Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Scotland: Rais Samia ametuangusha

Kinachojadiliwa ni hotuba yake Glasgow. Una maana yeye kila anakokwenda anatafuta pesa ya msaada? Suala la mazingira siyo jambo la kurukia tu na kuandikiwa hotuba. Alistahili awe na watu welevu wanaojua dynamics za mikutano ile. Sisi kama TZ tuna alama kubwa sana ya climate change; Kilimanjaro na Z'bar kama sehemu ya visiwa vinavyozama. Huo ungekuwa mtaji mkubwa sana wa kuwafanya viongozi wengine wasikilize. Kwa nini yeye ameishia kuzungumzia theories za climate change kwa watu wanaojua kuliko yeye?

Mkutano kama ule unaanza kueleza madhara ya climate change? Unamueleza nani asiyejua?
Mbona kaongelea hyo ya Zanzibar na kisiwa kuzama, barafu ya Kilimanjaro kuyeyuka, au ulitaka aongelee uwanja wa ndege wa Chato?
 
Heri kukopa kuliko ombaomba. Unapokopa unaonesha unauwezo wa kurejesha. Ombaomba utafanywa chochote. Kukopa hata nchi tajiri ukopa. Marekani, Ufaransa, Italy na nyinginezo zinamadeni kibao, kwa kukopa.
Ombaomba, ni kutokuwa na akili za ya kufikiri njia nyingine ya kumaliza au kukabiliana na tatizo.
Tanzania hatuna uharibifu mkubwa wa mazingira. Hivyo unapoomba hizo fedha hata wao wanaangalia na kucheka tu.
Katika uharibifu wa mazingira kuna sheria ya "Polutor pay system" hivyo Tanzania hatumo. Hela za nini, tusiwe tunajidhalilisha. Uwezo wa kutunza mazingira yetu bado tunao sisi wenyewe. Shida serikali haijui kupanga miji yetu. Wao wanadhani kujenga kila sehemu ndo maendeleo. Där es Salaam haina sehemu ya kupumlia, hakuna Park au bustani kubwa za miti katikati ya mji hata pembezoni.
Tanzania tunachojua ni kukatamiti na kujenga. Dar nzima utatembea na miji mingine hakuna hata benchi la kukaa mtu apumzike.
Wakati wa Nyerere alijaribu kuimarisha Park ktk miji kadhaaa lkn baadae ziligeuzwa viwanja kujenga.
Sasa tunachoomba ni nini wakati hatujui hata kutunza mazingira. Serikali ni waongo tu ndo maana fedha ya Uviko wao wanajengea madarasa. Wakati walisema tozo itajenga. Hizo fedha zingetumika kuboresha afya.
Watanzania tunapenda ushabiki, badala ya kumshauri kiongozi nini kifanyike chenye maslahi ya Taifa. Na kubwa wataalam wetu wanacopy na kupaste taarifa na hotuba. Ni wavivu kufikiria jumbo jipya. Hivyo kama Rais si mfuatiliaji atajikuta anajikita yaleyale. Kuomba fedha ni falsafa ya nchi za Afrika zikidhani hela ndo suluhisho kwa kila kitu. Hata wakipewa hazitumiki ktk kusudio lililoombewa.
Ndo maana wazungu wanatudharau na kutucheka kuwa tunafikiria hela na misaada kila wakati.
Uharibifu wa mazingira nchini Tanzania sio tatizo kubwa. Athari za mabadiliko ya tabia nchi hazitufikii kwa kiasi ambacho kinaweza kufikiriwa. Tanzania sio mlengwa mkuu wa mfuko wa carbon emitters
 
Hotuba safi kabisa imetolewa na yule mama wa Barbados. Huyo mama nimeona ni kiongozi anayejitambua na siyo wa kwetu ambaye ameonekana kuhangaikia kujulikana. Ni kama amekwenda kujitangaza ili ajulikane. Ni makosa yake na makosa ya kutafuta wasaidizi wabovu.
Hii ndo hotuba

Absolutely, Hangaya aone aibu! Lakini ndio hivyo tena wenzetu hawana aibu wamekaa kimipashopasho tu. Thank you Zygot for sharing.
 
Ndio iwe marufuku kila nyumba iwe na miti hafu 20 kwa 20 ujenzi ni uchafuzi wa mji mtaa unakosa hata kichochoro wala sehemu ya kupita hewa msongamano mkubwa
Hivi kijisehemu Cha 20x20 mtu anajengaje nyumba? Alafu anachimba kisima kirefu cha maji na kuweka underground sewer.
Hatari sana!
 
