Mkutano wa CHADEMA Arusha - Nov 29, 2013

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566
Mkutano wa chadema umeanza muda katika uwanja wa Ngarenaro, amezungumza Diwani Doita
anasema;
Halmashauri ya arusha imekuwa ikifanya mambo sivyo, kwa kuwa sasa ni katibu wa elimu na afya atashughulikia swala la rushwa hospitali, na michango mashuleni kwani kuna mil 900 iko haina kazi na sasa amemshauri mkurugenzi zika nunue madawati, yeye kama mwenyekiti hataki michango mashuleni, na wazazi msikubali kupitisha michango mbalimbali.

Doita anasema Sisi kama wanasiasa siyo kwamba tunaingilia walimu wakuu ila kwa hawa wanaokuja na njaa njaa zao tutapigana nao

Updates;
Anazungumza James Ole Milya, anasema chama kibaki kwa wananchi, hatuwezi kutaka magugu ndani ya ccm yatolewe wakati kwetu kuna magugu, tunatoa kwanza kwetu.

Milya anasema Simbachawene ni mpumba anaposema tutumie kibatari je computer, viwanda navyo vitumie vibatari, hili ni tatizo la kuweka waziri ambaye hata jimboni kwake hana umeme na hana uelewa anajua umeme ni kwaajili ya kuwasha taa..
Milya anasema sijutii kuondoka ccm, ninaomba kamati kuu tukaamshe vijijini..nina hasira na ccm na tukiwachekea watatumaliza, Mulongo ameendelea kuwa muongo, anasema baada ya div 5 wataenda mpaka div 7...

Ally Bananga anasema mfungwa anatamani kurudi gerezani, hawa mabwege wanafanya mabaya sana, ccm wajue wakitengeneza picha wajue watazanzania wanataka maji. Elimu bora,ajira kwa vijana..

Wanajamvi

Wakihutubia akiwemo Wakili James Milya, Madiwani, Viongozi wa CHADEMA ARUSHA Wameunga mkono kuvuliwa uanachama Zitto na Wenzake wakiwaita wasaliti, magugu,nk.

Hebu tujadili hoja aliyojenga pia Mhe Mbunge wa Lema katika hotuba yake kuwa mhe. Zitto ana Sifa ya kutokuwa mwanachama kutokana na usaliti, kuuza wagombea kwa ccm akirejea jimbo la mhe N. mkono na mambo aliyoshiriki na kushirikishwa ukiwemo waraka.

Wakati Kiongozi Golugwa amekiri wasaliti 4 ndo wamewakamata 46 watawanasa tu kwani walikuwa 50.

Je? ni kweli Mhe Zitto na Wenzake tuhuma 11 tusizo fahamu kwa sasa kwa tunazofahamu wameshiriki au wamehusishwa;

Zinatosheleza vigezo vya kutokuwa wanachama?

Kama wenzetu Waheshimiwa madiwani, Wabunge na Viongozi walivyotuhabarisha au kutuelimisha wanakosa sifa za kuendelea kuwa wanachama.

Source. Arusha mkutano wa madiwani na mbunge kwa Wananchi.

Naomba kuwasilisha.
Mbunge wa Arusha Mjini ambaye pia Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Mh Godbless Lema ameeleza kushangazwa sana na kinacholazimishwa na watu na viongozi wa CCM akiwemo Mwigulu Nchemba, January Makamba, Ridhiwani Kikwete na wengineo, kuwataka Chadema wapatane na kumrudishia vyeo Bw Zitto Kabwe.

Akiwahutubia wananchi wa Arusha jana viwanja vya Kilombero, Lema aliwaachia kama swali wananchi hao watafakari wenyewe kwamba "Migogoro ndani ya Chadema ni faida kwa CCM, sasa inakuwaje wanatamani Chadema wapatane!? Wanamaslahi gani na Upatanishao huo!?"

Katika mambo mengine Lema alisema pia kwamba tofauti na maigizo mengi ya waliovuliwa vyeo kuwa kuna watu wanachoma kadi na kutoa matamko wakisaidiwa na wanapropaganda wa CCM, ukweli ni kwamba wananchi wengi wanaipongeza Chadema kwa maamuzi ambayo hakuna chama kingine nchini kimeweza kufanya.

