakuwa kiini cha majadiliano na makubaliano mengi kwenye mkutano wa UNFCCC COP.
Mijadala itaendelea na nyakati wakati wanafikia muafaka. Sema kuna wakati mambo yanavurugika bila makubaliano yoyote ya maana!
Tufiatilie COP26 kule Glasgow tujue yatakayojiri!
 
Hotuba safi kabisa imetolewa na yule mama wa Barbados. Huyo mama nimeona ni kiongozi anayejitambua na siyo wa kwetu ambaye ameonekana kuhangaikia kujulikana. Ni kama amekwenda kujitangaza ili ajulikane. Ni makosa yake na makosa ya kutafuta wasaidizi wabovu.
Hii ndo hotuba

Hotuba zote ni hotuba... Kila mtu na kipaji chake!
Muhimu ujumbe ufike! #SSH hawezi kuwa huyo PM wa Barbados; Bi Mia Mottley! Ni binadamu wawili tofauti!
 
Kumekuchaaa

Screenshot_20211103-214444.jpg
 
Back
Top Bottom