Tafadhali fuatilia hapa umsikilize Waziri Mkuu wa Barbados....ameupiga mwingi sana! 👇👇


Kwa taarifa tu ni kuwa mkutano wa UNFCCC COP unatanguliwa na matoleo ya ripoti za kisayansi juu ya mabadiliko ya tabianchi. Fuatilia zaidi hapa:👇👇 IPCC — Intergovernmental Panel on Climate Change

KWa asilimia kubwa hizo reports ndo zinakuwa kiini cha majadiliano na makubaliano mengi kwenye mkutano wa UNFCCC COP.
Mijadala itaendelea na nyakati wakati wanafikia muafaka. Sema kuna wakati mambo yanavurugika bila makubaliano yoyote ya maana!
Tufiatilie COP26 kule Glasgow tujue yatakayojiri!
Labda niku ulize. Njia zipi huwa zinatumiwa na mataifa kupunguza au kuzuia mabadiliko ya tabia nchi?. Viongozi kutoka nchi ambazo zinasababisha mabadiliko haya kwa kiasi kikubwa wamejadili sana kuhusu uwezekano wa kuwa na "Net zero emissions" itakapo fika mwaka 2050. Je huwa wanatumia mikakati ipi kukabiliana na tatizo hili?. Katika kufanya haya, gharama kubwa huwa inahusishwa na kitu kipi labda?
 
Kubali hatima yako. Resign to your fate. Bila ya kuombaomba utawatesa watu tena utaua. Hakuna lolote utakalotoboa bila ya misaada zaidi ya nguo na viatu vyako kwa uchovu.
Hapo ndo tulipofikia?!! "Nchi ya viwanda...!!" Eti bila kuombaomba utawatesa watu, utaua...nk
Ingependeza ikiwa hiyo ombaomba yako ingefanywa kwa staha zaidi - walosaini mikataba mbalimbali yenye utata wakasulubiwa, matumizi mabaya yasokuwa ya lazima yakadhibitiwa, utajiri mkubwa wa madini na raslimali tulizo nazo ukaonekana kutumika vizuri kwa manufaa yetu na ufujaji unaoendelea kupatiwa dawa.
Ni uungwana pia, unapokwenda kuomba, ionekane kuwa wa nyumbani kwako wananufaika. Isiwe unatumia jina la uwakilishi kumbe ni kwa manufaa binafsi. Wanaokufa kwa kukosa matibabu wapungue, wajinga kwa kukosa elimu bora wapungue na tatizo la umaskini pia lipungue, na watu waone kuwa kuna umakini fulani unaoendelea. Na hizo hotuba zinazosifiwa mchana kutwa, usiku kucha zishuhudie hayo.
Kuwa ombaomba isifanywe kuwa tabia au utamaduni wetu... viongozi waone aibu, ingawa kidogo. Otherwise it's more of the same thing. Waimba mapambio nao wajue kuwa kuna wengi wanao kereka na wanayoyaona yakifanyika yasiyo na uhalisia wowote
 
Kubali hatima yako. Resign to your fate. Bila ya kuombaomba utawatesa watu tena utaua. Hakuna lolote utakalotoboa bila ya misaada zaidi ya nguo na viatu vyako kwa uchovu.
Hapo ndo tulipofikia?!! "Nchi ya viwanda...!!" Eti bila kuombaomba utawatesa watu, utaua...nk
Ingependeza ikiwa hiyo ombaomba yako ingefanywa kwa staha zaidi - walosaini mikataba mbalimbali yenye utata wakasulubiwa, matumizi mabaya yasokuwa ya lazima yakadhibitiwa, utajiri mkubwa wa madini na raslimali tulizo nazo ukaonekana kutumika vizuri kwa manufaa yetu na ufujaji unaoendelea kupatiwa dawa.
Ni uungwana pia, unapokwenda kuomba, ionekane kuwa wa nyumbani kwako wananufaika. Isiwe unatumia jina la uwakilishi kumbe ni kwa manufaa binafsi. Wanaokufa kwa kukosa matibabu wapungue, wajinga kwa kukosa elimu bora wapungue na tatizo la umaskini pia lipungue, na watu waone kuwa kuna umakini fulani unaoendelea. Na hizo hotuba zinazosifiwa mchana kutwa, usiku kucha zishuhudie hayo.
Kuwa ombaomba isifanywe kuwa tabia au utamaduni wetu... viongozi waone aibu, ingawa kidogo. Otherwise it's more of the same thing. Waimba mapambio nao wajue kuwa kuna wengi wanao kereka na wanayoyaona yakifanyika yasiyo na uhalisia wowote
 
