Mimi niliiona mkutano wa Arusha kwa luninga nikiwa Morogoro kupitia Star TV siku ya Ijumaa na Jumamosi. Bahati mbaya sauti haikutoka vizuri na haswa Jumamosi sauti haikusikika kabisa. Watu wengine niliongea nao wakiwa Dar walisema walikuwa wanasikia vizuri, sasa sijui kwa nini Morogoro sikuweza kupata sauti. Niliporudi Dar Jumapili tarehe 7 ndio ilikuwa siku ya mwisho, nilimsikia vizuri sana kupitia Star TV. Ujumbe mmoja wapo muhimu nilioupata ni kwamba kufanya dhambi huondoa uwepo wa Mwenyezi Mungu, hivyo tujitahidi kufanya maombi ya toba ili kuongeza uwepo wa utukufu wa BWANA.
Nilibahatika kumwona live kupitia star TV siku ya Jumamosi kulikuwepo na udhihirisho wa nguvu za Mungu usio wa kawaida.Mungu ambariki mtumishi wake huyu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.