Sentensi nyingine alizonukuliwa Mh Lema ziko hivi..
" Wanasema Chadema itaparaganyika. Chadema haitaparaganyika kwa sababu ya migogoro. Chadema itaimarika kwasababu ya changamoto na migogoro"

"Hakuna mtu maarufu zaidi kuliko Chadema. Chadema ni maarufu kuliko kiongozi yeyote. Kama mtu ni maarufu, umaarufu wake utusaidie kuimarisha chama na sio kuua chama"

Lema alihitimisha hotuba yake kwa kuzungumzia mzaha wa Serikali katika swala la gharama za umeme nchini na kuwatupia lawama wananchi kuwa ndio wanaruhusu kuonewa siku zote. Alisema tabia ya watanzania kuonekana wameshazoea umasikini na matatizo ndio mambo yanayowapa jeuri watawala kuendelea kuwanyonya. Alitolea mfano wa mashine za risiti za TRA kuwa ni mradi wa kinyonyaji kwasabu bei wanayouzia ni mara kumi ya bei halisi, kitu alichodai ni makakati wa kuwaibia wananchi kutafuta hela za kampeni 2015.

Lema pia alizungumzia utapeli unaotaka kufanywa na Lowassa jijini hapa kuteka kiwanja cha umma akidaiwa anataka kukodi kufungua Car Wash lakini mpaka sasa ameshajenga uzio wa thamani ya milioni 500. Uzio wa tofali 500mil kwa Car Wash ya kukusanya elfu 80 kwa siku??

NENO LA AMANI GOLUGWA (KATIBU WA KANDA YA KASKAZINI)
Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara jana Nov 29, 2013 Ndg Amani Golugwa aliwataka wananchi na wapenzi wa Chadema kuwa wavulimivu, wawaamini viongozi na wawape ushirikiano kukijenga chama. Alisema mtaji mkubwa wa Kiongozi ndani ya Chadema ni UADILIFu na hivyo chama hakitasita kumuwajibisha yeyote yule bila kujali cheo chake endapo anakwenda kinyume na misingi ya chama.

Golugwa alisema kwa Chadema kipaumbele cha sasa ni ujenzi wa chama kuanzia ngazi yamsingi na hivyo kuomba ushirikiano na wala wananchi wasihuzunishe na maamuzi ya chama chao maana inalazimu kufanya hivyo ili chama kiimarike.

Aliwashangaa wale waliovuliwa vyeo kuhaha kutoa matamko na kushangazwa na utetezi wao aliouita wa kijinga kuwa eti waliandaa mkakati ili waje wamshirikishe Zitto. Golugwa akahoji ni kiherehere gani kimewakumba kumuhangaikia mwanaume mwenzao kama kweli hawajui anahitaji ama la!?

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Arusha kilifanya mkutano wa hadhara eneo la Kilombero uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi ambao muda wote walikuwa wakikatisha hotuba za viongozi kwa kushangilia na kupandishia maneno yao. Mkutano huo ulihudhuriwa na madiwani karibu wote wa Chadema Arusha pamoja na Naibu Meya Msofe, huku viongozi mbalimbali wa Wilaya na Mkoa wakiwa miongoni mwao bila kuwasahau makamanda wengine kama Ally Bananga n.k!

View attachment 124023
Amani Golugwa Jukwaani

View attachment 124024
Ally Bananga jukwaa kuu
View attachment 124026
Naibu Meya, Diwani wa Daraja Mbili Mh Msofe akiteta na wadau
View attachment 124030
 
Updates
Mh Nanyaro anawashukuru wana wa Arusha kwa kuwaongezea madiwani, hivi sasa maamuzi mengi halmashauri, yanafanywa na Cdm, sasa wameweza kujenga madarasa 52 kwa hela za halmashauri,
Anamtambulisha naibu meya Msofe na kusema hadi sasa hakuna muafaka na ccm kuhusu meya ila kuna naibu meya aliyechaguliwa na vyama vyote
 
Chadema Daima
Suala la Viongozi watimuliwa nalo pia litolewe ufafanuzi ili kukanusha habar ziziso za kweli.
 
Watu kila siku wanachangia harusi halafu anakuja mwanasiasa anawakataza kuchagia elimu!

Hivi elimu na harusi kipi muhimu?

Chadema sifuri kabisa...

Hapa hadanganywi mtu.
Kodi wananchi wanatoa kwa ajili ya Maendeleo ya Taifa,Na sio kila siku michango Sifuri ni ccm haijui kuchambua sera.
 
