Naona anajaribu kujivimbisha mbele ya wahisani lakini bila kujiamini. Anaposema kwamba ushirikiano wa kupeana misaada kwa sasa umepitwa na wakati eti kwavile huzuia uhuru wa kisiasa kwa nchi za Afrika kujiamulia mambo yao wenyewe kwani hajui kwamba kuomba au kupokea misaada ya wahisani ni hiyari ya nchi zenyewe? Hivi ni huru gani wa kisiasa anaoulilia Rais Magufuli? Anataka kusiwe na mfumo wa vyama vingi na uchaguzi wa kidemokrasia?
Hata hivyo sidhani kwamba anachokisema anamaanisha kweli. Nasema hamaanishi kwasababu hatujawahi kusikia/kuona serikali anayoiongoza ikikataa misaada ya mabeberu. Sana sana tunasikia serikali imenyimwa misaada kwa sababu hizi na zile. Bali serikali yenyewe inapotokea kupewa msaada huchukulia kuwa ni "mafanikio ya jitihada za serikali ya awamu ya tano" na hutangaza kwenye kila chombo cha habari.
Ingawa Rais Magufuli anatamani nchi yake ijitegemee kiuchumi, hadi sasa bado anaonesha ameshindwa kuwa na mikakati sahihi ya kuitoa nchi kwenye utegemezi. Anachojua yeye ni kuorodhesha rasilimali za nchi na kujisifia kubarikiwa lakini hajui ni jinsi gani azitumie hizo rasilimali kujikuza kiuchumi. Mkakati pekee alionao wa kukuza uchumi ni kujenga mazingira bora ili kuwavutia wawekezaji (mabeberu). Kiufupi Magufuli hana jipya katika kukuza uchumi wa nchi.
Hata hivyo sidhani kwamba anachokisema anamaanisha kweli. Nasema hamaanishi kwasababu hatujawahi kusikia/kuona serikali anayoiongoza ikikataa misaada ya mabeberu. Sana sana tunasikia serikali imenyimwa misaada kwa sababu hizi na zile. Bali serikali yenyewe inapotokea kupewa msaada huchukulia kuwa ni "mafanikio ya jitihada za serikali ya awamu ya tano" na hutangaza kwenye kila chombo cha habari.
Ingawa Rais Magufuli anatamani nchi yake ijitegemee kiuchumi, hadi sasa bado anaonesha ameshindwa kuwa na mikakati sahihi ya kuitoa nchi kwenye utegemezi. Anachojua yeye ni kuorodhesha rasilimali za nchi na kujisifia kubarikiwa lakini hajui ni jinsi gani azitumie hizo rasilimali kujikuza kiuchumi. Mkakati pekee alionao wa kukuza uchumi ni kujenga mazingira bora ili kuwavutia wawekezaji (mabeberu). Kiufupi Magufuli hana jipya katika kukuza uchumi wa nchi.