Hivi kijisehemu Cha 20x20 mtu anajengaje nyumba? Alafu anachimba kisima kirefu cha maji na kuweka underground sewer.
Hatari sana!
Yani ndio vipigwe marufuku kabisa kwenye miji mikubwa imagine hicho kiwanja kilivo kidogo
 
Kinachojadiliwa ni hotuba yake Glasgow. Una maana yeye kila anakokwenda anatafuta pesa ya msaada? Suala la mazingira siyo jambo la kurukia tu na kuandikiwa hotuba. Alistahili awe na watu welevu wanaojua dynamics za mikutano ile. Sisi kama TZ tuna alama kubwa sana ya climate change; Kilimanjaro na Z'bar kama sehemu ya visiwa vinavyozama. Huo ungekuwa mtaji mkubwa sana wa kuwafanya viongozi wengine wasikilize. Kwa nini yeye ameishia kuzungumzia theories za climate change kwa watu wanaojua kuliko yeye?

Mkutano kama ule unaanza kueleza madhara ya climate change? Unamueleza nani asiyejua?
Sasa amekosea wapi? Mbona unaji contradict mwenyewe. Kwanza unakubali kuwa kwenye mkutano kuna watu wanajuwa kuliko yeye namna Tanzania inavyo athirika na mabadiliko ya tabia nchi. Kwa hiyo ulitaka arudie wanachoelewa?

Yeye amekidhi matakwa ya presidency kwa kukubali kuchukua hatua dhidi ya ukataji miti na kupunguza uzalishaji wa hewa jivu. Na amwsababisha nchi I qualify kwenye GCF grant ya COP 26!!

Hebu fanyeni ya kwenu na familia zenu, Samia ndiyo Rais na anafanya vizuri
 
Hao US wana miradi mingi wanataka tu data kufanya research zao kwa manufaa yao, watu wana pika data wana pata hela wanasepa, no body is your friend
 
Una kubali kwamba fedha hizo zinapatikana bila kuonyesha mikakati inayo tekelezeka na kubaini uzito wa tatizo hilo nchini?
Hiyo siyo level ya Rais. Kwenye mikutano kama hii, hutanguliwa na technical teams meetings hata mwezi mmoja kabla. Vile vile wakati plenary meetings za Marais zikifanyika kunakuwa na breakaway sessions by agenda and by country. Naamini hiyo mikakati unayoitaja iko kwenye documents za Waziri mwenye dhamana ya mazingira au NEMC
 
Labda niku ulize. Njia zipi huwa zinatumiwa na mataifa kupunguza au kuzuia mabadiliko ya tabia nchi?. Viongozi kutoka nchi ambazo zinasababisha mabadiliko haya kwa kiasi kikubwa wamejadili sana kuhusu uwezekano wa kuwa na "Net zero emissions" itakapo fika mwaka 2050. Je huwa wanatumia mikakati ipi kukabiliana na tatizo hili?. Katika kufanya haya, gharama kubwa huwa inahusishwa na kitu kipi labda?
Maswali mazuri!
Hatua zipo nyingi sana. Lakini moja wapo kubwa ni kubadilisha technolojia kutoka zile zinazotumia fossil fuels kupata nishati. Hapa zinatafutwa njia mbadala na rafiki kwa mazingira kama jua, upepo, mawimbi ya bahari, geothermal, hydro n.k.
Serikali hizo aidha zinafanya hivyo zenyewe au zinashirikisha sekta binafsi na watafiti!
FEdha nyingi zinahitajika kuwekeza kwenye technolojia hizo mpya ikiwa ni pamoja na kujenga ushawishi kwa wateja na watumiaji!
 
Maswali mazuri!
Hatua zipo nyingi sana. Lakini moja wapo kubwa ni kubadilisha technolojia kutoka zile zinazotumia fossil fuels kupata nishati. Hapa zinatafutwa njia mbadala na rafiki kwa mazingira kama jua, upepo, mawimbi ya bahari, geothermal, hydro n.k.
Serikali hizo aidha zinafanya hivyo zenyewe au zinashirikisha sekta binafsi na watafiti!
FEdha nyingi zinahitajika kuwekeza kwenye technolojia hizo mpya ikiwa ni pamoja na kujenga ushawishi kwa wateja na watumiaji!
 
Back
Top Bottom