Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,431
- 1,045
Natuma salamu za pongezi kwa hatua na mafanikio yaliyofikiwa na Chama Cha CHADEMA katika uchaguzi wa Igunga. Hizi ni salamu za awali kwa yale matukio na mitihani mliyokwisha-ishinda kuelekea kilele cha ushindi hapo kesho.
Kwa ukumbusho; CDM tayari mmeshinda propaganda ya kummwagia kijana wa ccm tindikali, kuchoma nyumba na ofisi za ccm na makada wao, kuingiza makomandoo kutoka nje ya nchi na mengine mengi. Na pia mmevuka mstari kwa kuweza kueleweka na kukubalika kwa kiasi kikubwa vijijini tofauti na chaguzi zilizopita. Mjini tayari mmekwishashinda.
Ushindi wenu wa kesho una maana kubwa sana kwa Taifa hili. Maana zaidi ya ile ionekanayo machoni na labda pia itakayojulikana na wanaochukulia mambo kijuujuu. Ushindi wenu utamaanisha makubwa yafuatayo:
Ila sijapendezwa na dau mnalotoa CDM kwa watu wa Usalama wa Taifa wanaowapigia simu na kuwapa taarifa za uhakika. Wakati nina taarifa za uhakika ccm kutumia zaidi ya bilioni 4 katika uchaguzi huu lazima pia tujue nanyi mmetumia ngapi na zinafadhiriuwa na nani? Za ccm tunafahamu ni za ufisadi na zinatolewa na magamba, zenu ninyi mnapewa na nani na zinatoka wapi?
Kwa kila hali na kila jinsi hakuna wa kuzuia ushindi wenu hapo kesho. Hata kutangazwa kwenu hakuna wa kukuzuia. CCM tayari wanakiri kwa vitendo kulipoteza Jimbo la Igunga. Kila walifanyalo linaonyesha kuchanganyikiwa na kuishiwa kabisa mbinu. Wamebaki kulaumiana tu.
Hapo kesho nitarudi hapa kuja kuweapongeza rasmi CHADEMA maana Ushindi Wenu ni Ushindi Sote Watanzania.
Mungu aendelee kuwa nanyi katika kumalizia ngwe ya mwisho, Amen
Kama umati huu wote wanasifa za kupiga kura na wakapiga kura kesho basi jimbo hili chadema italichukua......
Kwa ukumbusho; CDM tayari mmeshinda propaganda ya kummwagia kijana wa ccm tindikali, kuchoma nyumba na ofisi za ccm na makada wao, kuingiza makomandoo kutoka nje ya nchi na mengine mengi. Na pia mmevuka mstari kwa kuweza kueleweka na kukubalika kwa kiasi kikubwa vijijini tofauti na chaguzi zilizopita. Mjini tayari mmekwishashinda.
Ushindi wenu wa kesho una maana kubwa sana kwa Taifa hili. Maana zaidi ya ile ionekanayo machoni na labda pia itakayojulikana na wanaochukulia mambo kijuujuu. Ushindi wenu utamaanisha makubwa yafuatayo:
- Kwamba Watanzania hawagawanyiki tena kwa misingi ya UDINI. Watanzania lao ni moja; siasa za kweli kutafuta haki na maendeleo
- Kuwa Waumini wanajua misingi imara ya dini zao na hawakotayari kumuunga mkono mtu katika ukengeufu wake eti tu kwa sababu ni wa dini yao
- Kifo cha mpango wa ccm kujivua Magamba (EL na AC watapona).
- Dhana ya kwamba vyama vya upinzani vya kisanii na vile vya upinzani9 wa kweli visiposhirikiana basi basi ccm ndo inapata mwanya wa ushindi
- Nguvu ya Dola kwa maana ya usalama wa Taifa na Polisi katika kunganganiza matopkeo ya uchaguzi imefika kikomo.
- Utamaanisha sasa, si kwamba mko tayari tu, bali ccm haiwezi tena kuwazuia kuingia Ikuli mwaka 2015
Ila sijapendezwa na dau mnalotoa CDM kwa watu wa Usalama wa Taifa wanaowapigia simu na kuwapa taarifa za uhakika. Wakati nina taarifa za uhakika ccm kutumia zaidi ya bilioni 4 katika uchaguzi huu lazima pia tujue nanyi mmetumia ngapi na zinafadhiriuwa na nani? Za ccm tunafahamu ni za ufisadi na zinatolewa na magamba, zenu ninyi mnapewa na nani na zinatoka wapi?
Kwa kila hali na kila jinsi hakuna wa kuzuia ushindi wenu hapo kesho. Hata kutangazwa kwenu hakuna wa kukuzuia. CCM tayari wanakiri kwa vitendo kulipoteza Jimbo la Igunga. Kila walifanyalo linaonyesha kuchanganyikiwa na kuishiwa kabisa mbinu. Wamebaki kulaumiana tu.
Hapo kesho nitarudi hapa kuja kuweapongeza rasmi CHADEMA maana Ushindi Wenu ni Ushindi Sote Watanzania.
Mungu aendelee kuwa nanyi katika kumalizia ngwe ya mwisho, Amen
Picha za mkutano wa chadema leo uliofunika mikutano yote ya igunga iliyofanyika leo
Kama umati huu wote wanasifa za kupiga kura na wakapiga kura kesho basi jimbo hili chadema italichukua......