Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Wanabodi,
Ule mkutano kati ya Rais Jakaya Kikwete na Wazee wa Darisalaam, uliokuwa ufanyike leo, ukaahirishwa na kutangazwa ungefanyika kesho, umeahirishwa tena, sasa kufanyika Jumatatu!.
Taarifa toka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, iliyosomwa na TBC, imeeleza lengo la kusogezwa mbele mkutano huo, ni ili kutoa nafasi kwa Rais Kikwete, kujadiliana na wadau mbalimbali.
My Take!.
Nilipita mbele ya ukumbi Diamond, nikashuhudia masikini baadhi ya wabibi na wababu, walishajitanguliza mapema pale ukumbini, bila kujua mkutano umeahirishwa, na nadhani kulikuwa na ahadi ya kupeana japo nauli!, hivyo kujikuta hawana hili wa lile!.
Kuelezwa huelezwa kwa mdomo, lakini ahirisho ni kupitia electronic media, masikini wa watu, hawana redio wala TV, na siajabu kesho asubuhi, wengine wakadamkia Ukumbini!.
Naamini sababu kuu ya JK kutokutana na wazee hao, ni atakuwa ameisoma ile thread ya Mzee Mwanakijiji humu jukwaani na kuamua kuufuata ushauri wa JF!.
Kwa mliosoma baadhi ya sifa nzuri za JK ni "a good sense of humour", hivyo JK baada ya kusoma JF, akaamua kuwatafuta madaktari, aka wa 'charm' with a good sense of humour, kina Ulimboka wakalainika, kesho mtashuhudia wakimeza matapishi yao, kwa kutoa tamko la kuumaliza rasmi mgomo huo bila masharti yoyote!. JK atakapokutana na Wazee hiyo Jumatatu itakuwa ni kuwapatia tuu mrejesho!.
Hongera Mzee Mwanakijiji kwa kutoa angalizo muhimu!. Hongera JK kwa kumaliza kila kitu, na baada ya kina Ulimboka kuumaliza rasmi mgomo, Dr. Mponda na Dr. Nkya wajifungashie virago vyao na kujiondokea kwa amani na kwa heshima!.
Pasco.
Pasco unaongea kama unajua jambo fulani mkuu funguka usomeke JF kawaida hapa ni kufunguka kama una uhakika na unachosema