Bananga Anasema kama tuko kwenye mtungi halafu mwenzetu kwa kuwa ana kiu anaamua kutoboa mtumbwi ili amwenye maji, uki maliza maji si mtubwi utazama sasa sisi hatukubali atazama mwenyewe..
 
Nanyaro anazungumza anasema yeye anajikita kwenye matatu..hakuna mtoto atakae baki nyumbani eti madarasa yamejaa, tumejenga madarasa 51, hakuna mzazi kuchangishwa, 2. Natangaza hivi arusha mjini tuna naibu meya alie chaguliwa na vyama vyote
 
Nanyaro;
Hatuna mwafaka na ccm yaani na hatuwezi kuingia na mwafaka na meya fake ambaye amekali kiti chenye damu..hivyo kuanzia sasa naibu meya ndiyo meya wetu, na kwa muda mchache na usimamizi tulioufanya kwenye barabara mpaka pesa ikabaki hivyo wafadhili wamefurahi na wametuongeza bilion 20 na pesa hizi zitajenga brbr ya ungaltd mpaka dampo, sombetini, njiro, kaloleni..jiji liko chini ya chadema maana tumewazi hata huyo meya fake juzi alishindwa kuongea kiingereza...
 
Nanyaro;
Uwanja ulioko karibu na shoprite unarudishwa kwa wananchi kuanzia mwakani tutafanyia mikutano pale..wrong parking akiendelea kutuzingua tutamng'o..
 
Tunaomba uwakumbushe kutolea ufafanuzi mambo yafuatayo.

Chama kina kopesha wana chama wake?

Wanao kopeshwa wanarudisha na riba?

Ni lini chama kitajenga makao makuu na kuondokana na swala la kupangisha.

Ni kipengele kipi kwenye katiba ya chadema kina ruhusu mwanachama kumpiga tofali la kichwa mwanachama mwenzie anapo kosea?

Pesa wanazo changa wananchi zina kwenda wapi mbona huko mikoani hakuna ofisi?

Chama kipo tayari kuendelea kutonywa kinapo taka kufanyiwa ukaguzi wa pesa za wananchi?

cc Godbless J Lema
Henry Kilewo
Joshua nasary
 
Last edited by a moderator:
Nanyaro;
Wafanyabiashara wanatakiwa kutozwa usafi katikati ya mji ni 500 na siyo 10,000/=
 
Hakikisheni wasaliti wote Yuda Iskaryote tupa kule waende kwa masisiem yanayowatuma kuvuruga chama.
 
Watu kila siku wanachangia harusi halafu anakuja mwanasiasa anawakataza kuchagia elimu!

Hivi elimu na harusi kipi muhimu?

Chadema sifuri kabisa...

Kuna diwani mmoja wa upinzani mjinga sana kule morogoro alipanda majukwaani na kubabaika hivyohivyo @ wazazi msilipe michango yeyote na mwisho akasusiwa mashule yote ya kata yake kama sio mkuu wa wilaya kuingilia kati wale wanafunzi na wazazi wao waliodanganywa wangejuta sana. Watu hawa ni wa kuwapuuza tu.
 
Tunaomba uwakumbushe kutolea ufafanuzi mambo yafuatayo.

Chama kina kopesha wana chama wake?

Wanao kopeshwa wanarudisha na riba?

Ni lini chama kitajenga makao makuu na kuondokana na swala la kupangisha.

Ni kipengele kipi kwenye katiba ya chadema kina ruhusu mwanachama kumpiga tofali la kichwa mwanachama mwenzie anapo kosea?

Pesa wanazo changa wananchi zina kwenda wapi mbona huko mikoani hakuna ofisi?

Chama kipo tayari kuendelea kutonywa kinapo taka kufanyiwa ukaguzi wa pesa za wananchi?

cc Godbless J Lema
Henry Kilewo
Joshua nasary

Wao si wako safi sasa wanalialia kutonywa ili kuficha mvunguni madhaifu gani kama sio ulaghai huu.
 
Last edited by a moderator:
Watu kila siku wanachangia harusi halafu anakuja mwanasiasa anawakataza kuchagia elimu!

Hivi elimu na harusi kipi muhimu?

Chadema sifuri kabisa...

kuna milioni 900 hazina kazi pale manispaa, zitachangia elimu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom