Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Imefahamika kuwa kila matawi mawili ya CCM katika Jiji la Dar es salaam yatapatiwa basi moja, iwapo wangepeleka ombi lao kabla ya leo (Ijumaa) saa 7. Ili kufanikisha mkakati huo wa kutoa usafiri, makada wenye mabasi na malori wametakiwa kujitolea magari yao, ukiwa kama mchango wao kwa Chama. Aidha, viongozi wote wa mashina, vitongoji, mitaa, kata, wilaya na mkoa, kwa tiketi ya CCM wametakiwa kuhudhuria bila kukosa; labda kwa udhuru usioweza kuzuilika. Mitaa mingine wajumbe na wakereketwa wameombwa kuchangia walau shilingi elfu moja kwa ajili ya kukodi magari ya kuwapeleka na kuwarudisha mikutanoni.
Matawi yamehamasishwa kuandaa mabango yenye ujumbe wa kukiponda chama cha CHADEMA na vyama vya upinzani kwa ujumla.
Source: Rafiki yangu ambaye ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa (lakini anaipenda sana CHADEMA)
Matawi yamehamasishwa kuandaa mabango yenye ujumbe wa kukiponda chama cha CHADEMA na vyama vya upinzani kwa ujumla.
Source: Rafiki yangu ambaye ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa (lakini anaipenda sana CHADEMA)