Mkutano wa Biden na Xi: Dunia itarajie nini?

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,216
3,585
Marais wa dola mbili nguli wa siasa, uchumi na biashara, ulinzi na usalama; wenye nguvu za turufu duniani wamekutana kujadili mustakabali wa diplomasia baina yao zikiwemo agenda za mnyororo wa ugavi (biashara), hatima ya Taiwan, Olympics Beijing, muingiliano wa ki-uhamiaji, haki za binadamu, hali ya hewa duniani kufuatia COP26 Climate Summit in Glasgow, Scotland. Mkutano huo ulifanyika Jumatatu usiku 15 Novemba, 2021 kwa njia ya mtandao (virtual meeting).

Aidha, mkutano huo ulitazamiwa kurekebisha dosari za kidiplomasia zilizojiri wakati wa utawala wa Republican kupitia Rais Mstaafu Donald Trump dhidi ya Mamlaka ya Beijing hususan kwenye tasnia za biashara, afya (mlipuko wa kirusi cha Corona), upendeleo wa WHO kwa China dhidi ya US kwa habari ya Covid-19 nk. Dunia ilitega masikio kutaka kujuwa mustakabali wake wanapokutana mafahari hawa wawili.

Mataifa haya yana ushindani mkali wa kimaendeleo licha ya tofauti kubwa sana ya umri wao wa miaka 173 (zaidi ya karne moja na nusu) US miaka 245 na China miaka 72 (yaani China ilipata uhuru US ikiwa tayari ina miaka 173 ya uhuru), ambapo China imejituma kwa spidi kali hadi kuifikia US kimaendeleo. Bila shaka dunia inalo la kujifunza kwa China.

6f037c4288c9d7b96ab694534b65fda8
29415d66-bdb9-4138-9a58-693cfa987946_cx0_cy5_cw0_w1023_r1_s.jpg

Taswira kwa hisani ya Google
 
===
Kupunguza uwezekano wa kupigana
 
China ina miaka 72? acheni utani bwana sisi waislamu mtume wetu, Amesema tafuteni elimu mpaka China hio zaidi ya miaka 1400 iliopita.


Lunatic
 
China ina miaka 72? acheni utani bwana sisi waislamu mtume wetu, Amesema tafuteni elimu mpaka China hio zaidi ya miaka 1400 iliopita.


Lunatic
Ni ujinga Tu wa kutokujua naona China alikuwa na nguvu toka 1200 ndiye alikuwa na Dola kubwa eneo ya Asia nzima huu mradi WA belt road ulikuwa kwenye vitabu vyao toka miaka iyoo sema haukutekelezeka China imepitia vipindi vingi vya kiutawala
 
China ina miaka 72? acheni utani bwana sisi waislamu mtume wetu, Amesema tafuteni elimu mpaka China hio zaidi ya miaka 1400 iliopita.


Lunatic
The government of China considers October 1, 1949, as the date the country gained independence. This marks the date on which the People's Republic of China was established.

Source:

Nota Bene
1. That is the time from which Chinese sovereignty is counted. So go ask your Madrasa Teacher to calculate for you this simple arithmetic 2021 - 1949 (if he gives you the answer that is not 72 then abandon that religion)

2. Do you have any proof to establish that Mtume wako had at least a diploma (let alone a degree) in History? Avoid being irrational in the teachings of Madrasa. Mzee Mwinyi and Dr . Omar Ali Juma used to insist on the need of your religion community (theirs also) to pursue #elimudunia.

Mkuu, pole kumbe bado hujapona kifafa cha mimba?
 
The government of China considers October 1, 1949, as the date the country gained independence. This marks the date on which the People's Republic of China was established.

Source:

Nota Bene
1. That is the time from which Chinese sovereignty is counted. So go ask your Madrasa Teacher to calculate for you this simple arithmetic 2021 - 1949 (if he gives you the answer that is not 72 then abandon that religion)

2. Do you have any proof to establish that Mtume wako had at least a diploma (let alone a degree) in History? Avoid being irrational in the teachings of Madrasa. Mzee Mwinyi and Dr . Omar Ali Juma used to insist on the need of your religion community (theirs also) to pursue #elimudunia.

Mkuu, pole kumbe bado hujapona kifafa cha mimba?
Mnaongelea umri wa dola ya sasa ya China au taifa la China?
 
Mnaongelea umri wa dola ya sasa ya China au taifa la China?
Dola ya Kikomunisti ya sasa nchinu Uchina ilizaliwa mwaka 1949,
Lakini taifa la Uchina lilizaliwa miaka 6000 iliyopita, moja mataifa kongwe duniani,
Nchi ya Uchina imekuwa na madola tofauti yenye nguvu duniani kwa kipindi cha miaka tofauti tofauti.
Hahahahaaaaa.....

Mkuu, kimsingi kila dola ya sasa duniani ilikuwepo kabla ya uvamizi (hata km ilikuwepo km vidola vidogo vidogo).
Siyo kweli,.....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom