Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Wakuu,
Leo chama cha Chadema walikuwa na mkutano wao wa kampeini katika kata ya BILELE katika eneo la nje ya Soko kuu ambapo watu walijaa sana na kulazimika kuifunga barabara ya Jamhuri kwa masaa kadhaa.
Katika Mkutano huu Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho jimbo la Nkenge alikuwepo kuwaondoa wasi wasi wana Chadema kwamba amejiondoa. Amesema yeye bado ni mgombea wa jimbo hilo na ana hakika ya kwenda mujengo Dodoma.
Katika mkutano huu pia Chadema imemnadi mgombea udiwani kata hiyo ya Bilele kwa tiketi ya CUF Mr.Mabruk Ibrahim Idd kama mtu anayefaa kuwa mwakilishi. Lwakatare aliomba wapiga kura wa kata hilo wampe kura zao zote maana ndiye mgombea pekee anayefaa.
Wagombea wa Chadema, kutoka kulia, Mi Ikengya mgombea udiwani kata ya Kashai, Phocas Rwegasira mgombea wa Nkenge na Lwakatare mgombea wa Bukoba mjini.
Inaelekea wanamwambia Lwakatare "tutakupa kura zetu zote"
Lwakatare akihutubia
Sehemu ya umati wa watu waliokuwepo kuwasikiliza wagombea.
Phocas Rwegasira mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jimbo la Nkenge akisalimia wananchi.
Leo chama cha Chadema walikuwa na mkutano wao wa kampeini katika kata ya BILELE katika eneo la nje ya Soko kuu ambapo watu walijaa sana na kulazimika kuifunga barabara ya Jamhuri kwa masaa kadhaa.
Katika Mkutano huu Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho jimbo la Nkenge alikuwepo kuwaondoa wasi wasi wana Chadema kwamba amejiondoa. Amesema yeye bado ni mgombea wa jimbo hilo na ana hakika ya kwenda mujengo Dodoma.
Katika mkutano huu pia Chadema imemnadi mgombea udiwani kata hiyo ya Bilele kwa tiketi ya CUF Mr.Mabruk Ibrahim Idd kama mtu anayefaa kuwa mwakilishi. Lwakatare aliomba wapiga kura wa kata hilo wampe kura zao zote maana ndiye mgombea pekee anayefaa.
Wagombea wa Chadema, kutoka kulia, Mi Ikengya mgombea udiwani kata ya Kashai, Phocas Rwegasira mgombea wa Nkenge na Lwakatare mgombea wa Bukoba mjini.
Inaelekea wanamwambia Lwakatare "tutakupa kura zetu zote"
Lwakatare akihutubia
Sehemu ya umati wa watu waliokuwepo kuwasikiliza wagombea.
Phocas Rwegasira mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jimbo la Nkenge akisalimia wananchi.